Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Revelation

9

1O panshto angelo phurdia leski tuturaza. Dikhlem ek chererhai anda rhaio kai peli pe phuv. Ai ka leste sas dino e chaia ka o gropo (Abiss).
1Kisha malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la Kuzimu.
2Ai wo phuterdia o gropo ai thu avilo avri sar o thu katar o than kai si e bari iag. Ai o kham ai e barval aviline tuniariko katar o thu anda o gropo.
2Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la Kuzimu, kukatoka moshi wa tanuru kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa Kuzimu.
3Le sarancha hulenas tele pe phuv katar o thu. Won sas dine putiera sar le tsinorhe zhigeni kai pusavel.
3Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani wakapewa nguvu kama ya ng'e.
4Won sas phendo te na dukhaven e char vai zelene partia, vai kopachi, khash. Won sas te dukhaven ferdi le manush bi o semno le Devlesko pe lenge chikhaturia.
4Wakaamrishwa wasiharibu nyasi za nchi wala majani wala miti yoyote, bali wawaharibu wale tu ambao hawakupigwa mhuri wa Mungu katika paji la uso.
5Le sarancha nas te mudaren kodole manushen, numa won sas te den le bari dukh pala pansh shon. Ai e dukh sas sar avela katar ek tsinorhi zhigeni kai pusavel.
5Nzige hao hawakuruhusiwa kuwaua watu, ila kuwatesa tu kwa muda wa miezi mitano. Maumivu watakayosababisha ni kama maumivu yanayompata mtu wakati anapoumwa na ng'e.
6Le manush roden sar te meren ande kodola diesa, chi arakhen les. Won mangen te meren, numa e martia chi mekel le te meren.
6Muda huo watu watatafuta kifo lakini hawatakipata; watatamani kufa lakini kifo kitawakimbia.
7Le sarancha miazonas sar le gras kai zhan ka marimos. Sas vari so pe lenge shere kai miazolas e sumnakai konona, ai lenge mui miazol le muia le manushenge.
7Kwa kuonekana, nzige hao walikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita. Juu ya vichwa vyao walikuwa na taji zilizo kama za dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8Lenge bal sas sar le bal le zhuvliange ai lenge dand sas sar le dand le lionenge.
8Nywele zao zilikuwa kama nywele za wanawake, na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
9Sas pe lenge kolin sastrenge, ai o bunto katar lenge phaka sas sar o bunto katar but vurdona le but grastensa kai zhan ka marimos.
9Vifua vyao vilikuwa vimefunikwa kitu kama ngao ya chuma. Sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya msafara wa magari ya farasi wengi wanaokimbilia vitani.
10Sas le phoria sar ek tsinorhi zhegeni kai pusavel. E pusav avili katar lenge phoria. Ai lenge putiera sas te dukhaven le manushen pala pansh shon.
10Walikuwa na mikia na miiba kama ng'e, na kwa mikia hiyo, walikuwa na nguvu ya kuwadhuru watu kwa muda wa miezi mitano.
11Kadala sarancha sas le ek amperato. Wo si o angelo le gropomosko. Lesko anav ande Zhiduviska shib si Abbadon, numa ande Grekisko shib si Apollion.
11Tena wanaye mfalme anayewatawala, naye ndiye malaika wa kuzimu; jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki ni Apolioni, yaani mwangamizi.
12O pervo baio si gata. Ashun! Si mai dui te aven.
12Maafa ya kwanza yamepita; bado mengine mawili yanafuata.
13O shovto angelo phurdia leski tuturaza. Ashundem ek glaso kai avilo katar le shtar koltsuria le altareske o sumnakai angla O Del.
13Kisha malaika wa sita akapiga tarumbeta yake. Nami nikasikia sauti moja kutoka katika pembe nne za madhabahu ya dhahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.
14O glaso phendia ka o shovto angelo kai sas les e tuturaza, "Meken te zhan le shtar angeluria kai si phandade le lantsonsa ka o baro pai kai zhal Euphrates."
14Sauti hiyo ikamwambia huyo malaika wa sita mwenye tarumbeta, "Wafungulie malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Eufrate!"
15Won sas garade pala kodo chaso, ai dies, ai shon, ai bersh, ai sas mekle te zhan te mudaren e trito partia sa le manushenge kai traiin.
15Naye akawafungulia malaika hao wanne ambao walikuwa wametayarishwa kwa ajili ya saa hiyo ya siku ya mwezi huo, wa mwaka huohuo, kuua theluthi moja ya wanaadamu.
16E armia sas la dui shela miliwono ketani po grasten ai ashundem le kana phende sode zhene sas.
16Nilisikia idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa milioni mia mbili.
17Ande murho vizion, dikhlem le gras ai le manush pe lende, ai le manush ai le kotora sastri kai sas pe lenge kolin. Won sas loli sar iag, ai vunito sar o cheri, ai galbeno sar sulfer. Le shere le grastenge miazonas sar le shere le liononge. E iag ai thu ai sulfer avile anda lenge mui.
17Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika hiyo njozi: Walikuwa na ngao vifuani zilizokuwa moto mtupu, zenye rangi ya samawati na njano kama kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vya simba; na moto, moshi, na kiberiti vilikuwa vinatoka kinywani mwao.
18O trito partia anda sa le manushenge sas mudarde pala e iag ai thu ai sulfer kai avile anda lenge mui.
18Theluthi moja ya wanaadamu waliuawa kwa mabaa hayo matatu yaani, moto, moshi na kiberiti, yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vyao;
19E putiera le grastenge sas ande lenge mui ai ande lenge phoria. Lenge phoria sas sar le shere le sapenge kai dindaren ai mudaren.
19maana nguvu ya farasi hao ilikuwa vinywani mwao na katika mikia yao. Mikia yao ilikuwa na vichwa kama nyoka, na waliitumia hiyo kuwadhuru watu.
20Le manush kai traiinas inker pala kadala baiuria, chi keisaile, chi mekle le dieli kai kerde lenge vastensa, le ikoni kai sas kerde anda sumnakai, rup, xarkune, bax ai khash: kai nashtin te ashunen, dikhen, vai mishkin, vai phiren. Won chi aterdile te luvudin ai rhuginpe ka le dela le xoxamle, le bengen.
20Wanaadamu wengine waliobaki ambao hawakuuawa na mabaa hayo, hawakugeuka na kuviacha vitu walivyokuwa wametengeneza kwa mikono yao wenyewe; bali wakaendelea kuabudu pepo, sanamu za dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti, vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia wala kutembea.
21Won chi keisaile katar o mudarimos kai won kerenas, vai chi amboldinisaile katar o drabarimos, vai chi katar e kurvi, vai chi katar o chorimos.
21Wala hawakutubu na kuacha kufanya mauaji, uchawi, uzinzi, na wizi.