1Murhe phral, mange drago sa murhe ilesa, ai so mangav katar O Del le Zhidovonge si te aven skepime.
1Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
2Ke sai mothav pa lende ke sa penge ilesa mangen te keren buchi le Devleske, numa bi gojako.
2Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
3Ke chi haliarde sar O Del kerel le manushen te aven vorta angla leste, ai won rode te keren pengo zakono te aven vorta, ai kadia chi manglia te keren sar O Del kerel andal manush vorta.
3Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
4Ke o Kristosi kai getolpe o zakono te kerel te aven vorta angla Del kodola kai pachanpe.
4Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
5Eta so o Moses ramosardia pa sar sai te aves vorta angla Del trobul te les tu pala zokono, o manush kai lela pe pala zakono traiila katar kodo zakono.
5Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: "Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi."
6Numa eta, sar si phendo te sai aves vorta angla Del pala pachamos: na phen ande cho ilo, kon zhala ando rhaio?
6Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: "Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
7Kodia si te keres te hulel o Kristo. Ai chi na phen, kon zhala ande iado? Kodia si te keres te avel o Kristo palpale katar le mule.
7wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu)."
8So mothol kacha? E vorba pashe tute la ande cho mui, ai ande cho ilo:
8Maandiko Matakatifu yesema hivi, "Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako" nao ndio ile imani tunayoihubiri.
9kodia vorba si e viasta le pachamoski kai phenas, anda cho mui mothos angla savorhenge ke O Jesus si O Del, ai te pachasa tu ande cho ilo ke O Del andia les katar e martia ka traio, avesa skipime.
9Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
10Ke o manush pachalpe ande pesko ilo, ai O Del kerel les te avel vorta angla leste; o manush mothol peske muiesa, ai O Del skepil les.
10Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
11Ke E Vorba le Devleski mothol, kon godi pachalape ando Del chi avela leske lazhav.
11Maandiko Matakatifu yasema: "Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika."
12Le Zhiduvuria ai kodola kai Nai Zhiduvuria saikfialo le, savorhe si le iek Del kai del pesko mishtimos ka sa kodola kai akharen les.
12Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
13Kon godi kai akharel po anav le Devlesko avela skepime.
13Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa."
14Numa sar te akharena pe kodo kai chi pachaiepe ande leste? Ai sar te pachanpe ande kodo kai chi ashunde pa leste? Ai sar te ashunen pa leste kana nai khonik te mothol pa leste?
14Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
15Ai sar te avel manush kai den duma pa Del, te na avena tradine? Che shukar le punrhe kodolenge kai mothon pai pacha, ai kodola kai anen e lashi viasta!
15Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!"
16Numa chi linepe savorhe palai lashi viasta. o Esaiah mothol, "Devla, kon pachaiepe kana diam duma pa tute?"
16Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: "Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?"
17No antunchi o pachamos avel katar so ashunes, ai so ashunes avel katar E Vorba le Devleske.
17Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
18Numa me mothav, pate zhi ashunde e lashi viasta? E, ashunde la, lenge vorba ashundili pe sa e lumia.
18Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu."
19Numa me mothav, pate le Zhiduvuria chi zhanenas? o Moses o pervo phendia, kerava te avel tume xoli pe kodola kai nai chacho them, kerava te xolavon pek them kai nai gojaver.
19Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: "Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu."
20O Esaiah tromal te mothol mai but, "Arakhlema kodola kai chi rodenas ma; sikadilem kodolenge kai chi mangenas mandar kanchi.
20Tena Isaya anathubutu hata kusema: "Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu."
21Numa le Zhidovonge mothol, sorho dies vazdem le vas karing iek narodo kai chi pachal o mui ai kai chi mangen.
21Lakini kuhusu Israeli anasema: "Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii."