Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Romans

11

1Phushav tumen, O Del dia rigate peske narodos? Nichi, ke I me sim zhidovo andai vitsa le Abrahamoski, andal Benjamin.
1Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2O Del chi dia vov si rigate peske narodos kai zhanelas len mai anglal, pate chi zhanen so mothol E Vorba le Devleski pa Elijah? o Elijah mothol le Devleske ke le Zhiduvuria chi keren mishto. Phenelas,
2Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
3"Devla, mudarde le profeton, ai perade che altaria; me ashilem korkorho, ai roden te mudaren vi man."
3"Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?"
4Ai so phendia leske O Del, "Garadem mange efta mi zhene kai chi dine changa angla o xoxamlo del o Baal."
4Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: "Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali."
5Ai vi akana mai si xantsi narodo kai O Del alosardia len pala pesko lashimos.
5Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
6Alosardia le pala pesko lashimos, na ke won keren vari so mishto; ke antunchi o lashimos le Devlesko nas te avel chacho lashimos.
6Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
7So te mothas? So rodenas le Zhiduvuria chi line, ferdi kodolen kai alosardia O Del line so rodenas, le kolaver lengo ilo zurailo sas,
7Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
8Sar si ramome ande Vorbe le Devleski, O Del kerdia te sovel lenge goji, ai kerdia te na dikhen penge iakhensa, ai te na ashunen penge khanensa, zhi adies.
8kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao."
9O David mai mothol, "Lengi skafidi te avel lenge duzhmano, ai te peren, ai te pochinen o baio kai kerde.
9Naye Daudi anasema: "Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
10Lenge iakha te phandadion ai te na mai dikhen, ai ker te aven sagda lenge zea bange.
10Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!"
11Phushav, kana le Zhiduvuria pele, pele ai nashti mai vazden pe? Nichi, numa pala penge shipki, o kolaver narodo sai lia o skepimos, ai sai sikipin le Zhidovon.
11Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
12Te sas ke palai shipka le Zhidovongi. E lumia lia barvalimos ando Del, ai kai sas won mekle tele o kolaver narodo barvalo ando Del. Sode mai but avela kana dena pa savorhe ka Del?
12Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
13Me mothav tumenge ke chi san Zhiduvuria, me sim e sluga kai sas shinadi le narodoski kai Nai Zhiduvuria, ai kai sim kadia raduime sim anda kadia buchi kai sima.
13Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
14Ai te sai xoliarav te dashtiva murhe narodos kai si zhaluzo, ai te skepiv unen.
14nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
15E, kana sas thodine rigate e lumia kadia lashardili le Devlesa. So kerdiola kana lela le O Del pasha peste? Antunchi avela o traio kodolenge kai sas mule.
15Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
16Te si o pervo kotor le manrhesko andino angla Del, sa manrho antrego lesko si; te si le vuni la krenzhaki dine le Devleske, vi le krenzhi si leske.
16Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
17Le Zhiduvuria si sar iek khash maslenengo kai si lasharde, ai kai uni krenzhi sas shinde, tu kai chi san Zhidovo, tu san sar iek krenzha maslenengi chorhi thodino ando lengo than, ai tu akana les andai vuna kai pravarel le maslenen kai si lasharde.
17Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
18Anda kodia c hi trobul te avel tuke gratsia le krenzhi kai sas shinde. Sar te keres barimata? Ke chi san tu kai ingeres le vunen - numa le vuni ingeren tut.
18Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
19Amborim mothos mange, "Ke kodola krenzhi shinde sas katar o khash te avav me astardo ande lengo than."
19Lakini utasema: "Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake."
20E vorta, shinde sas kodola krenzhi katar o khash ke nas le dosta pachamos, ai tu san akana ande lengo than ke tu pachas tu. Numa arakh tu katar le barimata ai arakh tu.
20Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
21Ke te nas defial lasho O Del le Zhidovonsa kai si krenzhi lashe, chi tusa chi avela lasho.
21Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
22Le sama sar O Del sikavel pesko lashimos ai peske xoli, xoliariko lo pe kodola kai durile lestar, ai lasho lo tusa, numa trobul te beshes ande lesko lashimos; te na nichi, vi tu avesa shinado sar iek krenzha.
22Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
23Ai te mangena le Zhiduvuria te boldenpe karing mande, ai te pachanpe, aven astarde kotse kai sas astarde mai anglal, ke O Del si les e putiera te astarel le palpale.
23Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24Tu kai chi san Zhidovo, tu san ferdi iek krenzha ieke khashteske maslenengo chorho shinde la, ai astarde la kai chi trobulas pe iek khash maslenengo lashardo le Zhiduvuria, won si le krenzhi le chache kodole khashtesko maslenengo kai si lashardo, No avela but mai lioxo te astaras le pale po khash kai sas vunzhe mai anglal.
24Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
25Murhe phral, eta iek chachimos garado kai mangav te mothav tumenge. Saxke te na gindin ke gojaver san, uni andal Zhiduvuria nashtin te haliaren, numa kodia chi avela sagda, numa zhi kai le kolaver thema aven skepime.
25Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
26Ai eta, sa le Zhiduvuria avena skepime. Sar mothol Vorba le Devleske, "O skepitori avela anda Zion, ankalavela so godi si chorho andai vitsa le Iakovoske.
26Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: "Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
27Ai eta, so kerela lensa, kana lava le bezexa pa lende."
27Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao."
28Te dikhasa sar le Zhiduvuria chi mangle e lashi viasta, won si le duzhmaia le Devleske pe tumaro lashimos. Numa te dikhasa o alomos kai sas kerdo katar O Del, won si kodola kai O Del mangel pala lenge dada.
28Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
29Ke O Del chi lel palpale so dia, ai chi parhuvel pesko gindo karing kodola kai akhardia le.
29Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
30Mai anglal chi pachaian o mui le Devlesko, numa akana lian o lashimos le Devlesko ke le Zhiduvuria chi pachaie lesko mui.
30Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
31Ai vi chi pachaie le Devlesko mui, akana saxke o lashimos le Devlesko avel tumen dino, numa saxke vi won sai zhanen akana kodo lashimos.
31Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
32Ke O Del kerdia anda sako manush te avel phanglo ai te na pachal o mui, saxke te sikavel savorhenge pesko lashimos.
32Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote.
33Che baro lo o barvalimos le Devlesko, ai che bari leski goji ai sode zhanel, kon sai mothol so mangel te kerel O Del?
33Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
34Kon sai haliarela so mangel te kerel? "Kon zhanel o gindo le Devlesko?
34"Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
35Kon sai mothol leske so te kerel? Kon sas o pervo kai dia les vari so, ai porme te avel pochindo lestar?"
35Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?"
36Ke swako fialo avel katar O Del, swako fialo si pala leste, ai leske, ka Del te avel sa o barimos ande swako vriama! Amen.
36Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina.