Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Romans

3

1So mai niris te aves Zhidovo, o semno mai nai kanchi? But si te niris ande soste godi!
1Basi, Myahudi ana nini zaidi kuliko watu wengine? Au kutahiriwa kuna faida gani?
2Ai mai anglal kal Zhiduvuria O Del meklia kado divano.
2Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.
3Apo, so te mothos te sas mashkar lende kai chi kerde o zakono, O Del si te mekel le ke won mekle les?
3Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?
4Nichi! Trobul O Del te kerel buchi le chachimasa, marka te avela swako manush xoxamlo, sar mothol E Vorba le Devleski, trobul te arakhen ke vorta sam ande so mothos; ai te niris kana den tu pe kris.
4Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kila usemapo, maneno yako ni ya haki; na katika hukumu, wewe hushinda."
5Numa o bezex kai keres si te sikavel ke O Del vorta lo, so mothas ame? O Del nai vorta ke dosharel ame? Dav duma sar den duma le manush.
5Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).
6Nichi! Ke O Del te na avilino vorta, sar sai del pe kris la lumia?
6Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?
7Ai pala murho xoxaimos o chachimos le Devlesko sikadiol mai but pe lesko barimos; sostar te mai avav jindo sar iek bezexalo?
7Labda utasema: "Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!"
8Ai porme, sostar te na mothas, "Keras o bi lashimos saxke te anklel o lashimas." Chaches uni mothon bi lashimos pa mande ai dosharel ma ke sostar mothav, 'Kodola manush avena doshale sar trobul pe.'"
8Ni sawa na kusema: tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!
9Numa sam ame le Zhiduvuria mai lashe sar le kolaver manush? Nichi! Ke vunzhe phendem ke le Zhiduvuria ai le kolaver manush iek fialo le, ai savorhe bezexale le.
9Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora zaidi kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.
10Sar si ramome ande Vorba le Devleski, "Nai chi iek manush kai si vorta, nai, chi iek.
10Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!
11Chi iek kai haliarel, khonik chi rodel le Devles (Ps 14:2).
11Hakuna mtu anayeelewa, wala anayemtafuta Mungu.
12Savorhe xasarde le katar O Del; ai xasaile, nai chi iek kai kerel o mishtimos, chi iek.
12Wote wamepotoka wote wamekosa; hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja.
13Lenge kox si sar iek grepoäevo phuterdo, lenge shib si kai xoxaven lasa, le vorbi kai anklen anda lengo vursh si sar e votrava le sapesko; (Ps 5:9, 140:3).
13Makoo yao ni kama kaburi wazi, ndimi zao zimejaa udanganyifu, midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.
14Lengo mui pherdo bi vuzhimos ai den armaia.
14Vinywa vyao vimejaa laana chungu.
15Nashen zurales te mudaren:
15Miguu yao iko mbioni kumwaga damu,
16Ai katar godi nakhen, phagaven ai keren baio:
16popote waendapo husababisha maafa na mateso;
17Chi zhanen o drom la pachako,
17njia ya amani hawaijui.
18Nai dar le Devleski angla lenge iakha.
18Hawajali kabisa kumcha Mungu."
19Zhanas ke so godi mothol o zakono, mothol les kodolenge kai si tela zakono, saxke swako mui te avel phandado, ai sa e lumia te avel arakhli doshali angla Del.
19Tunajua kwamba Sheria huwahusu walio chini ya Sheria hiyo, hata hawawezi kuwa na kisingizio chochote, na ulimwengu wote uko chini ya hukumu ya Mungu.
20Ke khonik chi avela arakho vorta angla Del ke kerdia so motholas o zakono; o zakono si ferdi te sikavel le manusheske ke bezexalo lo.
20Maana hakuna binadamu yeyote anayekubaliwa kuwa mwadilifu mbele yake Mungu kwa kuishika Sheria; kazi ya Sheria ni kumwonyesha tu mtu kwamba ametenda dhambi.
21Numa akana O Del sikadia amenge sar kerel anda amende, vorta angla leste bi le zakonosko. o zakono ai le profeturia phende sas pa kadia diela.
21Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea Sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
22O Del kerel te aven le manush vorta ke pachanpe ando Jesus Kristo. Ai kodia si sa kodolenge kai pachanpe ando Kristo, ke angla Del savorhe iek fialo sam:
22Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
23Ke savorhe bezexale le, ai dur si katar lesko skepimos.
23Watu wote wametenda dhambi na wametindikiwa utukufu wa Mungu.
24Numa O Del ande pesko lashimos kerel te aven vorta ivia pala O Kristo Jesus, kai skepil le.
24Lakini kwa zawadi ya neema ya Mungu, watu wote hukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Yesu Kristo anayewakomboa.
25O Del thodia les po trushul, o iertimos le bezexengo avel pala o rat le Kristosko kana pachanpe ande leste, O Del manglia te sikavel sar pesko Shav O Jesus Kristo si chacho. Mai anglal, azhukerelas ai chi kerelas baio le bezexalenge;
25Mungu alimtoa Yesu kusudi, kwa damu yake, awe njia ya kuwaondolea watu dhambi zao kwa imani yao kwake. Alifanya hivyo ili apate kuonyesha kwamba yeye ni mwadilifu. Hapo zamani Mungu alikuwa mvumilivu bila kuzijali dhambi za watu;
26Numa akana O Del sikavel sar iertil le bezexa le manushenge te aven vorta. Ke wo mangel te sikavel kai wo si vorta, ai vi te kerel vorta anda sa kodola kai pachanpe ando Jesus.
26lakini sasa, wakati huu, anazikabili dhambi za watu apate kuonyesha uadilifu wake. Kwa namna hiyo Mungu mwenyewe huonyesha kwamba yeye ni mwadilifu na kwamba humkubali kuwa mwadilifu mtu yeyote anayemwamini Yesu.
27Mai si, le manushen, voia te keren barimata? Nichi, vov si! Si te keren so mothol o zakono? Nichi, Numa ke pachanpe ando Kristo.
27Basi, tunaweza kujivunia nini? Hakuna! Kwa nini? Je, kwa sababu ya kutimiza Sheria? La! Bali kwa sababu tunaamini.
28Ke ame gindisaras ke o manush vorta lo pala pesko pachamos bi te kerel so mothol o zakono.
28Maana mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa imani, wala si kwa kutimiza matakwa ya Sheria.
29O Del si ferdi O Del le Zhidovongo? Nai vi kodolengo kai Nai Zhiduvuria? E, wo si O Del kai Nai Zhiduvuria.
29Au je, Mungu nu Mungu wa Wayahudi tu, ama pia wa watu wa mataifa mengine? Naam, wa mataifa mengine pia.
30Ke ferdi iek Del si, kai kerela te aven vorta pala pachamos le Zhiduvuria, ai vi kodola kai Nai Zhiduvuria.
30Mungu ni mmoja, naye atawakubali Wayahudi kuwa waadilifu kwa imani yao, na watu wa mataifa mengine pia kwa imani yao.
31Apo, akana chi mai keras o zakono ke pala pachamos? Nichi, akana mai but te las ame.
31Je, tunaitumia imani kuibatilisha Sheria? Hata kidogo; bali tunaipa Sheria thamani yake kamili.