1Tarirai kuti rudo rwakadini Baba rwavakatipa, kuti tinzi vanakomana vaMwari; nekuda kwaizvozvi nyika haitizivi, nekuti haina kumuziva iye.
1Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
2Vadiwa, ikozvino tiri vana vaMwari, uye zvichigere kuonekwa kuti tichazovei. Asi tinoziva kuti kana achizoonekwa isu tichafanana naye; nekuti tichamuona sezvaakaita.
2Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
3Uye umwe neumwe une tariro iyi maari, unozvichenesa sezvaakachena iye.
3Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
4Umwe neumwe unoita chivi unodarika nomurairowo; nekuti chivi ndiko kudarika murairo.
4Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
5Munoziva kuti iye wakaratidzwa kuti abvise zvivi zvedu; uye maari hamuna zvivi.
5Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
6Ani nani unogara maari haatadzi; ani nani unotadza haana kumuona kana kumuziva.
6Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
7Vana vaduku, ngakurege kuva neunokunyengerai; uyo unoita kururama wakarurama, saiye akarurama.
7Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
8Uyo unoita chivi unobva kuna dhiabhorosi, nekuti dhiabhorosi unotadza kubva pakutanga. Mwanakomana waMwari wakaratidzwa nemhaka iyi kuti aparadze mabasa adhiabhorosi.
8Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
9Umwe neumwe wakaberekwa naMwari haaiti chivi, nekuti mbeu yake inogara maari, saka haangatadzi, nekuti wakaberekwa naMwari.
9Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
10Muna izvozvi vana vaMwari navana vadhiabhorosi vanoratidzwa; umwe neumwe usingaiti zvakarurama haabvi kuna Mwari, naiyewo usingadi hama yake.
10Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
11Nekuti iri ndiro shoko ramakanzwa kubva pakutanga, kuti tidanane;
11Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
12kwete saKaini, wakabva kuna iye wakaipa, akaponda munin'ina wake. Ko wakamuponderei? Nekuti mabasa ake akanga akaipa, asi omunin'ina wake akarurama.
12Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
13Musashamisika hama dzangu, kana nyika ichikuvengai.
13Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
14Tinoziva kuti takabva murufu tikapinda muupenyu, nekuti tinoda hama. Uyo, usingadi hama yake unogara murufu.
14Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
15Umwe neumwe unovenga hama yake imhondi; uye munoziva kuti hakuna mhondi ine upenyu hwusingaperi hwunogara mairi.
15Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake.
16Ndizvo zvatinoziva nazvo rudo, nekuti wakatiradzikira upenyu hwake; nesu tinofanira kuradzikira hama upenyu.
16Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
17Asi ani nani ane fuma yenyika ino asi achiona hama yake ichishaiwa, akamupfigira tsitsi dzake, rudo rwaMwari runogara seiko maari?
17Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
18Vana vangu vaduku, ngatirege kuda neshoko kana norurimi, asi muzviito nemuchokwadi.
18Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
19Ndizvo zvatinoziva nazvo kuti tiri vechokwadi, tigosimbisa moyo yedu pamberi pake.
19Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
20Nekuti kana moyo yedu ichitipa mhosva, Mwari mukuru kumoyo wedu, uye unoziva zvinhu zvose.
20Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
21Vadiwa, kana moyo wedu usingatipi mhosva, tine ushingi pamberi paMwari;
21Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
22uye zvose zvatinokumbira tinogamuchira kubva kwaari, nekuti tinochengeta mirairo yake, tichiita zvinhu zvinofadza pamberi pake.
22na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
23Uye uyu ndiwo murairo wake, kuti titende kuzita roMwanakomana wake Jesu Kristu, uye tidanane, sezvaakatipa murairo.
23Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
24Uye uyo unochengeta mirairo yake unogara maari, naiye maari. Ndizvo zvatinoziva nazvo kuti unogara matiri nomweya waakatipa.
24Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.