Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

1 Corinthians

1

1Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
1Paul, a called apostle of Jesus Christ, through the will of God, and Sosthenes the brother,
2tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
2to the assembly of God that is in Corinth, to those sanctified in Christ Jesus, called saints, with all those calling upon the name of our Lord Jesus Christ in every place — both theirs and ours:
3Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
3Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ!
4Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
4I give thanks to my God always concerning you for the grace of God that was given to you in Christ Jesus,
5Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
5that in every thing ye were enriched in him, in all discourse and all knowledge,
6kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
6according as the testimony of the Christ was confirmed in you,
7hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
7so that ye are not behind in any gift, waiting for the revelation of our Lord Jesus Christ,
8Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
8who also shall confirm you unto the end — unblamable in the day of our Lord Jesus Christ;
9Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
9faithful [is] God, through whom ye were called to the fellowship of His Son Jesus Christ our Lord.
10Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
10And I call upon you, brethren, through the name of our Lord Jesus Christ, that the same thing ye may all say, and there may not be divisions among you, and ye may be perfected in the same mind, and in the same judgment,
11Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
11for it was signified to me concerning you, my brethren, by those of Chloe, that contentions are among you;
12Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, "Mimi ni wa Paulo," mwingine: "Mimi ni wa Apolo," mwingine: "Mimi ni wa Kefa," na mwingine: "Mimi ni wa Kristo,".
12and I say this, that each one of you saith, `I, indeed, am of Paul` — `and I of Apollos,` — `and I of Cephas,` — `and I of Christ.`
13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
13Hath the Christ been divided? was Paul crucified for you? or to the name of Paul were ye baptized;
14Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
14I give thanks to God that no one of you did I baptize, except Crispus and Gaius —
15Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
15that no one may say that to my own name I did baptize;
16(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
16and I did baptize also Stephanas` household — further, I have not known if I did baptize any other.
17Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
17For Christ did not send me to baptize, but — to proclaim good news; not in wisdom of discourse, that the cross of the Christ may not be made of none effect;
18Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
18for the word of the cross to those indeed perishing is foolishness, and to us — those being saved — it is the power of God,
19Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali."
19for it hath been written, `I will destroy the wisdom of the wise, and the intelligence of the intelligent I will bring to nought;`
20Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
20where [is] the wise? where the scribe? where a disputer of this age? did not God make foolish the wisdom of this world?
21Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
21for, seeing in the wisdom of God the world through the wisdom knew not God, it did please God through the foolishness of the preaching to save those believing.
22Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
22Since also Jews ask a sign, and Greeks seek wisdom,
23lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
23also we — we preach Christ crucified, to Jews, indeed, a stumbling-block, and to Greeks foolishness,
24lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
24and to those called — both Jews and Greeks — Christ the power of God, and the wisdom of God,
25Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
25because the foolishness of God is wiser than men, and the weakness of God is stronger than men;
26Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
26for see your calling, brethren, that not many [are] wise according to the flesh, not many mighty, not many noble;
27Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
27but the foolish things of the world did God choose, that the wise He may put to shame; and the weak things of the world did God choose that He may put to shame the strong;
28Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
28and the base things of the world, and the things despised did God choose, and the things that are not, that the things that are He may make useless —
29Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
29that no flesh may glory before Him;
30Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
30and of Him ye — ye are in Christ Jesus, who became to us from God wisdom, righteousness also, and sanctification, and redemption,
31Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana."
31that, according as it hath been written, `He who is glorying — in the Lord let him glory.`