1Ndugu, mimi nilipokuja kwenu sikuwahubiria siri ya ujumbe wa Mungu kwa ufasaha wa lugha, au kwa hekima ya binadamu.
1And I, having come unto you, brethren, came — not in superiority of discourse or wisdom — declaring to you the testimony of God,
2Nilipokuwa kwenu niliamua kutojua chochote kile isipokuwa tu kumjua Yesu Kristo; naam, Kristo aliyesulubiwa.
2for I decided not to know any thing among you, except Jesus Christ, and him crucified;
3Nilipokuwa kwenu nilikuwa dhaifu, natetemeka kwa hofu nyingi.
3and I, in weakness, and in fear, and in much trembling, was with you;
4Hotuba zangu na mahubiri yangu sikuyatoa kwa maneno ya kuvutia na ya hekima, bali kwa uthibitisho mwingi na nguvu ya Roho.
4and my word and my preaching was not in persuasive words of human wisdom, but in demonstration of the Spirit and of power —
5Nilifanya hivyo kusudi imani yenu ipate kutegemea nguvu ya Mungu, na si hekima ya binadamu.
5that your faith may not be in the wisdom of men, but in the power of God.
6Hata hivyo, sisi tunatumia lugha ya hekima kwa wale waliokomaa kiroho; lakini hekima hiyo si ya hapa duniani, wala si ya watawala wa dunia hii ambao wako katika mkumbo wa kupotea.
6And wisdom we speak among the perfect, and wisdom not of this age, nor of the rulers of this age — of those becoming useless,
7Hekima tunayotumia ni hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichika, ambayo Mungu aliiazimia tangu mwanzo kwa ajili ya utukufu wetu.
7but we speak the hidden wisdom of God in a secret, that God foreordained before the ages to our glory,
8Ni hekima ambayo watawala wa dunia hii hawakuielewa; maana wangalielewa, hawangalimsulubisha Bwana wa utukufu.
8which no one of the rulers of this age did know, for if they had known, the Lord of the glory they would not have crucified;
9Lakini, ni kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mambo ambayo jicho halijapata kuyaona wala sikio kuyasikia, mambo ambayo binadamu hajapata kuyafikiria moyoni, hayo ndiyo Mungu aliyowatayarishia wale wampendao."
9but, according as it hath been written, `What eye did not see, and ear did not hear, and upon the heart of man came not up, what God did prepare for those loving Him —`
10Hayo ndiyo mambo Mungu aliyotufunulia kwa njia ya Roho wake. Maana Roho huchunguza kila kitu hata mambo ya ndani kabisa ya Mungu.
10but to us did God reveal [them] through His Spirit, for the Spirit all things doth search, even the depths of God,
11Nani awezaye kujua mambo ya ndani ya mtu isipokuwa roho yake mtu huyo? Hali kadhalika, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
11for who of men hath known the things of the man, except the spirit of the man that [is] in him? so also the things of God no one hath known, except the Spirit of God.
12Sasa sisi hatukuipokea roho ya ulimwengu, bali tumepokea Roho atokaye kwa Mungu ili atuwezeshe kujua yale tuliyojaliwa na Mungu.
12And we the spirit of the world did not receive, but the Spirit that [is] of God, that we may know the things conferred by God on us,
13Basi sisi twafundisha, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya binadamu, bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua mambo ya kiroho kwa walio na huyo Roho.
13which things also we speak, not in words taught by human wisdom, but in those taught by the Holy Spirit, with spiritual things spiritual things comparing,
14Mtu wa kidunia hapokei mambo ya Roho wa Mungu. Kwake mtu huyo mambo hayo ni upumbavu mtupu; yanapita akili yake; maana yanaweza tu kutambuliwa kwa msaada wa Roho.
14and the natural man doth not receive the things of the Spirit of God, for to him they are foolishness, and he is not able to know [them], because spiritually they are discerned;
15Lakini mtu aliye na huyo Roho anaweza kubainisha ubora wa kila kitu, naye mwenyewe hahukumiwi na mtu mwingine.
15and he who is spiritual, doth discern indeed all things, and he himself is by no one discerned;
16Maandiko yasema: "Nani awezaye kuifahamu akili ya Bwana? Nani awezaye kumshauri?" Lakini sisi tunayo akili ya Kristo.
16for who did know the mind of the Lord that he shall instruct Him? and we — we have the mind of Christ.