1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
1And I, brethren, was not able to speak to you as to spiritual, but as to fleshly — as to babes in Christ;
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
2with milk I fed you, and not with meat, for ye were not yet able, but not even yet are ye now able,
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
3for yet ye are fleshly, for where [there is] among you envying, and strife, and divisions, are ye not fleshly, and in the manner of men do walk?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
4for when one may say, `I, indeed, am of Paul;` and another, `I — of Apollos;` are ye not fleshly?
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
5Who, then, is Paul, and who Apollos, but ministrants through whom ye did believe, and to each as the Lord gave?
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
6I planted, Apollos watered, but God was giving growth;
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
7so that neither is he who is planting anything, nor he who is watering, but He who is giving growth — God;
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
8and he who is planting and he who is watering are one, and each his own reward shall receive, according to his own labour,
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
9for of God we are fellow-workmen; God`s tillage, God`s building ye are.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
10According to the grace of God that was given to me, as a wise master-builder, a foundation I have laid, and another doth build on [it],
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
11for other foundation no one is able to lay except that which is laid, which is Jesus the Christ;
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
12and if any one doth build upon this foundation gold, silver, precious stones, wood, hay, straw —
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
13of each the work shall become manifest, for the day shall declare [it], because in fire it is revealed, and the work of each, what kind it is, the fire shall prove;
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
14if of any one the work doth remain that he built on [it], a wage he shall receive;
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
15if of any the work is burned up, he shall suffer loss; and himself shall be saved, but so as through fire.
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
16have ye not known that ye are a sanctuary of God, and the Spirit of God doth dwell in you?
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
17if any one the sanctuary of God doth waste, him shall God waste; for the sanctuary of God is holy, the which ye are.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
18Let no one deceive himself; if any one doth seem to be wise among you in this age — let him become a fool, that he may become wise,
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
19for the wisdom of this world is foolishness with God, for it hath been written, `Who is taking the wise in their craftiness;`
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
20and again, `The Lord doth know the reasonings of the wise, that they are vain.`
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
21So then, let no one glory in men, for all things are yours,
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
22whether Paul, or Apollos, or Cephas, or the world, or life, or death, or things present, or things about to be — all are yours,
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.
23and ye [are] Christ`s, and Christ [is] God`s.