Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

1 Corinthians

10

1Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
1And I do not wish you to be ignorant, brethren, that all our fathers were under the cloud, and all passed through the sea,
2Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
2and all to Moses were baptized in the cloud, and in the sea;
3Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
3and all the same spiritual food did eat,
4wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
4and all the same spiritual drink did drink, for they were drinking of a spiritual rock following them, and the rock was the Christ;
5Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
5but in the most of them God was not well pleased, for they were strewn in the wilderness,
6Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
6and those things became types of us, for our not passionately desiring evil things, as also these did desire.
7Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: "Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza."
7Neither become ye idolaters, as certain of them, as it hath been written, `The people sat down to eat and to drink, and stood up to play;`
8Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
8neither may we commit whoredom, as certain of them did commit whoredom, and there fell in one day twenty-three thousand;
9Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
9neither may we tempt the Christ, as also certain of them did tempt, and by the serpents did perish;
10Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
10neither murmur ye, as also some of them did murmur, and did perish by the destroyer.
11Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili.
11And all these things as types did happen to those persons, and they were written for our admonition, to whom the end of the ages did come,
12Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
12so that he who is thinking to stand — let him observe, lest he fall.
13Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
13No temptation hath taken you — except human; and God is faithful, who will not suffer you to be tempted above what ye are able, but He will make, with the temptation, also the outlet, for your being able to bear [it].
14Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
14Wherefore, my beloved, flee from the idolatry;
15Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
15as to wise men I speak — judge ye what I say:
16Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
16The cup of the blessing that we bless — is it not the fellowship of the blood of the Christ? the bread that we break — is it not the fellowship of the body of the Christ?
17Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
17because one bread, one body, are we the many — for we all of the one bread do partake.
18Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
18See Israel according to the flesh! are not those eating the sacrifices in the fellowship of the altar?
19Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
19what then do I say? that an idol is anything? or that a sacrifice offered to an idol is anything? —
20Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
20[no,] but that the things that the nations sacrifice — they sacrifice to demons and not to God; and I do not wish you to come into the fellowship of the demons.
21Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
21Ye are not able the cup of the Lord to drink, and the cup of demons; ye are not able of the table of the Lord to partake, and of the table of demons;
22Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
22do we arouse the Lord to jealousy? are we stronger than He?
23Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
23All things to me are lawful, but all things are not profitable; all things to me are lawful, but all things do not build up;
24Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
24let no one seek his own — but each another`s.
25Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
25Whatever in the meat-market is sold eat ye, not inquiring, because of the conscience,
26maana Maandiko yasema: "Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana."
26for the Lord`s [is] the earth, and its fulness;
27Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
27and if any one of the unbelieving do call you, and ye wish to go, all that is set before you eat, nothing inquiring, because of the conscience;
28Lakini mtu akiwaambieni: "Chakula hiki kimetambikiwa sanamu," basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
28and if any one may say to you, `This is a thing sacrificed to an idol,` — do not eat, because of that one who shewed [it], and of the conscience, for the Lord`s [is] the earth and its fulness:
29Nasema, "kwa ajili ya dhamiri," si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: "Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
29and conscience, I say, not of thyself, but of the other, for why [is it] that my liberty is judged by another`s conscience?
30Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?"
30and if I thankfully do partake, why am I evil spoken of, for that for which I give thanks?
31Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
31Whether, then, ye eat, or drink, or do anything, do all to the glory of God;
32Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
32become offenceless, both to Jews and Greeks, and to the assembly of God;
33Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
33as I also in all things do please all, not seeking my own profit, but that of many — that they may be saved.