1Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
1Followers of me become ye, as I also [am] of Christ.
2Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
2And I praise you, brethren, that in all things ye remember me, and according as I did deliver to you, the deliverances ye keep,
3Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
3and I wish you to know that of every man the head is the Christ, and the head of a woman is the husband, and the head of Christ is God.
4Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
4Every man praying or prophesying, having the head covered, doth dishonour his head,
5Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
5and every woman praying or prophesying with the head uncovered, doth dishonour her own head, for it is one and the same thing with her being shaven,
6Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
6for if a woman is not covered — then let her be shorn, and if [it is] a shame for a woman to be shorn or shaven — let her be covered;
7Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
7for a man, indeed, ought not to cover the head, being the image and glory of God, and a woman is the glory of a man,
8Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
8for a man is not of a woman, but a woman [is] of a man,
9Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
9for a man also was not created because of the woman, but a woman because of the man;
10Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
10because of this the woman ought to have [a token of] authority upon the head, because of the messengers;
11Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
11but neither [is] a man apart from a woman, nor a woman apart from a man, in the Lord,
12Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
12for as the woman [is] of the man, so also the man [is] through the woman, and the all things [are] of God.
13Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
13In your own selves judge ye; is it seemly for a woman uncovered to pray to God?
14Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
14doth not even nature itself teach you, that if a man indeed have long hair, a dishonour it is to him?
15lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
15and a woman, if she have long hair, a glory it is to her, because the hair instead of a covering hath been given to her;
16Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
16and if any one doth think to be contentious, we have no such custom, neither the assemblies of God.
17Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
17And this declaring, I give no praise, because not for the better, but for the worse ye come together;
18Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
18for first, indeed, ye coming together in an assembly, I hear of divisions being among you, and partly I believe [it],
19maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
19for it behoveth sects also to be among you, that those approved may become manifest among you;
20Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
20ye, then, coming together at the same place — it is not to eat the Lord`s supper;
21Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
21for each his own supper doth take before in the eating, and one is hungry, and another is drunk;
22Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
22why, have ye not houses to eat and to drink in? or the assembly of God do ye despise, and shame those not having? what may I say to you? shall I praise you in this? I do not praise!
23Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
23For I — I received from the Lord that which also I did deliver to you, that the Lord Jesus in the night in which he was delivered up, took bread,
24akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: "Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
24and having given thanks, he brake, and said, `Take ye, eat ye, this is my body, that for you is being broken; this do ye — to the remembrance of me.`
25Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: "Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka."
25In like manner also the cup after the supping, saying, `This cup is the new covenant in my blood; this do ye, as often as ye may drink [it] — to the remembrance of me;`
26Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
26for as often as ye may eat this bread, and this cup may drink, the death of the Lord ye do shew forth — till he may come;
27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
27so that whoever may eat this bread or may drink the cup of the Lord unworthily, guilty he shall be of the body and blood of the Lord:
28Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
28and let a man be proving himself, and so of the bread let him eat, and of the cup let him drink;
29maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
29for he who is eating and drinking unworthily, judgment to himself he doth eat and drink — not discerning the body of the Lord.
30Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
30Because of this, among you many [are] weak and sickly, and sleep do many;
31Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
31for if ourselves we were discerning, we would not be being judged,
32Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
32and being judged by the Lord, we are chastened, that with the world we may not be condemned;
33Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
33so then, my brethren, coming together to eat, for one another wait ye;
34Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.
34and if any one is hungry, at home let him eat, that to judgment ye may not come together; and the rest, whenever I may come, I shall arrange.