1Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
1And concerning the spiritual things, brethren, I do not wish you to be ignorant;
2Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
2ye have known that ye were nations, unto the dumb idols — as ye were led — being carried away;
3Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: "Yesu alaaniwe!" Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: "Yesu ni Bwana," asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
3wherefore, I give you to understand that no one, in the Spirit of God speaking, saith Jesus [is] anathema, and no one is able to say Jesus [is] Lord, except in the Holy Spirit.
4Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.
4And there are diversities of gifts, and the same Spirit;
5Kuna namna nyingi za kutumikia, lakini Bwana anayetumikiwa ni mmoja.
5and there are diversities of ministrations, and the same Lord;
6Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.
6and there are diversities of workings, and it is the same God — who is working the all in all.
7Kila mtu hupewa mwangaza wa Roho kwa faida ya wote.
7And to each hath been given the manifestation of the Spirit for profit;
8Roho humpa mmoja ujumbe wa hekima, na mwingine ujumbe wa elimu apendavyo Roho huyohuyo.
8for to one through the Spirit hath been given a word of wisdom, and to another a word of knowledge, according to the same Spirit;
9Roho huyohuyo humpa mmoja imani, na humpa mwingine kipaji cha kuponya;
9and to another faith in the same Spirit, and to another gifts of healings in the same Spirit;
10humpa mmoja kipaji cha kufanya miujiza, mwingine kipaji cha kusema ujumbe wa Mungu, mwingine kipaji cha kubainisha vipaji vitokavyo kwa Roho na visivyo vya Roho; humpa mmoja kipaji cha kusema lugha ngeni, na mwingine kipaji cha kuzifafanua.
10and to another in-workings of mighty deeds; and to another prophecy; and to another discernings of spirits; and to another [divers] kinds of tongues; and to another interpretation of tongues:
11Hizo zote ni kazi za Roho huyohuyo mmoja, ambaye humpa kila mtu kipaji tofauti, kama apendavyo mwenyewe.
11and all these doth work the one and the same Spirit, dividing to each severally as he intendeth.
12Kama vile mwili ulivyo mmoja wenye viungo vingi, na viungo hivyo vyote--ingawaje ni vingi--hufanya mwili mmoja, ndivyo ilivyo pia kwa Kristo.
12For, even as the body is one, and hath many members, and all the members of the one body, being many, are one body, so also [is] the Christ,
13Maana sisi, tukiwa Wayahudi au watu wa mataifa mengine, watumwa au watu huru, sote tumebatizwa kwa Roho mmoja katika mwili huo mmoja; na sote tukanyweshwa Roho huyo mmoja.
13for also in one Spirit we all to one body were baptized, whether Jews or Greeks, whether servants or freemen, and all into one Spirit were made to drink,
14Mwili hauna kiungo kimoja tu, bali una viungo vingi.
14for also the body is not one member, but many;
15Kama mguu ungejisemea: "Kwa kuwa mimi si mkono, basi mimi si mali ya mwili", je, ungekoma kuwa sehemu ya mwili? La hasha!
15if the foot may say, `Because I am not a hand, I am not of the body;` it is not, because of this, not of the body;
16Kama sikio lingejisemea: "Kwa vile mimi si jicho, basi mimi si mali ya mwili", je, kwa hoja hiyo lingekoma kuwa sehemu ya mwili? La!
16and if the ear may say, `Because I am not an eye, I am not of the body;` it is not, because of this, not of the body?
17Kama mwili wote ungekuwa jicho, sikio lingekuwa wapi? Na kama mwili wote ungekuwa sikio, mtu angewezaje kunusa?
17If the whole body [were] an eye, where the hearing? if the whole hearing, where the smelling?
18Lakini kama ilivyo, Mungu alizipanga sehemu hizo tofauti katika mwili kama alivyopenda.
18and now, God did set the members each one of them in the body, according as He willed,
19Kama sehemu zote zingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
19and if all were one member, where the body?
20Ukweli ni kwamba, sehemu za mwili ni nyingi, lakini mwili ni mmoja.
20and now, indeed, [are] many members, and one body;
21Basi, jicho haliwezi kuuambia mkono: "Sikuhitaji wewe", wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: "Siwahitaji ninyi."
21and an eye is not able to say to the hand, `I have no need of thee;` nor again the head to the feet, `I have no need of you.`
22Zaidi ya hayo, inaonekana kwamba sehemu zile za mwili zinazoonekana kuwa ni dhaifu ndizo zilizo muhimu zaidi.
22But much more the members of the body which seem to be more infirm are necessary,
23Tena, viungo vile tunavyovifikiria kuwa havistahili heshima kubwa, ndivyo tunavyovitunza kwa uangalifu zaidi; viungo vya mwili ambavyo havionekani kuwa vizuri sana, huhifadhiwa zaidi,
23and those that we think to be less honourable of the body, around these we put more abundant honour, and our unseemly things have seemliness more abundant,
24ambapo viungo vingine havihitaji kushughulikiwa. Mungu mwenyewe ameuweka mwili katika mpango, akakipa heshima zaidi kiungo kile kilichopungukiwa heshima,
24and our seemly things have no need; but God did temper the body together, to the lacking part having given more abundant honour,
25ili kusiweko na utengano katika mwili bali viungo vyote vishughulikiane.
25that there may be no division in the body, but that the members may have the same anxiety for one another,
26Kama kiungo kimoja kinaumia viungo vyote huumia pamoja nacho. Kiungo kimoja kikisifiwa viungo vingine vyote hufurahi pamoja nacho.
26and whether one member doth suffer, suffer with [it] do all the members, or one member is glorified, rejoice with [it] do all the members;
27Basi, ninyi nyote ni mwili wa Kristo; kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.
27and ye are the body of Christ, and members in particular.
28Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu; kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia; viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
28And some, indeed, did God set in the assembly, first apostles, secondly prophets, thirdly teachers, afterwards powers, afterwards gifts of healings, helpings, governings, divers kinds of tongues;
29Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni walimu? Wote ni wenye kipaji cha kufanya miujiza?
29[are] all apostles? [are] all prophets? [are] all teachers? [are] all powers?
30Je, wote ni wenye kipaji cha kuponya? Wote ni wenye kipaji cha kusema lugha ngeni? Je, wote hufafanua lugha?
30have all gifts of healings? do all speak with tongues? do all interpret?
31Muwe basi, na tamaa ya kupata vipaji muhimu zaidi. Nami sasa nitawaonyesheni njia bora zaidi kuliko hizi zote.
31and desire earnestly the better gifts; and yet a far excelling way do I shew to you: