Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

1 Corinthians

13

1Hata kama nikinena lugha za watu na hata za malaika, lakini kama sina upendo mimi nimekuwa tu kama sauti ya debe tupu au kengele.
1If with the tongues of men and of messengers I speak, and have not love, I have become brass sounding, or a cymbal tinkling;
2Tena, naweza kuwa na kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, nikafahamu siri zote na kujua kila kitu; naweza kuwa na imani yote hata nikaweza kuihamisha milima, lakini kama sina upendo mimi si kitu.
2and if I have prophecy, and know all the secrets, and all the knowledge, and if I have all the faith, so as to remove mountains, and have not love, I am nothing;
3Nikitoa mali yangu yote na kuwapa maskini, na tena nikiutoa mwili wangu uchomwe, kama sina upendo hiyo hainifai chochote.
3and if I give away to feed others all my goods, and if I give up my body that I may be burned, and have not love, I am profited nothing.
4Mwenye upendo huvumilia, hufadhili; mwenye upendo hana wivu, hajidai, wala hajivuni.
4The love is long-suffering, it is kind, the love doth not envy, the love doth not vaunt itself, is not puffed up,
5Mwenye upendo hakosi adabu, hatafuti faida yake binafsi, wala hana wepesi wa hasira; haweki kumbukumbu ya mabaya,
5doth not act unseemly, doth not seek its own things, is not provoked, doth not impute evil,
6hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli.
6rejoiceth not over the unrighteousness, and rejoiceth with the truth;
7Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote.
7all things it beareth, all it believeth, all it hopeth, all it endureth.
8Upendo hauna kikomo kamwe. Kama kuna vipaji vya kutangaza ujumbe wa Mungu, hivyo vitatoweka siku moja; kama ni vipaji vya kusema lugha ngeni, vitakoma; kama kuna elimu, nayo itapita.
8The love doth never fail; and whether [there be] prophecies, they shall become useless; whether tongues, they shall cease; whether knowledge, it shall become useless;
9Maana ujuzi wetu si kamili, na kipaji chetu cha kutangaza neno la Mungu si kamili.
9for in part we know, and in part we prophecy;
10Lakini kile kilicho kikamilifu kitakapofika, vyote visivyo vikamilifu vitatoweka.
10and when that which is perfect may come, then that which [is] in part shall become useless.
11Nilipokuwa mtoto mchanga nilisema kitoto, nilifahamu kitoto, nilifikiri kitoto. Lakini sasa, maadam mimi ni mtu mzima, mambo ya kitoto nimeyaacha.
11When I was a babe, as a babe I was speaking, as a babe I was thinking, as a babe I was reasoning, and when I have become a man, I have made useless the things of the babe;
12Tunachoona sasa ni kama tu sura hafifu katika kioo, lakini hapo baadaye tutaona uso kwa uso. Sasa ninajua kiasi fulani tu, lakini hapo baadaye nitajua yote kikamilifu, kama vile Mungu anavyonijua mimi.
12for we see now through a mirror obscurely, and then face to face; now I know in part, and then I shall fully know, as also I was known;
13Sasa yanadumu haya matatu: imani, tumaini na upendo; lakini lililo kuu kupita yote ni upendo.
13and now there doth remain faith, hope, love — these three; and the greatest of these [is] love.