1Basi, Mungu, kwa huruma yake, ametukabidhi kazi hii na hivyo hatufi moyo.
1Because of this, having this ministration, according as we did receive kindness, we do not faint,
2Tumeyaacha kabisa mambo yote ya aibu na ya kisirisiri. Hatuishi tena kwa udanganyifu, wala kwa kulipotosha neno la Mungu; bali tunaudhihirisha ukweli kwa kuufanya ukweli, na hivyo kujiweka chini ya uamuzi wa dhamiri za watu mbele ya Mungu.
2but did renounce for ourselves the hidden things of shame, not walking in craftiness, nor deceitfully using the word of God, but by the manifestation of the truth recommending ourselves unto every conscience of men, before God;
3Maana, kama Habari Njema tunayohubiri imefichika, imefichika tu kwa wale wanaopotea.
3and if also our good news is vailed, in those perishing it is vailed,
4Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu.
4in whom the god of this age did blind the minds of the unbelieving, that there doth not shine forth to them the enlightening of the good news of the glory of the Christ, who is the image of God;
5Maana hatujitangazi sisi wenyewe, ila tunamhubiri Yesu Kristo aliye Bwana, sisi wenyewe tukiwa watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
5for not ourselves do we preach, but Christ Jesus — Lord, and ourselves your servants because of Jesus;
6Mungu ambaye alisema, "Mwanga na uangaze kutoka gizani," ndiye mwenye kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao katika uso wa Kristo.
6because [it is] God who said, Out of darkness light [is] to shine, who did shine in our hearts, for the enlightening of the knowledge of the glory of God in the face of Jesus Christ.
7Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu wala si kwetu sisi wenyewe.
7And we have this treasure in earthen vessels, that the excellency of the power may be of God, and not of us;
8Daima twapata taabu, lakini hatugandamizwi; twapata mashaka, lakini hatukati tamaa;
8on every side being in tribulation, but not straitened; perplexed, but not in despair;
9twateseka, lakini hatuachwi bila msaada; na ingawa tumeangushwa chini, hatukuangamizwa.
9persecuted, but not forsaken; cast down, but not destroyed;
10Kila wakati tumekuwa tukichukua mwilini mwetu kifo cha Kristo, ili uhai wake Yesu pia udhihirike katika miili yetu.
10at all times the dying of the Lord Jesus bearing about in the body, that the life also of Jesus in our body may be manifested,
11Naam, katika maisha yetu yote tunakabiliwa na kifo daima kwa ajili ya Yesu, ili uzima wake Yesu udhihirike katika miili yetu inayokufa.
11for always are we who are living delivered up to death because of Jesus, that the life also of Jesus may be manifested in our dying flesh,
12Hii ina maana kwamba ndani yetu kifo kinafanya kazi, lakini ndani yenu uhai unafanya kazi.
12so that, the death indeed in us doth work, and the life in you.
13Maandiko Matakatifu yasema: "Niliamini, ndiyo maana nilinena." Nasi pia, tukiwa na moyo huohuo wa imani, tunaamini, na kwa sababu hiyo twanena.
13And having the same spirit of the faith, according to that which hath been written, `I believed, therefore I did speak;` we also do believe, therefore also do we speak;
14Tunajua kwamba yule aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuweka mbele yake pamoja nanyi.
14knowing that He who did raise up the Lord Jesus, us also through Jesus shall raise up, and shall present with you,
15Yote haya ni kwa faida yenu; ili kama vile neema ya Mungu inavyoenea kwa watu wengi zaidi na zaidi vivyo hivyo watu wengi zaidi watoe shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
15for the all things [are] because of you, that the grace having been multiplied, because of the thanksgiving of the more, may abound to the glory of God;
16Kwa sababu hiyo hatufi moyo; na hata kama maumbile yetu ya nje yataoza, lakini kwa ndani tunafanywa wapya siku kwa siku.
16wherefore, we faint not, but if also our outward man doth decay, yet the inward is renewed day by day;
17Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho.
17for the momentary light matter of our tribulation, more and more exceedingly an age-during weight of glory doth work out for us —
18Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele.
18we not looking to the things seen, but to the things not seen; for the things seen [are] temporary, but the things not seen [are] age-during.