Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

2 Corinthians

5

1Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono.
1For we have known that if our earthly house of the tabernacle may be thrown down, a building from God we have, an house not made with hands — age-during — in the heavens,
2Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
2for also in this we groan, with our dwelling that is from heaven earnestly desiring to clothe ourselves,
3Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
3if so be that, having clothed ourselves, we shall not be found naked,
4Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
4for we also who are in the tabernacle do groan, being burdened, seeing we wish not to unclothe ourselves, but to clothe ourselves, that the mortal may be swallowed up of the life.
5Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
5And He who did work us to this self-same thing [is] God, who also did give to us the earnest of the Spirit;
6Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
6having courage, then, at all times, and knowing that being at home in the body, we are away from home from the Lord, —
7Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
7for through faith we walk, not through sight —
8Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
8we have courage, and are well pleased rather to be away from the home of the body, and to be at home with the Lord.
9Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
9Wherefore also we are ambitious, whether at home or away from home, to be well pleasing to him,
10Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
10for all of us it behoveth to be manifested before the tribunal of the Christ, that each one may receive the things [done] through the body, in reference to the things that he did, whether good or evil;
11Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
11having known, therefore, the fear of the Lord, we persuade men, and to God we are manifested, and I hope also in your consciences to have been manifested;
12Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
12for not again ourselves do we recommend to you, but we are giving occasion to you of glorifying in our behalf, that ye may have [something] in reference to those glorifying in face and not in heart;
13Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
13for whether we were beside ourselves, [it was] to God; whether we be of sound mind — [it is] to you,
14Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
14for the love of the Christ doth constrain us, having judged thus: that if one for all died, then the whole died,
15Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
15and for all he died, that those living, no more to themselves may live, but to him who died for them, and was raised again.
16Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
16So that we henceforth have known no one according to the flesh, and even if we have known Christ according to the flesh, yet now we know him no more;
17Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
17so that if any one [is] in Christ — [he is] a new creature; the old things did pass away, lo, become new have the all things.
18Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
18And the all things [are] of God, who reconciled us to Himself through Jesus Christ, and did give to us the ministration of the reconciliation,
19Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
19how that God was in Christ — a world reconciling to Himself, not reckoning to them their trespasses; and having put in us the word of the reconciliation,
20Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
20in behalf of Christ, then, we are ambassadors, as if God were calling through us, we beseech, in behalf of Christ, `Be ye reconciled to God;`
21Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.
21for him who did not know sin, in our behalf He did make sin, that we may become the righteousness of God in him.