Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

2 Thessalonians

2

1Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
1And we ask you, brethren, in regard to the presence of our Lord Jesus Christ, and of our gathering together unto him,
2msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
2that ye be not quickly shaken in mind, nor be troubled, neither through spirit, neither through word, neither through letters as through us, as that the day of Christ hath arrived;
3Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
3let not any one deceive you in any manner, because — if the falling away may not come first, and the man of sin be revealed — the son of the destruction,
4Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
4who is opposing and is raising himself up above all called God or worshipped, so that he in the sanctuary of God as God hath sat down, shewing himself off that he is God — [the day doth not come].
5Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
5Do ye not remember that, being yet with you, these things I said to you?
6Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
6and now, what is keeping down ye have known, for his being revealed in his own time,
7Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
7for the secret of the lawlessness doth already work, only he who is keeping down now [will hinder] — till he may be out of the way,
8Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
8and then shall be revealed the Lawless One, whom the Lord shall consume with the spirit of his mouth, and shall destroy with the manifestation of his presence,
9Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
9[him,] whose presence is according to the working of the Adversary, in all power, and signs, and lying wonders,
10na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
10and in all deceitfulness of the unrighteousness in those perishing, because the love of the truth they did not receive for their being saved,
11Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
11and because of this shall God send to them a working of delusion, for their believing the lie,
12Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
12that they may be judged — all who did not believe the truth, but were well pleased in the unrighteousness.
13Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
13And we — we ought to give thanks to God always for you, brethren, beloved by the Lord, that God did choose you from the beginning to salvation, in sanctification of the Spirit, and belief of the truth,
14Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
14to which He did call you through our good news, to the acquiring of the glory of our Lord Jesus Christ;
15Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
15so, then, brethren, stand ye fast, and hold the deliverances that ye were taught, whether through word, whether through our letter;
16Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema,
16and may our Lord Jesus Christ himself, and our God and Father, who did love us, and did give comfort age-during, and good hope in grace,
17aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.
17comfort your hearts, and establish you in every good word and work.