Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

2 Thessalonians

3

1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
1As to the rest, pray ye, brethren, concerning us, that the word of the Lord may run and may be glorified, as also with you,
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
2and that we may be delivered from the unreasonable and evil men, for the faith [is] not of all;
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
3and stedfast is the Lord, who shall establish you, and shall guard [you] from the evil;
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
4and we have confidence in the Lord touching you, that the things that we command you ye both do and will do;
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
5and the Lord direct your hearts to the love of God, and to the endurance of the Christ.
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
6And we command you, brethren, in the name of our Lord Jesus Christ, to withdraw yourselves from every brother disorderly walking, and not after the deliverance that ye received from us,
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
7for yourselves have known how it behoveth [you] to imitate us, because we did not act disorderly among you;
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
8nor for nought did we eat bread of any one, but in labour and in travail, night and day working, not to be chargeable to any of you;
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
9not because we have not authority, but that ourselves a pattern we might give to you, to imitate us;
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
10for even when we were with you, this we did command you, that if any one is not willing to work, neither let him eat,
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
11for we hear of certain walking among you disorderly, nothing working, but over working,
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
12and such we command and exhort through our Lord Jesus Christ, that with quietness working, their own bread they may eat;
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
13and ye, brethren, may ye not be weary doing well,
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
14and if any one do not obey our word through the letter, this one note ye, and have no company with him, that he may be ashamed,
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
15and as an enemy count [him] not, but admonish ye [him] as a brother;
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
16and may the Lord of the peace Himself give to you the peace always in every way; the Lord [is] with you all!
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
17The salutation by the hand of me, Paul, which is a sign in every letter; thus I write;
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
18the grace of our Lord Jesus Christ [is] with you all! Amen.