Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

2 Timothy

2

1Basi, wewe mwanangu, uwe na nguvu katika neema tunayopata katika kuungana na Kristo Yesu.
1Thou, therefore, my child, be strong in the grace that [is] in Christ Jesus,
2Chukua yale mafundisho uliyonisikia nikitangaza mbele ya mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu wanaoaminika, ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
2and the things that thou didst hear from me through many witnesses, these things be committing to stedfast men, who shall be sufficient also others to teach;
3Shiriki katika mateso kama askari mwaminifu wa Kristo yesu.
3thou, therefore, suffer evil as a good soldier of Jesus Christ;
4Mwanajeshi vitani hujiepusha na shughuli za maisha ya kawaida ili aweze kumpendeza mkuu wa jeshi.
4no one serving as a soldier did entangle himself with the affairs of life, that him who did enlist him he may please;
5Mwanariadha yeyote hawezi kushinda na kupata zawadi ya ushindi kama asipozitii sheria za michezo.
5and if also any one may strive, he is not crowned, except he may strive lawfully;
6Mkulima ambaye amefanya kazi ngumu anastahili kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
6the labouring husbandman it behoveth first of the fruits to partake;
7Fikiria hayo ninayosema, kwani Bwana atakuwezesha uyaelewe yote.
7be considering what things I say, for the Lord give to thee understanding in all things.
8Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka wafu, aliyekuwa wa ukoo wa Daudi, kama isemavyo Habari Njema ninayoihubiri.
8Remember Jesus Christ, raised out of the dead, of the seed of David, according to my good news,
9Kwa sababu ya kuihubiri Habari Njema mimi nateseka na nimefungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu haliwezi kufungwa minyororo,
9in which I suffer evil -- unto bonds, as an evil-doer, but the word of God hath not been bound;
10na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele.
10because of this all things do I endure, because of the choice ones, that they also salvation may obtain that [is] in Christ Jesus, with glory age-during.
11Usemi huu ni wa kweli: "Ikiwa tulikufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
11Stedfast [is] the word: For if we died together -- we also shall live together;
12Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pia pamoja naye. Tukimkana, naye pia atatukana.
12if we do endure together -- we shall also reign together; if we deny [him], he also shall deny us;
13Tukikosa kuwa waaminifu, yeye hubaki mwaminifu daima, maana yeye hawezi kujikana mwenyewe."
13if we are not stedfast, he remaineth stedfast; to deny himself he is not able.
14Basi, wakumbushe watu wako mambo haya, na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.
14These things remind [them] of, testifying fully before the Lord -- not to strive about words to nothing profitable, but to the subversion of those hearing;
15Jitahidi kupata kibali kamili mbele ya Mungu kama mfanyakazi ambaye haoni haya juu ya kazi yake, na ambaye hufundisha sawa ule ujumbe wa kweli.
15be diligent to present thyself approved to God -- a workman irreproachable, rightly dividing the word of the truth;
16Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ya kipumbavu; kwani hayo huzidi kuwatenga watu mbali na Mungu.
16and the profane vain talkings stand aloof from, for to more impiety they will advance,
17Mafundisho ya aina hiyo ni kama donda linalokula mwili. Miongoni mwa hao waliofundisha hayo ni Humenayo na Fileto.
17and their word as a gangrene will have pasture, of whom is Hymenaeus and Philetus,
18Hawa wamepotoka kabisa mbali na ukweli, na wanatia imani ya watu wengine katika wasiwasi kwa kusema ati ufufuo wetu umekwisha fanyika.
18who concerning the truth did swerve, saying the rising again to have already been, and do overthrow the faith of some;
19Lakini msingi thabiti uliowekwa na Mungu uko imara, na juu yake yameandikwa maneno haya: "Bwana anawafahamu wale walio wake," na "Kila asemaye yeye ni wa Bwana, ni lazima aachane na uovu."
19sure, nevertheless, hath the foundation of God stood, having this seal, `The Lord hath known those who are His,' and `Let him depart from unrighteousness -- every one who is naming the name of Christ.'
20Katika nyumba kubwa kuna mabakuli na vyombo vya kila namna: vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine vya mbao na udongo, vingine ni vya matumizi ya pekee na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
20And in a great house there are not only vessels of gold and of silver, but also of wood and of earth, and some to honour, and some to dishonour:
21Basi, kama mtu atajitakasa kwa kujitenga mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee, kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa Bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.
21if, then, any one may cleanse himself from these, he shall be a vessel to honour, sanctified and profitable to the master -- to every good work having been prepared,
22Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.
22and the youthful lusts flee thou, and pursue righteousness, faith, love, peace, with those calling upon the Lord out of a pure heart;
23Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.
23and the foolish and uninstructed questions be avoiding, having known that they beget strife,
24Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,
24and a servant of the Lord it behoveth not to strive, but to be gentle unto all, apt to teach, patient under evil,
25ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.
25in meekness instructing those opposing -- if perhaps God may give to them repentance to an acknowledging of the truth,
26Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.
26and they may awake out of the devil's snare, having been caught by him at his will.