Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

2 Timothy

3

1Kumbuka kwamba, katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za taabu.
1And this know thou, that in the last days there shall come perilous times,
2watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu;
2for men shall be lovers of themselves, lovers of money, boasters, proud, evil-speakers, to parents disobedient, unthankful, unkind,
3watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia chochote kilicho chema;
3without natural affection, implacable, false accusers, incontinent, fierce, not lovers of those who are good,
4watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu.
4traitors, heady, lofty, lovers of pleasure more than lovers of God,
5Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.
5having a form of piety, and its power having denied; and from these be turning away,
6Baadhi yao huenda katika nyumba za watu na huwateka wanawake dhaifu waliolemewa mizigo ya dhambi na ambao wanaongozwa na tamaa za kila aina;
6for of these there are those coming into the houses and leading captive the silly women, laden with sins, led away with desires manifold,
7wanawake ambao wanajaribu daima kujifunza lakini hawawezi kuufikia ujuzi wa huo ukweli.
7always learning, and never to a knowledge of truth able to come,
8Watu hao huupinga ukweli kama vile Yane na Yambre walivyompinga Mose.
8and, even as Jannes and Jambres stood against Moses, so also these do stand against the truth, men corrupted in mind, disapproved concerning the faith;
9Lakini hawataweza kuendelea zaidi kwa maana upumbavu wao utaonekana wazi kwa wote. Ndivyo ilivyokuwa kwa akina Yane na Yambre.
9but they shall not advance any further, for their folly shall be manifest to all, as theirs also did become.
10Wewe lakini, umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu, subira yangu,
10And thou -- thou hast followed after my teaching, manner of life, purpose, faith, long-suffering, love, endurance,
11udhalimu na mateso yangu. Unayajua mambo yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Lustra. Nilivumilia udhalimu mkubwa mno! Lakini Bwana aliniokoa katika mambo hayo yote.
11the persecutions, the afflictions, that befel me in Antioch, in Iconium, in Lystra; what persecutions I endured, and out of all the Lord did deliver me,
12Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kumcha Mungu katika kuungana na Kristo Yesu lazima adhulumiwe.
12and all also who will to live piously in Christ Jesus shall be persecuted,
13Watu waovu na wadanyanyifu watazidi kuwa waovu zaidi na zaidi kwa kuwadanganya wengine na kudanganyika wao wenyewe.
13and evil men and impostors shall advance to the worse, leading astray and being led astray.
14Lakini wewe dumu katika ukweli ule uliofundishwa, ukaukubali kabisa. Unawajua wale waliokuwa walimu wako.
14And thou -- be remaining in the things which thou didst learn and wast entrusted with, having known from whom thou didst learn,
15Unakumbuka kwamba tangu utoto wako umeyajua Maandiko Matakatifu ambayo yaweza kukupatia hekima iletayo wokovu kwa njia ya imani kwa Kristo Yesu.
15and because from a babe the Holy Writings thou hast known, which are able to make thee wise -- to salvation, through faith that [is] in Christ Jesus;
16Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya, kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili,
16every Writing [is] God-breathed, and profitable for teaching, for conviction, for setting aright, for instruction that [is] in righteousness,
17ili mtu anayemtumikia Mungu awe mkamilifu, na tayari kabisa kufanya kila tendo jema.
17that the man of God may be fitted -- for every good work having been completed.