Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

2 Timothy

4

1Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
1I do fully testify, then, before God, and the Lord Jesus Christ, who is about to judge living and dead at his manifestation and his reign --
2hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
2preach the word; be earnest in season, out of season, convict, rebuke, exhort, in all long-suffering and teaching,
3Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
3for there shall be a season when the sound teaching they will not suffer, but according to their own desires to themselves they shall heap up teachers -- itching in the hearing,
4Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
4and indeed, from the truth the hearing they shall turn away, and to the fables they shall be turned aside.
5Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
5And thou -- watch in all things; suffer evil; do the work of one proclaiming good news; of thy ministration make full assurance,
6Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
6for I am already being poured out, and the time of my release hath arrived;
7Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
7the good strife I have striven, the course I have finished, the faith I have kept,
8Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
8henceforth there is laid up for me the crown of the righteousness that the Lord -- the Righteous Judge -- shall give to me in that day, and not only to me, but also to all those loving his manifestation.
9Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
9Be diligent to come unto me quickly,
10Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia.
10for Demas forsook me, having loved the present age, and went on to Thessalonica, Crescens to Galatia, Titus to Dalmatia,
11Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
11Lukas only is with me; Markus having taken, bring with thyself, for he is profitable to me for ministration;
12Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
12and Tychicus I sent to Ephesus;
13Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
13the cloak that I left in Troas with Carpus, coming, bring thou and the books -- especially the parchments.
14Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
14Alexander the coppersmith did me much evil; may the Lord repay to him according to his works,
15Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
15of whom also do thou beware, for greatly hath he stood against our words;
16Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
16in my first defence no one stood with me, but all forsook me, (may it not be reckoned to them!)
17Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
17and the Lord stood by me, and did strengthen me, that through me the preaching might be fully assured, and all the nations might hear, and I was freed out of the mouth of a lion,
18Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina.
18and the Lord shall free me from every evil work, and shall save [me] -- to his heavenly kingdom; to whom [is] the glory to the ages of the ages! Amen.
19Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
19Salute Prisca and Aquilas, and Onesiphorus' household;
20Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
20Erastus did remain in Corinth, and Trophimus I left in Miletus infirm;
21Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
21be diligent to come before winter. Salute thee doth Eubulus, and Pudens, and Linus, and Claudia, and all the brethren.
22Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.
22The Lord Jesus Christ [is] with thy spirit; the grace [is] with you! Amen.