1Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
1And in the day of the Pentecost being fulfilled, they were all with one accord at the same place,
2Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
2and there came suddenly out of the heaven a sound as of a bearing violent breath, and it filled all the house where they were sitting,
3Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
3and there appeared to them divided tongues, as it were of fire; it sat also upon each one of them,
4Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
4and they were all filled with the Holy Spirit, and began to speak with other tongues, according as the Spirit was giving them to declare.
5Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
5And there were dwelling in Jerusalem Jews, devout men from every nation of those under the heaven,
6Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
6and the rumour of this having come, the multitude came together, and was confounded, because they were each one hearing them speaking in his proper dialect,
7Walistaajabu na kushangaa, wakisema, "Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
7and they were all amazed, and did wonder, saying one unto another, `Lo, are not all these who are speaking Galileans?
8Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
8and how do we hear, each in our proper dialect, in which we were born?
9Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
9Parthians, and Medes, and Elamites, and those dwelling in Mesopotamia, in Judea also, and Cappadocia, Pontus, and Asia,
10Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
10Phrygia also, and Pamphylia, Egypt, and the parts of Libya, that [are] along Cyrene, and the strangers of Rome, both Jews and proselytes,
11Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu."
11Cretes and Arabians, we did hear them speaking in our tongues the great things of God.`
12Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, "Hii ina maana gani?"
12And they were all amazed, and were in doubt, saying one unto another, `What would this wish to be?`
13Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, "Watu hawa wamelewa divai mpya!"
13and others mocking said, — `They are full of sweet wine;`
14Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: "Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
14and Peter having stood up with the eleven, lifted up his voice and declared to them, `Men, Jews! and all those dwelling in Jerusalem, let this be known to you, and harken to my sayings,
15Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
15for these are not drunken, as ye take it up, for it is the third hour of the day.
16Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
16`But this is that which hath been spoken through the prophet Joel:
17Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
17And it shall be in the last days, saith God, I will pour out of My Spirit upon all flesh, and your sons and your daughters shall prophesy, and your young men shall see visions, and your old men shall dream dreams;
18Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
18and also upon My men-servants, and upon My maid-servants, in those days, I will pour out of My Spirit, and they shall prophesy;
19Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
19and I will give wonders in the heaven above, and signs upon the earth beneath — blood, and fire, and vapour of smoke,
20jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
20the sun shall be turned to darkness, and the moon to blood, before the coming of the day of the Lord — the great and illustrious;
21Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
21and it shall be, every one — whoever shall call upon the name of the Lord, he shall be saved.
22"Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
22`Men, Israelites! hear these words, Jesus the Nazarene, a man approved of God among you by mighty works, and wonders, and signs, that God did through him in the midst of you, according as also ye yourselves have known;
23Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
23this one, by the determinate counsel and foreknowledge of God, being given out, having taken by lawless hands, having crucified — ye did slay;
24Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
24whom God did raise up, having loosed the pains of the death, because it was not possible for him to be held by it,
25Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
25for David saith in regard to him: I foresaw the Lord always before me — because He is on my right hand — that I may not be moved;
26Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
26because of this was my heart cheered, and my tongue was glad, and yet — my flesh also shall rest on hope,
27kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze.
27because Thou wilt not leave my soul to hades, nor wilt Thou give Thy Kind One to see corruption;
28Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
28Thou didst make known to me ways of life, Thou shalt fill me with joy with Thy countenance.
29"Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
29`Men, brethren! it is permitted to speak with freedom unto you concerning the patriarch David, that he both died and was buried, and his tomb is among us unto this day;
30Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
30a prophet, therefore, being, and knowing that with an oath God did swear to him, out of the fruit of his loins, according to the flesh, to raise up the Christ, to sit upon his throne,
31Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza.
31having foreseen, he did speak concerning the rising again of the Christ, that his soul was not left to hades, nor did his flesh see corruption.
32Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
32`This Jesus did God raise up, of which we are all witnesses;
33Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
33at the right hand then of God having been exalted — also the promise of the Holy Spirit having received from the Father — he was shedding forth this, which now ye see and hear;
34Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
34for David did not go up to the heavens, and he saith himself: The Lord saith to my lord, Sit thou at my right hand,
35hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
35till I make thy foes thy footstool;
36"Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo."
36assuredly, therefore, let all the house of Israel know, that both Lord and Christ did God make him — this Jesus whom ye did crucify.`
37Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: "Ndugu zetu, tufanye nini?"
37And having heard, they were pricked to the heart; they say also to Peter, and to the rest of the apostles, `What shall we do, men, brethren?`
38Petro akajibu, "Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
38and Peter said unto them, `Reform, and be baptized each of you on the name of Jesus Christ, to remission of sins, and ye shall receive the gift of the Holy Spirit,
39Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake."
39for to you is the promise, and to your children, and to all those afar off, as many as the Lord our God shall call.`
40Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, "Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu."
40Also with many more other words he was testifying and exhorting, saying, `Be saved from this perverse generation;`
41Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
41then those, indeed, who did gladly receive his word were baptized, and there were added on that day, as it were, three thousand souls,
42Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
42and they were continuing stedfastly in the teaching of the apostles, and the fellowship, and the breaking of the bread, and the prayers.
43Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
43And fear came on every soul, many wonders also and signs were being done through the apostles,
44Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
44and all those believing were at the same place, and had all things common,
45Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
45and the possessions and the goods they were selling, and were parting them to all, according as any one had need.
46Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
46Daily also continuing with one accord in the temple, breaking also at every house bread, they were partaking of food in gladness and simplicity of heart,
47Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.
47praising God, and having favour with all the people, and the Lord was adding those being saved every day to the assembly.