Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Colossians

3

1Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
1If, then, ye were raised with the Christ, the things above seek ye, where the Christ is, on the right hand of God seated,
2Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
2the things above mind ye, not the things upon the earth,
3Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
3for ye did die, and your life hath been hid with the Christ in God;
4Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
4when the Christ — our life — may be manifested, then also we with him shall be manifested in glory.
5Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
5Put to death, then, your members that [are] upon the earth — whoredom, uncleanness, passion, evil desire, and the covetousness, which is idolatry —
6Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
6because of which things cometh the anger of God upon the sons of the disobedience,
7Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
7in which also ye — ye did walk once, when ye lived in them;
8Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
8but now put off, even ye, the whole — anger, wrath, malice, evil-speaking, filthy talking — out of your mouth.
9Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
9Lie not one to another, having put off the old man with his practices,
10mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
10and having put on the new, which is renewed in regard to knowledge, after the image of Him who did create him;
11Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
11where there is not Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, foreigner, Scythian, servant, freeman — but the all and in all — Christ.
12Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
12Put on, therefore, as choice ones of God, holy and beloved, bowels of mercies, kindness, humble-mindedness, meekness, long-suffering,
13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
13forbearing one another, and forgiving each other, if any one with any one may have a quarrel, as also the Christ did forgive you — so also ye;
14Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
14and above all these things, [have] love, which is a bond of the perfection,
15Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
15and let the peace of God rule in your hearts, to which also ye were called in one body, and become thankful.
16Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
16Let the word of Christ dwell in you richly, in all wisdom, teaching and admonishing each other, in psalms, and hymns, and spiritual songs, in grace singing in your hearts to the Lord;
17Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
17and all, whatever ye may do in word or in work, [do] all things in the name of the Lord Jesus — giving thanks to the God and Father, through him.
18Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
18The wives! be subject to your own husbands, as is fit in the Lord;
19Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
19the husbands! love your wives, and be not bitter with them;
20Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
20the children! obey the parents in all things, for this is well-pleasing to the Lord;
21Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
21the fathers! vex not your children, lest they be discouraged.
22Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
22The servants! obey in all things those who are masters according to the flesh, not in eye-service as men-pleasers, but in simplicity of heart, fearing God;
23Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
23and all, whatever ye may do — out of soul work — as to the Lord, and not to men,
24Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
24having known that from the Lord ye shall receive the recompense of the inheritance — for the Lord Christ ye serve;
25Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.
25and he who is doing unrighteously shall receive what he did unrighteously, and there is no acceptance of persons.