1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
1The masters! that which is righteous and equal to the servants give ye, having known that ye also have a Master in the heavens.
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
2In the prayer continue ye, watching in it in thanksgiving;
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
3praying at the same time also for us, that God may open to us a door for the word, to speak the secret of the Christ, because of which also I have been bound,
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
4that I may manifest it, as it behoveth me to speak;
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
5in wisdom walk ye toward those without, the time forestalling;
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
6your word always in grace — with salt being seasoned — to know how it behoveth you to answer each one.
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
7All the things concerning me make known to you shall Tychicus — the beloved brother, and faithful ministrant, and fellow-servant in the Lord —
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
8whom I did send unto you for this very thing, that he might know the things concerning you, and might comfort your hearts,
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
9with Onesimus the faithful and beloved brother, who is of you; all things to you shall they make known that [are] here.
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
10Salute you doth Aristarchus, my fellow-captive, and Marcus, the nephew of Barnabas, (concerning whom ye did receive commands — if he may come unto you receive him,)
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
11and Jesus who is called Justus, who are of the circumcision: these only [are] fellow-workers for the reign of God who did become a comfort to me.
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
12Salute you doth Epaphras, who [is] of you, a servant of Christ, always striving for you in the prayers, that ye may stand perfect and made full in all the will of God,
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
13for I do testify to him, that he hath much zeal for you, and those in Laodicea, and those in Hierapolis.
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
14Salute you doth Lukas, the beloved physician, and Demas;
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
15salute ye those in Laodicea — brethren, and Nymphas, and the assembly in his house;
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
16and when the epistle may be read with you, cause that also in the assembly of the Laodiceans it may be read, and the [epistle] from Laodicea that ye also may read;
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
17and say to Archippus, `See to the ministration that thou didst receive in the Lord, that thou mayest fulfil it.`
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.
18The salutation by the hand of me, Paul; remember my bonds; the grace [is] with you. Amen.