1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
1Become, then, followers of God, as children beloved,
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
2and walk in love, as also the Christ did love us, and did give himself for us, an offering and a sacrifice to God for an odour of a sweet smell,
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
3and whoredom, and all uncleanness, or covetousness, let it not even be named among you, as becometh saints;
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
4also filthiness, and foolish talking, or jesting, — the things not fit — but rather thanksgiving;
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
5for this ye know, that every whoremonger, or unclean, or covetous person, who is an idolater, hath no inheritance in the reign of the Christ and God.
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
6Let no one deceive you with vain words, for because of these things cometh the anger of God upon the sons of the disobedience,
7Basi, msishirikiane nao.
7become not, then, partakers with them,
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
8for ye were once darkness, and now light in the Lord; as children of light walk ye,
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
9for the fruit of the Spirit [is] in all goodness, and righteousness, and truth,
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
10proving what is well-pleasing to the Lord,
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
11and have no fellowship with the unfruitful works of the darkness and rather even convict,
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
12for the things in secret done by them it is a shame even to speak of,
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
13and all the things reproved by the light are manifested, for everything that is manifested is light;
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
14wherefore he saith, `Arouse thyself, thou who art sleeping, and arise out of the dead, and the Christ shall shine upon thee.`
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
15See, then, how exactly ye walk, not as unwise, but as wise,
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
16redeeming the time, because the days are evil;
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
17because of this become not fools, but — understanding what [is] the will of the Lord,
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
18and be not drunk with wine, in which is dissoluteness, but be filled in the Spirit,
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
19speaking to yourselves in psalms and hymns and spiritual songs, singing and making melody in your heart to the Lord,
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
20giving thanks always for all things, in the name of our Lord Jesus Christ, to the God and Father;
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
21subjecting yourselves to one another in the fear of God.
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
22The wives! to your own husbands subject yourselves, as to the Lord,
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
23because the husband is head of the wife, as also the Christ [is] head of the assembly, and he is saviour of the body,
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
24but even as the assembly is subject to Christ, so also [are] the wives to their own husbands in everything.
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
25The husbands! love your own wives, as also the Christ did love the assembly, and did give himself for it,
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
26that he might sanctify it, having cleansed [it] with the bathing of the water in the saying,
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
27that he might present it to himself the assembly in glory, not having spot or wrinkle, or any of such things, but that it may be holy and unblemished;
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
28so ought the husbands to love their own wives as their own bodies: he who is loving his own wife — himself he doth love;
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
29for no one ever his own flesh did hate, but doth nourish and cherish it, as also the Lord — the assembly,
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
30because members we are of his body, of his flesh, and of his bones;
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
31`for this cause shall a man leave his father and mother, and shall be joined to his wife, and they shall be — the two — for one flesh;`
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
32this secret is great, and I speak in regard to Christ and to the assembly;
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.
33but ye also, every one in particular — let each his own wife so love as himself, and the wife — that she may reverence the husband.