Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Ephesians

6

1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
1The children! obey your parents in the Lord, for this is righteous;
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
2honour thy father and mother,
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
3which is the first command with a promise, `That it may be well with thee, and thou mayest live a long time upon the land.`
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
4And the fathers! provoke not your children, but nourish them in the instruction and admonition of the Lord.
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
5The servants! obey the masters according to the flesh with fear and trembling, in the simplicity of your heart, as to the Christ;
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
6not with eye-service as men-pleasers, but as servants of the Christ, doing the will of God out of soul,
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
7with good-will serving, as to the Lord, and not to men,
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
8having known that whatever good thing each one may do, this he shall receive from the Lord, whether servant or freeman.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
9And the masters! the same things do ye unto them, letting threatening alone, having known that also your Master is in the heavens, and acceptance of persons is not with him.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
10As to the rest, my brethren, be strong in the Lord, and in the power of his might;
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
11put on the whole armour of God, for your being able to stand against the wiles of the devil,
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
12because we have not the wrestling with blood and flesh, but with the principalities, with the authorities, with the world-rulers of the darkness of this age, with the spiritual things of the evil in the heavenly places;
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
13because of this take ye up the whole armour of God, that ye may be able to resist in the day of the evil, and all things having done — to stand.
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
14Stand, therefore, having your loins girt about in truth, and having put on the breastplate of the righteousness,
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
15and having the feet shod in the preparation of the good-news of the peace;
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
16above all, having taken up the shield of the faith, in which ye shall be able all the fiery darts of the evil one to quench,
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
17and the helmet of the salvation receive, and the sword of the Spirit, which is the saying of God,
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
18through all prayer and supplication praying at all times in the Spirit, and in regard to this same, watching in all perseverance and supplication for all the saints —
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
19and in behalf of me, that to me may be given a word in the opening of my mouth, in freedom, to make known the secret of the good news,
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
20for which I am an ambassador in a chain, that in it I may speak freely — as it behoveth me to speak.
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
21And that ye may know — ye also — the things concerning me — what I do, all things make known to you shall Tychicus, the beloved brother and faithful ministrant in the Lord,
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
22whom I did send unto you for this very thing, that ye might know the things concerning us, and that he might comfort your hearts.
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
23Peace to the brethren, and love, with faith, from God the Father, and the Lord Jesus Christ!
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.
24The grace with all those loving our Lord Jesus Christ — undecayingly! Amen.