Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Luke

20

1Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
1And it came to pass, on one of those days, as he is teaching the people in the temple, and proclaiming good news, the chief priests and the scribes, with the elders, came upon [him],
2wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
2and spake unto him, saying, `Tell us by what authority thou dost these things? or who is he that gave to thee this authority?`
3Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
3And he answering said unto them, `I will question you — I also — one thing, and tell me:
4mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
4the baptism of John, from heaven was it, or from men?`
5Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
5And they reasoned with themselves, saying — `If we may say, From heaven, he will say, Wherefore, then, did ye not believe him?
6Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
6and if we may say, From men, all the people will stone us, for they are having been persuaded John to be a prophet.`
7Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
7And they answered, that they knew not whence [it was],
8Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
8and Jesus said to them, `Neither do I say to you by what authority I do these things.`
9Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
9And he began to speak unto the people this simile: `A certain man planted a vineyard, and gave it out to husbandmen, and went abroad for a long time,
10Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
10and at the season he sent unto the husbandmen a servant, that from the fruit of the vineyard they may give to him, but the husbandmen having beat him, did send [him] away empty.
11Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
11`And he added to send another servant, and they that one also having beaten and dishonoured, did send away empty;
12Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
12and he added to send a third, and this one also, having wounded, they did cast out.
13Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
13`And the owner of the vineyard said, What shall I do? I will send my son — the beloved, perhaps having seen this one, they will do reverence;
14Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
14and having seen him, the husbandmen reasoned among themselves, saying, This is the heir; come, we may kill him, that the inheritance may become ours;
15Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
15and having cast him outside of the vineyard, they killed [him]; what, then, shall the owner of the vineyard do to them?
16Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
16He will come, and destroy these husbandmen, and will give the vineyard to others.` And having heard, they said, `Let it not be!`
17Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
17and he, having looked upon them, said, `What, then, is this that hath been written: A stone that the builders rejected — this became head of a corner?
18Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
18every one who hath fallen on that stone shall be broken, and on whom it may fall, it will crush him to pieces.`
19Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
19And the chief priests and the scribes sought to lay hands on him in that hour, and they feared the people, for they knew that against them he spake this simile.
20Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
20And, having watched [him], they sent forth liers in wait, feigning themselves to be righteous, that they might take hold of his word, to deliver him up to the rule and to the authority of the governor,
21Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
21and they questioned him, saying, `Teacher, we have known that thou dost say and teach rightly, and dost not accept a person, but in truth the way of God dost teach;
22Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
22Is it lawful to us to give tribute to Caesar or not?`
23Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
23And he, having perceived their craftiness, said unto them, `Why me do ye tempt?
24"Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
24shew me a denary; of whom hath it an image and superscription?` and they answering said, `Of Caesar:`
25Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
25and he said to them, `Give back, therefore, the things of Caesar to Caesar, and the things of God to God;`
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
26and they were not able to take hold on his saying before the people, and having wondered at his answer, they were silent.
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
27And certain of the Sadducees, who are denying that there is a rising again, having come near, questioned him,
28"Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
28saying, `Teacher, Moses wrote to us, If any one`s brother may die, having a wife, and he may die childless — that his brother may take the wife, and may raise up seed to his brother.
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
29`There were, then, seven brothers, and the first having taken a wife, died childless,
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
30and the second took the wife, and he died childless,
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
31and the third took her, and in like manner also the seven — they left not children, and they died;
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
32and last of all died also the woman:
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
33in the rising again, then, of which of them doth she become wife? — for the seven had her as wife.`
34Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
34And Jesus answering said to them, `The sons of this age do marry and are given in marriage,
35lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
35but those accounted worthy to obtain that age, and the rising again that is out of the dead, neither marry, nor are they given in marriage;
36Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
36for neither are they able to die any more — for they are like messengers — and they are sons of God, being sons of the rising again.
37Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
37`And that the dead are raised, even Moses shewed at the Bush, since he doth call the Lord, the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob;
38Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
38and He is not a God of dead men, but of living, for all live to Him.`
39Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
39And certain of the scribes answering said, `Teacher, thou didst say well;`
40Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
40and no more durst they question him anything.
41Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
41And he said unto them, `How do they say the Christ to be son of David,
42Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
42and David himself saith in the Book of Psalms, The Lord said to my lord, Sit thou on my right hand,
43mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
43till I shall make thine enemies thy footstool;
44Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?"
44David, then, doth call him lord, and how is he his son?`
45Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
45And, all the people hearing, he said to his disciples,
46"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
46`Take heed of the scribes, who are wishing to walk in long robes, and are loving salutations in the markets, and first seats in the synagogues, and first couches in the suppers,
47Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"
47who devour the houses of the widows, and for a pretence make long prayers, these shall receive more abundant judgment.`