Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Luke

21

1Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
1And having looked up, he saw those who did cast their gifts to the treasury — rich men,
2akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
2and he saw also a certain poor widow casting there two mites,
3Basi, akasema, "Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
3and he said, `Truly I say to you, that this poor widow did cast in more than all;
4Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."
4for all these out of their superabundance did cast into the gifts to God, but this one out of her want, all the living that she had, did cast in.`
5Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
5And certain saying about the temple, that with goodly stones and devoted things it hath been adorned, he said,
6"Haya yote mnayoyaona--zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
6`These things that ye behold — days will come, in which there shall not be left a stone upon a stone, that shall not be thrown down.`
7Basi, wakamwuliza, "Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?"
7And they questioned him, saying, `Teacher, when, then, shall these things be? and what [is] the sign when these things may be about to happen?`
8Yesu akawajibu, "Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
8And he said, `See — ye may not be led astray, for many shall come in my name, saying — I am [he], and the time hath come nigh; go not on then after them;
9Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado."
9and when ye may hear of wars and uprisings, be not terrified, for it behoveth these things to happen first, but the end [is] not immediately.`
10Halafu akaendelea kusema: "Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
10Then said he to them, `Nation shall rise against nation, and kingdom against kingdom,
11Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
11great shakings also in every place, and famines, and pestilences, there shall be; fearful things also, and great signs from heaven there shall be;
12Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
12and before all these, they shall lay on you their hands, and persecute, delivering up to synagogues and prisons, being brought before kings and governors for my name`s sake;
13Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
13and it shall become to you for a testimony.
14Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
14`Settle, then, to your hearts, not to meditate beforehand to reply,
15kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
15for I will give to you a mouth and wisdom that all your opposers shall not be able to refute or resist.
16Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
16`And ye shall be delivered up also by parents, and brothers, and kindred, and friends, and they shall put of you to death;
17Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
17and ye shall be hated by all because of my name —
18Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
18and a hair out of your head shall not perish;
19Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
19in your patience possess ye your souls.
20"Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
20`And when ye may see Jerusalem surrounded by encampments, then know that come nigh did her desolation;
21Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
21then those in Judea, let them flee to the mountains; and those in her midst, let them depart out; and those in the countries, let them not come in to her;
22Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
22because these are days of vengeance, to fulfil all things that have been written.
23Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
23`And wo to those with child, and to those giving suck, in those days; for there shall be great distress on the land, and wrath on this people;
24Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
24and they shall fall by the mouth of the sword, and shall be led captive to all the nations, and Jerusalem shall be trodden down by nations, till the times of nations be fulfilled.
25"Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
25`And there shall be signs in sun, and moon, and stars, and on the land [is] distress of nations with perplexity, sea and billow roaring;
26Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
26men fainting at heart from fear, and expectation of the things coming on the world, for the powers of the heavens shall be shaken.
27Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
27`And then they shall see the Son of Man, coming in a cloud, with power and much glory;
28Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia."
28and these things beginning to happen bend yourselves back, and lift up your heads, because your redemption doth draw nigh.`
29Kisha akawaambia mfano: "Angalieni mtini na miti mingine yote.
29And he spake a simile to them: `See the fig-tree, and all the trees,
30Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
30when they may now cast forth, having seen, of yourselves ye know that now is the summer nigh;
31Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
31so also ye, when ye may see these things happening, ye know that near is the reign of God;
32Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
32verily I say to you — This generation may not pass away till all may have come to pass;
33Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
33the heaven and the earth shall pass away, but my words may not pass away.
34"Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
34`And take heed to yourselves, lest your hearts may be weighed down with surfeiting, and drunkenness, and anxieties of life, and suddenly that day may come on you,
35Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
35for as a snare it shall come on all those dwelling on the face of all the land,
36Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu."
36watch ye, then, in every season, praying that ye may be accounted worthy to escape all these things that are about to come to pass, and to stand before the Son of Man.`
37Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
37And he was during the days in the temple teaching, and during the nights, going forth, he was lodging at the mount called of Olives;
38Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.
38and all the people were coming early unto him in the temple to hear him.