1Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
1A beginning of the good news of Jesus Christ, Son of God.
2Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
2As it hath been written in the prophets, `Lo, I send My messenger before thy face, who shall prepare thy way before thee,` —
3Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake."
3`A voice of one calling in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, straight make ye his paths,` —
4Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
4John came baptizing in the wilderness, and proclaiming a baptism of reformation — to remission of sins,
5Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
5and there were going forth to him all the region of Judea, and they of Jerusalem, and they were all baptized by him in the river Jordan, confessing their sins.
6Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
6And John was clothed with camel`s hair, and a girdle of skin around his loins, and eating locusts and honey of the field,
7Naye alihubiri akisema, "Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
7and he proclaimed, saying, `He doth come — who is mightier than I — after me, of whom I am not worthy — having stooped down — to loose the latchet of his sandals;
8Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu."
8I indeed did baptize you with water, but he shall baptize you with the Holy Spirit.`
9Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
9And it came to pass in those days, Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by John at the Jordan;
10Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
10and immediately coming up from the water, he saw the heavens dividing, and the Spirit as a dove coming down upon him;
11Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
11and a voice came out of the heavens, `Thou art My Son — the Beloved, in whom I did delight.`
12Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
12And immediately doth the Spirit put him forth to the wilderness,
13akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
13and he was there in the wilderness forty days, being tempted by the Adversary, and he was with the beasts, and the messengers were ministering to him.
14Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
14And after the delivering up of John, Jesus came to Galilee, proclaiming the good news of the reign of God,
15"Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!"
15and saying — `Fulfilled hath been the time, and the reign of God hath come nigh, reform ye, and believe in the good news.`
16Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
16And, walking by the sea of Galilee, he saw Simon, and Andrew his brother, casting a drag into the sea, for they were fishers,
17Yesu akawaambia, "Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
17and Jesus said to them, `Come ye after me, and I shall make you to become fishers of men;`
18Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
18and immediately, having left their nets, they followed him.
19Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
19And having gone on thence a little, he saw James of Zebedee, and John his brother, and they were in the boat refitting the nets,
20Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
20and immediately he called them, and, having left their father Zebedee in the boat with the hired servants, they went away after him.
21Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
21And they go on to Capernaum, and immediately, on the sabbaths, having gone into the synagogue, he was teaching,
22Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
22and they were astonished at his teaching, for he was teaching them as having authority, and not as the scribes.
23Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
23And there was in their synagogue a man with an unclean spirit, and he cried out,
24akapaaza sauti, "Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!"
24saying, `Away! what — to us and to thee, Jesus the Nazarene? thou didst come to destroy us; I have known thee who thou art — the Holy One of God.`
25Yesu akamkemea, "Nyamaza! Mtoke mtu huyu."
25And Jesus rebuked him, saying, `Be silenced, and come forth out of him,`
26Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
26and the unclean spirit having torn him, and having cried with a great voice, came forth out of him,
27Watu wote wakashangaa, wakaulizana, "Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!"
27and they were all amazed, so as to reason among themselves, saying, `What is this? what new teaching [is] this? that with authority also the unclean spirits he commandeth, and they obey him!`
28Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
28And the fame of him went forth immediately to all the region, round about, of Galilee.
29Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
29And immediately, having come forth out of the synagogue, they went to the house of Simon and Andrew, with James and John,
30Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
30and the mother-in-law of Simon was lying fevered, and immediately they tell him about her,
31Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
31and having come near, he raised her up, having laid hold of her hand, and the fever left her immediately, and she was ministering to them.
32Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
32And evening having come, when the sun did set, they brought unto him all who were ill, and who were demoniacs,
33Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
33and the whole city was gathered together near the door,
34Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
34and he healed many who were ill of manifold diseases, and many demons he cast forth, and was not suffering the demons to speak, because they knew him.
35Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
35And very early, it being yet night, having risen, he went forth, and went away to a desert place, and was there praying;
36Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
36and Simon and those with him went in quest of him,
37Walipomwona wakamwambia, "Kila mtu anakutafuta."
37and having found him, they say to him, — `All do seek thee;`
38Yesu akawaambia, "Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo."
38and he saith to them, `We may go to the next towns, that there also I may preach, for for this I came forth.`
39Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
39And he was preaching in their synagogues, in all Galilee, and is casting out the demons,
40Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, "Ukitaka, waweza kunitakasa!"
40and there doth come to him a leper, calling on him, and kneeling to him, and saying to him — `If thou mayest will, thou art able to cleanse me.`
41Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, "Nataka, takasika!"
41And Jesus having been moved with compassion, having stretched forth the hand, touched him, and saith to him, `I will; be thou cleansed;`
42Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
42and he having spoken, immediately the leprosy went away from him, and he was cleansed.
43Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
43And having sternly charged him, immediately he put him forth,
44"Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
44and saith to him, `See thou mayest say nothing to any one, but go away, thyself shew to the priest, and bring near for thy cleansing the things Moses directed, for a testimony to them.`
45Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
45And he, having gone forth, began to proclaim much, and to spread abroad the thing, so that no more he was able openly to enter into the city, but he was without in desert places, and they were coming unto him from every quarter.