1Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
1Then Jesus spake to the multitudes, and to his disciples,
2"Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
2saying, `On the seat of Moses sat down the scribes and the Pharisees;
3Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
3all, then, as much as they may say to you to observe, observe and do, but according to their works do not, for they say, and do not;
4Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
4for they bind together burdens heavy and grievous to be borne, and lay upon the shoulders of men, but with their finger they will not move them.
5Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
5`And all their works they do to be seen by men, and they make broad their phylacteries, and enlarge the fringes of their garments,
6Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
6they love also the chief couches in the supper, and the chief seats in the synagogues,
7Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
7and the salutations in the market-places, and to be called by men, Rabbi, Rabbi.
8Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
8`And ye — ye may not be called Rabbi, for one is your director — the Christ, and all ye are brethren;
9Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
9and ye may not call [any] your father on the earth, for one is your Father, who is in the heavens,
10Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
10nor may ye be called directors, for one is your director — the Christ.
11Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
11And the greater of you shall be your ministrant,
12Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
12and whoever shall exalt himself shall be humbled, and whoever shall humble himself shall be exalted.
13"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
13`Wo to you, Scribes and Pharisees, hypocrites! because ye shut up the reign of the heavens before men, for ye do not go in, nor those going in do ye suffer to enter.
14Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
14`Wo to you, Scribes and Pharisees, hypocrites! because ye eat up the houses of the widows, and for a pretence make long prayers, because of this ye shall receive more abundant judgment.
15"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe.
15`Wo to you, Scribes and Pharisees, hypocrites! because ye go round the sea and the dry land to make one proselyte, and whenever it may happen — ye make him a son of gehenna twofold more than yourselves.
16"Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
16`Wo to you, blind guides, who are saying, Whoever may swear by the sanctuary, it is nothing, but whoever may swear by the gold of the sanctuary — is debtor!
17Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
17Fools and blind! for which [is] greater, the gold, or the sanctuary that is sanctifying the gold?
18Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
18`And, whoever may swear by the altar, it is nothing; but whoever may swear by the gift that is upon it — is debtor!
19Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
19Fools and blind! for which [is] greater, the gift, or the altar that is sanctifying the gift?
20Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
20`He therefore who did swear by the altar, doth swear by it, and by all things on it;
21Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
21and he who did swear by the sanctuary, doth swear by it, and by Him who is dwelling in it;
22Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
22and he who did swear by the heaven, doth swear by the throne of God, and by Him who is sitting upon it.
23Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
23`Wo to you, Scribes and Pharisees, hypocrites! because ye give tithe of the mint, and the dill, and the cumin, and did neglect the weightier things of the Law — the judgment, and the kindness, and the faith; these it behoved [you] to do, and those not to neglect.
24Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
24`Blind guides! who are straining out the gnat, and the camel are swallowing.
25"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
25`Wo to you, Scribes and Pharisees, hypocrites! because ye make clean the outside of the cup and the plate, and within they are full of rapine and incontinence.
26Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
26`Blind Pharisee! cleanse first the inside of the cup and the plate, that the outside of them also may become clean.
27"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
27`Wo to you, Scribes and Pharisees, hypocrites! because ye are like to whitewashed sepulchres, which outwardly indeed do appear beautiful, and within are full of bones of dead men, and of all uncleanness;
28Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
28so also ye outwardly indeed do appear to men righteous, and within ye are full of hypocrisy and lawlessness.
29"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
29`Wo to you, Scribes and Pharisees, hypocrites! because ye build the sepulchres of the prophets, and adorn the tombs of the righteous,
30Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
30and say, If we had been in the days of our fathers, we would not have been partakers with them in the blood of the prophets.
31Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
31So that ye testify to yourselves, that ye are sons of them who did murder the prophets;
32Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
32and ye — ye fill up the measure of your fathers.
33Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu?
33`Serpents! brood of vipers! how may ye escape from the judgment of the gehenna?
34Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
34`Because of this, lo, I send to you prophets, and wise men, and scribes, and of them ye will kill and crucify, and of them ye will scourge in your synagogues, and will pursue from city to city;
35Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
35that on you may come all the righteous blood being poured out on the earth from the blood of Abel the righteous, unto the blood of Zacharias son of Barachias, whom ye slew between the sanctuary and the altar:
36Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
36verily I say to you, all these things shall come upon this generation.
37"Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
37`Jerusalem, Jerusalem, that art killing the prophets, and stoning those sent unto thee, how often did I will to gather thy children together, as a hen doth gather her own chickens under the wings, and ye did not will.
38Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
38Lo, left desolate to you is your house;
39Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."
39for I say to you, ye may not see me henceforth, till ye may say, Blessed [is] he who is coming in the name of the Lord.`