Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Philemon

1

1Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
1Paul, a prisoner of Christ Jesus, and Timotheus the brother, to Philemon our beloved and fellow-worker,
2na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
2and Apphia the beloved, and Archippus our fellow-soldier, and the assembly in thy house:
3Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
3Grace to you, and peace, from God our Father, and the Lord Jesus Christ!
4Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
4I give thanks to my God, always making mention of thee in my prayers,
5maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
5hearing of thy love and faith that thou hast unto the Lord Jesus and toward all the saints,
6Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
6that the fellowship of thy faith may become working in the full knowledge of every good thing that [is] in you toward Christ Jesus;
7Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
7for we have much joy and comfort in thy love, because the bowels of the saints have been refreshed through thee, brother.
8Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
8Wherefore, having in Christ much boldness to command thee that which is fit —
9Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
9because of the love I rather entreat, being such an one as Paul the aged, and now also a prisoner of Jesus Christ;
10Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
10I entreat thee concerning my child — whom I did beget in my bonds — Onesimus,
11Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
11who once was to thee unprofitable, and now is profitable to me and to thee,
12Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
12whom I did send again, and thou him (that is, my own bowels) receive,
13Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
13whom I did wish to retain to myself, that in thy behalf he might minister to me in the bonds of the good news,
14Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
14and apart from thy mind I willed to do nothing, that as of necessity thy good deed may not be, but of willingness,
15Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima.
15for perhaps because of this he did depart for an hour, that age-duringly thou mayest have him,
16Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
16no more as a servant, but above a servant — a brother beloved, especially to me, and how much more to thee, both in the flesh and in the Lord!
17Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
17If, then, with me thou hast fellowship, receive him as me,
18Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
18and if he did hurt to thee, or doth owe anything, this to me be reckoning;
19Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
19I, Paul did write with my hand, I — I will repay; that I may not say that also thyself, besides, to me thou dost owe.
20Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
20Yes, brother, may I have profit of thee in the Lord; refresh my bowels in the Lord;
21Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
21having been confident in thy obedience I did write to thee, having known that also above what I may say thou wilt do;
22Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
22and at the same time also prepare for me a lodging, for I hope that through your prayers I shall be granted to you.
23Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
23Salute thee doth Epaphras, (my fellow-captive in Christ Jesus,)
24Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
24Markus, Aristarchus, Demas, Lukas, my fellow-workmen!
25Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
25The grace of our Lord Jesus Christ [is] with your spirit! Amen.