Swahili: New Testament

Young`s Literal Translation

Titus

3

1Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
1Remind them to be subject to principalities and authorities, to obey rule, unto every good work to be ready,
2Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
2of no one to speak evil, not to be quarrelsome -- gentle, showing all meekness to all men,
3Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
3for we were once -- also we -- thoughtless, disobedient, led astray, serving desires and pleasures manifold, in malice and envy living, odious -- hating one another;
4Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
4and when the kindness and the love to men of God our Saviour did appear
5alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
5(not by works that [are] in righteousness that we did but according to His kindness,) He did save us, through a bathing of regeneration, and a renewing of the Holy Spirit,
6Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
6which He poured upon us richly, through Jesus Christ our Saviour,
7ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia.
7that having been declared righteous by His grace, heirs we may become according to the hope of life age-during.
8Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
8Stedfast [is] the word; and concerning these things I counsel thee to affirm fully, that they may be thoughtful, to be leading in good works -- who have believed God; these are the good and profitable things to men,
9Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
9and foolish questions, and genealogies, and contentions, and strivings about law, stand away from -- for they are unprofitable and vain.
10Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
10A sectarian man, after a first and second admonition be rejecting,
11Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
11having known that he hath been subverted who [is] such, and doth sin, being self-condemned.
12Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
12When I shall send Artemas unto thee, or Tychicus, be diligent to come unto me to Nicopolis, for there to winter I have determined.
13Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
13Zenas the lawyer and Apollos bring diligently on their way, that nothing to them may be lacking,
14Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
14and let them learn -- ours also -- to be leading in good works to the necessary uses, that they may not be unfruitful.
15Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.
15Salute thee do all those with me; salute those loving us in faith; the grace [is] with you all!