Swahili: New Testament

الكتاب المقدس (Van Dyke)

Galatians

5

1Kristo alitupa uhuru akataka tubaki huru. Basi, simameni imara wala msikubali tena kuwa chini ya nira ya utumwa.
1فاثبتوا اذا في الحرية التي قد حررنا المسيح بها ولا ترتبكوا ايضا بنير عبودية.
2Sikilizeni! Ni mimi Paulo ninayesema nanyi! Kama mkikubali kutahiriwa, Kristo hatawafaidia chochote.
2ها انا بولس اقول لكم انه ان اختتنتم لا ينفعكم المسيح شيئا.
3Nasema tena wazi: kila anayekubali kutahiriwa itambidi kuishika Sheria yote.
3لكن اشهد ايضا لكل انسان مختتن انه ملتزم ان يعمل بكل الناموس.
4Kama mnatazamia kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Sheria, basi, mmejitenga mbali na Kristo; mko nje ya neema ya Mungu.
4قد تبطلتم عن المسيح ايها الذين تتبررون بالناموس. سقطتم من النعمة
5Kwa upande wetu, lakini, sisi tunatumaini kwamba kwa nguvu ya Roho tunakubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani.
5فاننا بالروح من الايمان نتوقع رجاء بر.
6Maana ikiwa tumeungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutotahiriwa hakuna maana; cha maana ni imani ifanyayo kazi kwa mapendo.
6لانه في المسيح يسوع لا الختان ينفع شيئا ولا الغرلة بل الايمان العامل بالمحبة.
7Mwenendo wenu ulikuwa mzuri! Nani, basi aliyewazuia kuuzingatia ukweli?
7كنتم تسعون حسنا. فمن صدكم حتى لا تطاوعوا للحق.
8Aliyesababisha hali hiyo si Mungu ambaye amewaiteni.
8هذه المطاوعة ليست من الذي دعاكم.
9"chachu kidogo tu huchachusha donge lote la unga!"
9خميرة صغيرة تخمّر العجين كله.
10Kutokana na kuungana kwetu na Bwana, nina tumaini kubwa kwamba ninyi hamtakuwa na msimamo tofauti nami. Tena yeyote huyo anayewavurugeni--awe nani au nani--hakika ataadhibiwa.
10ولكنني اثق بكم في الرب انكم لا تفتكرون شيئا آخر. ولكن الذي يزعجكم سيحمل الدينونة ايّ من كان.
11Na kwa upande wangu, ndugu zangu, kama bado ninahubiri kwamba kutahiriwa ni lazima, kwa nini basi, bado ninadhulumiwa? Kama ingalikuwa hivyo, mahubiri yangu juu ya msalaba wa Kristo yasingalileta aibu yoyote.
11واما انا ايها الاخوة فان كنت بعد اكرز بالختان فلماذا أضطهد بعد. اذا عثرة الصليب قد بطلت.
12Laiti hao wanaowavurugeni wangejikatakata wenyewe!
12يا ليت الذين يقلقونكم يقطعون ايضا
13Ninyi, ndugu, mliitwa muwe watu huru. Lakini uhuru huo usiwe kisingizio cha kutawaliwa na tamaa za kidunia; ila mnapaswa kutumikiana kwa upendo.
13فانكم انما دعيتم للحرية ايها الاخوة. غير انه لا تصيّروا الحرية فرصة للجسد بل بالمحبة اخدموا بعضكم بعضا.
14Maana Sheria yote hutimizwa katika kushika amri hii moja: "Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
14لان كل الناموس في كلمة واحده يكمل. تحب قريبك كنفسك.
15Lakini ikiwa mtaumana na kutafunana kama wanyama, jihadharini msije mkaangamizana wenyewe kwa wenyewe!
15فاذا كنتم تنهشون وتأكلون بعضكم بعضا فانظروا لئلا تفنوا بعضكم بعضا
16Basi, nasema hivi: mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia.
16وانما اقول اسلكوا بالروح فلا تكملوا شهوة الجسد.
17Maana, tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamwezi kufanya yale mnayotaka ninyi wenyewe.
17لان الجسد يشتهي ضد الروح والروح ضد الجسد. وهذان يقاوم احدهما الآخر حتى تفعلون ما لا تريدون.
18Kama mkiongozwa na Roho, basi, hamko tena chini ya Sheria.
18ولكن اذا انقدتم بالروح فلستم تحت الناموس.
19Basi, matendo ya kidunia yanajulikana: uzinzi, uasherati, ufisadi;
19واعمال الجسد ظاهرة التي هي زنى عهارة نجاسة دعارة
20kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, choyo, mabishano, mafarakano;
20عبادة الاوثان سحر عداوة خصام غيرة سخط تحزب شقاق بدعة
21husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine kama hayo. Nawaambieni tena kama nilivyokwisha sema: watu wanaotenda mambo hayo hawatakuwa na nafasi yao katika ufalme wa Mungu.
21حسد قتل سكر بطر وامثال هذه التي اسبق فاقول لكم عنها كما سبقت فقلت ايضا ان الذين يفعلون مثل هذه لا يرثون ملكوت الله.
22Lakini matokeo ya kuongozwa na Roho ni mapendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu,
22واما ثمر الروح فهو محبة فرح سلام طول اناة لطف صلاح ايمان
23upole na kuwa na kiasi. Hakuna Sheria inayoweza kupinga mambo hayo.
23وداعة تعفف. ضد امثال هذه ليس ناموس.
24Wale walio wa Kristo wameisulubisha hali yao ya kidunia pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
24ولكن الذين هم للمسيح قد صلبوا الجسد مع الاهواء والشهوات.
25Tukiishi kwa msaada wa Roho, na tuufuate mwongozo wake.
25ان كنا نعيش بالروح فلنسلك ايضا بحسب الروح.
26Basi, tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.
26لا نكن معجبين نغاضب بعضنا بعضا ونحسد بعضنا بعضا