1Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, ninyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa.
1ايها الاخوة ان انسبق انسان فأخذ في زلة ما فاصلحوا انتم الروحانيين مثل هذا بروح الوداعة ناظرا الى نفسك لئلا تجرب انت ايضا.
2Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.
2احملوا بعضكم اثقال بعض وهكذا تمموا ناموس المسيح.
3Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe.
3لانه ان ظن احد انه شيء وهو ليس شيئا فانه يغش نفسه.
4Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.
4ولكن ليمتحن كل واحد عمله وحينئذ يكون له الفخر من جهة نفسه فقط لا من جهة غيره.
5Maana kila mmoja anao mzigo wake mwenyewe wa kubeba.
5لان كل واحد سيحمل حمل نفسه
6Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
6ولكن ليشارك الذي يتعلّم الكلمة المعلّم في جميع الخيرات.
7Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.
7لا تضلوا. الله لا يشمخ عليه. فان الذي يزرعه الانسان اياه يحصد ايضا.
8Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele.
8لان من يزرع لجسده فمن الجسد يحصد فسادا. ومن يزرع للروح فمن الروح يحصد حياة ابدية.
9Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.
9فلا نفشل في عمل الخير لاننا سنحصد في وقته ان كنا لا نكل.
10Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
10فاذا حسبما لنا فرصة فلنعمل الخير للجميع ولا سيما لاهل الايمان
11Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe.
11انظروا ما اكبر الاحرف التي كتبتها اليكم بيدي.
12Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha ninyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.
12جميع الذين يريدون ان يعملوا منظرا حسنا في الجسد هؤلاء يلزمونكم ان تختتنوا لئلا يضطهدوا لاجل صليب المسيح فقط.
13Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki Sheria; huwataka ninyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu.
13لان الذين يختتنون هم لا يحفظون الناموس بل يريدون ان تختتنوا انتم لكي يفتخروا في جسدكم.
14Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.
14واما من جهتي فحاشا لي ان افتخر الا بصليب ربنا يسوع المسيح الذي به قد صلب العالم لي وانا للعالم.
15Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.
15لانه في المسيح يسوع ليس الختان ينفع شيئا ولا الغرلة بل الخليقة الجديدة.
16Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli--Wateule wa Mungu.
16فكل الذين يسلكون بحسب هذا القانون عليهم سلام ورحمة وعلى اسرائيل الله.
17Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
17في ما بعد لا يجلب احد عليّ اتعابا لاني حامل في جسدي سمات الرب يسوع
18Ndugu, nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Kristo. Amina.
18نعمة ربنا يسوع المسيح مع روحكم ايها الاخوة. آمين