Swahili: New Testament

American Standard Version

Ephesians

6

1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
1Children, obey your parents in the Lord: for this is right.
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
2Honor thy father and mother (which is the first commandment with promise),
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
3that it may be well with thee, and thou mayest live long on the earth.
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
4And, ye fathers, provoke not your children to wrath: but nurture them in the chastening and admonition of the Lord.
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
5Servants, be obedient unto them that according to the flesh are your masters, with fear and trembling, in singleness of your heart, as unto Christ;
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
6not in the way of eyeservice, as men-pleasers; but as servants of Christ, doing the will of God from the heart;
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
7with good will doing service, as unto the Lord, and not unto men:
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
8knowing that whatsoever good thing each one doeth, the same shall he receive again from the Lord, whether [he be] bond or free.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
9And, ye masters, do the same things unto them, and forbear threatening: knowing that he who is both their Master and yours is in heaven, and there is no respect of persons with him.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
10Finally, be strong in the Lord, and in the strength of his might.
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
11Put on the whole armor of God, that ye may be able to stand against the wiles of the devil.
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
12For our wrestling is not against flesh and blood, but against the principalities, against the powers, against the world-rulers of this darkness, against the spiritual [hosts] of wickedness in the heavenly [places].
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
13Wherefore take up the whole armor of God, that ye may be able to withstand in the evil day, and, having done all, to stand.
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
14Stand therefore, having girded your loins with truth, and having put on the breastplate of righteousness,
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
15and having shod your feet with the preparation of the gospel of peace;
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
16withal taking up the shield of faith, wherewith ye shall be able to quench all the fiery darts of the evil [one].
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
17And take the helmet of salvation, and the sword of the Spirit, which is the word of God:
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
18with all prayer and supplication praying at all seasons in the Spirit, and watching thereunto in all perseverance and supplication for all the saints,
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
19And on my behalf, that utterance may be given unto me in opening my mouth, to make known with boldness the mystery of the gospel,
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
20for which I am an ambassador in chains; that in it I may speak boldly, as I ought to speak.
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
21But that ye also may know my affairs, how I do, Tychicus, the beloved brother and faithful minister in the Lord, shall make known to you all things:
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
22whom I have sent unto you for this very purpose, that ye may know our state, and that he may comfort your hearts.
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
23Peace be to the brethren, and love with faith, from God the Father and the Lord Jesus Christ.
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.
24Grace be with all them that love our Lord Jesus Christ with [a love] incorruptible.