1Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
1Now a certain man was sick, Lazarus of Bethany, of the village of Mary and her sister Martha.
2Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
2And it was that Mary who anointed the Lord with ointment, and wiped his feet with her hair, whose brother Lazarus was sick.
3Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: "Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!"
3The sisters therefore sent unto him, saying, Lord, behold, he whom thou lovest is sick.
4Yesu aliposikia hivyo akasema, "Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe."
4But when Jesus heard it, he said, This sickness is not unto death, but for the glory of God, that the Son of God may be glorified thereby.
5Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
5Now Jesus loved Martha, and her sister, and Lazarus.
6Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
6When therefore he heard that he was sick, he abode at that time two days in the place where he was.
7Kisha akawaambia wanafunzi wake, "Twendeni tena Yudea!"
7Then after this he saith to the disciples, Let us go into Judaea again.
8Wanafunzi wakamwambia, "Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?"
8The disciples say unto him, Rabbi, the Jews were but now seeking to stone thee; and goest thou thither again?
9Yesu akajibu, "Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
9Jesus answered, Are there not twelve hours in the day? If a man walk in the day, he stumbleth not, because he seeth the light of this world.
10Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake."
10But if a man walk in the night, he stumbleth, because the light is not in him.
11Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, "Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha."
11These things spake he: and after this he saith unto them, Our friend Lazarus is fallen asleep; but I go, that I may awake him out of sleep.
12Wanafunzi wake wakamwambia, "Bwana, ikiwa amelala, basi atapona."
12The disciples therefore said unto him, Lord, if he is fallen asleep, he will recover.
13Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
13Now Jesus had spoken of his death: but they thought that he spake of taking rest in sleep.
14Basi, Yesu akawaambia waziwazi, "Lazaro amekufa;
14Then Jesus therefore said unto them plainly, Lazarus is dead.
15Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake."
15And I am glad for your sakes that I was not there, to the intent ye may believe; nevertheless let us go unto him.
16Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, "Twendeni nasi tukafe pamoja naye!"
16Thomas therefore, who is called Didymus, said unto his fellow-disciples, Let us also go, that we may die with him.
17Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
17So when Jesus came, he found that he had been in the tomb four days already.
18Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
18Now Bethany was nigh unto Jerusalem, about fifteen furlongs off;
19Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
19and many of the Jews had come to Martha and Mary, to console them concerning their brother.
20Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
20Martha therefore, when she heard that Jesus was coming, went and met him: but Mary still sat in the house.
21Martha akamwambia Yesu, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
21Martha therefore said unto Jesus, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
22Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa."
22And even now I know that, whatsoever thou shalt ask of God, God will give thee.
23Yesu akamwambia, "Kaka yako atafufuka."
23Jesus saith unto her, Thy brother shall rise again.
24Martha akamjibu, "Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho."
24Martha saith unto him, I know that he shall rise again in the resurrection at the last day.
25Yesu akamwambia, "Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
25Jesus said unto her, I am the resurrection, and the life: he that believeth on me, though he die, yet shall he live;
26na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?"
26and whosoever liveth and believeth on me shall never die. Believest thou this?
27Martha akamwambia, "Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni."
27She saith unto him, Yea, Lord: I have believed that thou art the Christ, the Son of God, [even] he that cometh into the world.
28Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, "Mwalimu yuko hapa, anakuita."
28And when she had said this, she went away, and called Mary her sister secretly, saying, The Teacher is her, and calleth thee.
29Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
29And she, when she heard it, arose quickly, and went unto him.
30Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
30(Now Jesus was not yet come into the village, but was still in the place where Martha met him.)
31Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
31The Jews then who were with her in the house, and were consoling her, when they saw Mary, that she rose up quickly and went out, followed her, supposing that she was going unto the tomb to weep there.
32Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!"
32Mary therefore, when she came where Jesus was, and saw him, fell down at his feet, saying unto him, Lord, if thou hadst been here, my brother had not died.
33Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
33When Jesus therefore saw her weeping, and the Jews [also] weeping who came with her, he groaned in the spirit, and was troubled,
34Kisha akawauliza, "Mlimweka wapi?" Wakamwambia, "Bwana, njoo uone."
34and said, Where have ye laid him? They say unto him, Lord, come and see.
35Yesu akalia machozi.
35Jesus wept.
36Basi, Wayahudi wakasema, "Tazameni jinsi alivyompenda!"
36The Jews therefore said, Behold how he loved him!
37Lakini baadhi yao wakasema, "Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?"
37But some of them said, Could not this man, who opened the eyes of him that was blind, have caused that this man also should not die?
38Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
38Jesus therefore again groaning in himself cometh to the tomb. Now it was a cave, and a stone lay against it.
39Yesu akasema, "Ondoeni hilo jiwe!" Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, "Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!"
39Jesus saith, Take ye away the stone. Martha, the sister of him that was dead, saith unto him, Lord, by this time the body decayeth; for he hath been [dead] four days.
40Yesu akamwambia, "Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?"
40Jesus saith unto her, Said I not unto thee, that, if thou believedst, thou shouldest see the glory of God?
41Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, "Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
41So they took away the stone. And Jesus lifted up his eyes, and said, Father, I thank thee that thou heardest me.
42Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma."
42And I knew that thou hearest me always: but because of the multitude that standeth around I said it, that they may believe that thou didst send me.
43Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: "Lazaro! Toka nje!"
43And when he had thus spoken, he cried with a loud voice, Lazarus, come forth.
44Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, "Mfungueni, mkamwache aende zake."
44He that was dead came forth, bound hand and foot with grave-clothes; and his face was bound about with a napkin. Jesus saith unto them, Loose him, and let him go.
45Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
45Many therefore of the Jews, who came to Mary and beheld that which he did, believed on him.
46Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
46But some of them went away to the Pharisees, and told them the things which Jesus had done.
47kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, "Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
47The chief priests therefore and the Pharisees gathered a council, and said, What do we? for this man doeth many signs.
48Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!"
48If we let him thus alone, all men will believe on him: and the Romans will come and take away both our place and our nation.
49Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, "Ninyi hamjui kitu!
49But a certain one of them, Caiaphas, being high priest that year, said unto them, Ye know nothing at all,
50Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?"
50nor do ye take account that it is expedient for you that one man should die for the people, and that the whole nation perish not.
51Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
51Now this he said not of himself: but, being high priest that year, he prophesied that Jesus should die for the nation;
52na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
52and not for the nation only, but that he might also gather together into one the children of God that are scattered abroad.
53Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
53So from that day forth they took counsel that they might put him to death.
54Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
54Jesus therefore walked no more openly among the Jews, but departed thence into the country near to the wilderness, into a city called Ephraim; and there he tarried with the disciples.
55Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
55Now the passover of the Jews was at hand: and many went up to Jerusalem out of the country before the passover, to purify themselves.
56Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, "Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?"
56They sought therefore for Jesus, and spake one with another, as they stood in the temple, What think ye? That he will not come to the feast?
57Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
57Now the chief priests and the Pharisees had given commandment, that, if any man knew where he was, he should show it, that they might take him.