Swahili: New Testament

American Standard Version

Luke

2

1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
1Now it came to pass in those days, there went out a decree from Caesar Augustus, that all the world should be enrolled.
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
2This was the first enrolment made when Quirinius was governor of Syria.
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
3And all went to enrol themselves, every one to his own city.
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
4And Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, into Judaea, to the city of David, which is called Bethlehem, because he was of the house and family of David;
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
5to enrol himself with Mary, who was betrothed to him, being great with child.
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
6And it came to pass, while they were there, the days were fulfilled that she should be delivered.
7akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
7And she brought forth her firstborn son; and she wrapped him in swaddling clothes, and laid him in a manger, because there was no room for them in the inn.
8Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
8And there were shepherds in the same country abiding in the field, and keeping watch by night over their flock.
9Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
9And an angel of the Lord stood by them, and the glory of the Lord shone round about them: and they were sore afraid.
10Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
10And the angel said unto them, Be not afraid; for behold, I bring you good tidings of great joy which shall be to all the people:
11Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
11for there is born to you this day in the city of David a Saviour, who is Christ the Lord.
12Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini."
12And this [is] the sign unto you: Ye shall find a babe wrapped in swaddling clothes, and lying in a manger.
13Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
13And suddenly there was with the angel a multitude of the heavenly host praising God, and saying,
14"Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
14Glory to God in the highest, And on earth peace among men in whom he is well pleased.
15Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: "Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha."
15And it came to pass, when the angels went away from them into heaven, the shepherds said one to another, Let us now go even unto Bethlehem, and see this thing that is come to pass, which the Lord hath made known unto us.
16Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
16And they came with haste, and found both Mary and Joseph, and the babe lying in the manger.
17Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
17And when they saw it, they made known concerning the saying which was spoken to them about this child.
18Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
18And all that heard it wondered at the things which were spoken unto them by the shepherds.
19Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
19But Mary kept all these sayings, pondering them in her heart.
20Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
20And the shepherds returned, glorifying and praising God for all the things that they had heard and seen, even as it was spoken unto them.
21Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
21And when eight days were fulfilled for circumcising him, his name was called JESUS, which was so called by the angel before he was conceived in the womb.
22Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
22And when the days of their purification according to the law of Moses were fulfilled, they brought him up to Jerusalem, to present him to the Lord
23Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana."
23(as it is written in the law of the Lord, Every male that openeth the womb shall be called holy to the Lord),
24Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
24and to offer a sacrifice according to that which is said in the law of the Lord, A pair of turtledoves, or two young pigeons.
25Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
25And behold, there was a man in Jerusalem whose name was Simeon; and this man was righteous and devout, looking for the consolation of Israel: and the Holy Spirit was upon him.
26Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
26And it had been revealed unto him by the Holy Spirit, that he should not see death, before he had seen the Lord's Christ.
27Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
27And he came in the Spirit into the temple: and when the parents brought in the child Jesus, that they might do concerning him after the custom of the law,
28Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
28then he received him into his arms, and blessed God, and said,
29"Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
29Now lettest thou thy servant depart, Lord, According to thy word, in peace;
30Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
30For mine eyes have seen thy salvation,
31ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
31Which thou hast prepared before the face of all peoples;
32Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."
32A light for revelation to the Gentiles, And the glory of thy people Israel.
33Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
33And his father and his mother were marvelling at the things which were spoken concerning him;
34Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, "Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
34and Simeon blessed them, and said unto Mary his mother, Behold, this [child] is set for the falling and the rising of many in Israel; and for a sign which is spoken against;
35na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako."
35yea and a sword shall pierce through thine own soul; that thoughts out of many hearts may be revealed.
36Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
36And there was one Anna, a prophetess, the daughter of Phanuel, of the tribe of Asher (she was of a great age, having lived with a husband seven years from her virginity,
37Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
37and she had been a widow even unto fourscore and four years), who departed not from the temple, worshipping with fastings and supplications night and day.
38Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
38And coming up at that very hour she gave thanks unto God, and spake of him to all them that were looking for the redemption of Jerusalem.
39Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
39And when they had accomplished all things that were according to the law of the Lord, they returned into Galilee, to their own city Nazareth.
40Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
40And the child grew, and waxed strong, filled with wisdom: and the grace of God was upon him.
41Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
41And his parents went every year to Jerusalem at the feast of the passover.
42Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
42And when he was twelve years old, they went up after the custom of the feast;
43Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
43and when they had fulfilled the days, as they were returning, the boy Jesus tarried behind in Jerusalem; and his parents knew it not;
44Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
44but supposing him to be in the company, they went a day's journey; and they sought for him among their kinsfolk and acquaintance:
45Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
45and when they found him not, they returned to Jerusalem, seeking for him.
46Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
46And it came to pass, after three days they found him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both hearing them, and asking them questions:
47Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
47and all that heard him were amazed at his understanding and his answers.
48Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni."
48And when they saw him, they were astonished; and his mother said unto him, Son, why hast thou thus dealt with us? behold, thy father and I sought thee sorrowing.
49Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?"
49And he said unto them, How is it that ye sought me? knew ye not that I must be in my Father's house?
50Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
50And they understood not the saying which he spake unto them.
51Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
51And he went down with them, and came to Nazareth; and he was subject unto them: and his mother kept all [these] sayings in her heart.
52Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
52And Jesus advanced in wisdom and stature, and in favor with God and men.