Swahili: New Testament

American Standard Version

Matthew

14

1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
1At that season Herod the tetrarch heard the report concerning Jesus,
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
2and said unto his servants, This is John the Baptist; he is risen from the dead; and therefore do these powers work in him.
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
3For Herod had laid hold on John, and bound him, and put him in prison for the sake of Herodias, his brother Philip's wife.
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
4For John said unto him, It is not lawful for thee to have her.
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
5And when he would have put him to death, he feared the multitude, because they counted him as a prophet.
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
6But when Herod's birthday came, the daughter of Herodias danced in the midst, and pleased Herod.
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
7Whereupon he promised with an oath to give her whatsoever she should ask.
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
8And she, being put forward by her mother, saith, Give me here on a platter the head of John the Baptist.
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
9And the king was grieved; but for the sake of his oaths, and of them that sat at meat with him, he commanded it to be given;
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
10and he sent and beheaded John in the prison.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
11And his head was brought on a platter, and given to the damsel: and she brought it to her mother.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
12And his disciples came, and took up the corpse, and buried him; and they went and told Jesus.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
13Now when Jesus heard [it], he withdrew from thence in a boat, to a desert place apart: and when the multitudes heard [thereof,] they followed him on foot from the cities.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
14And he came forth, and saw a great multitude, and he had compassion on them, and healed their sick.
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
15And when even was come, the disciples came to him, saying, The place is desert, and the time is already past; send the multitudes away, that they may go into the villages, and buy themselves food.
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
16But Jesus said unto them, They have no need to go away; give ye them to eat.
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
17And they say unto him, We have here but five loaves, and two fishes.
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
18And he said, Bring them hither to me.
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
19And he commanded the multitudes to sit down on the grass; and he took the five loaves, and the two fishes, and looking up to heaven, he blessed, and brake and gave the loaves to the disciples, and the disciples to the multitudes.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
20And they all ate, and were filled: and they took up that which remained over of the broken pieces, twelve baskets full.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
21And they that did eat were about five thousand men, besides women and children.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
22And straightway he constrained the disciples to enter into the boat, and to go before him unto the other side, till he should send the multitudes away.
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
23And after he had sent the multitudes away, he went up into the mountain apart to pray: and when even was come, he was there alone.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
24But the boat was now in the midst of the sea, distressed by the waves; for the wind was contrary.
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
25And in the fourth watch of the night he came unto them, walking upon the sea.
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
26And when the disciples saw him walking on the sea, they were troubled, saying, It is a ghost; and they cried out for fear.
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
27But straightway Jesus spake unto them, saying Be of good cheer; it is I; be not afraid.
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
28And Peter answered him and said, Lord, if it be thou, bid me come unto the upon the waters.
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
29And he said, Come. And Peter went down from the boat, and walked upon the waters to come to Jesus.
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
30But when he saw the wind, he was afraid; and beginning to sink, he cried out, saying, Lord, save me.
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
31And immediately Jesus stretched forth his hand, and took hold of him, and saith unto him, O thou of little faith, wherefore didst thou doubt?
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
32And when they were gone up into the boat, the wind ceased.
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
33And they that were in the boat worshipped him, saying, Of a truth thou art the Son of God.
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
34And when they had crossed over, they came to the land, unto Gennesaret.
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
35And when the men of that place knew him, they sent into all that region round about, and brought unto him all that were sick,
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.
36and they besought him that they might only touch the border of his garment: and as many as touched were made whole.