Swahili: New Testament

American Standard Version

Matthew

26

1Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
1And it came to pass, when Jesus had finished all these words, he said unto his disciples,
2"Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe."
2Ye know that after two days the passover cometh, and the Son of man is delivered up to be crucified.
3Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
3Then were gathered together the chief priests, and the elders of the people, unto the court of the high priest, who was called Caiaphas;
4Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
4and they took counsel together that they might take Jesus by subtlety, and kill him.
5Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
5But they said, Not during the feast, lest a tumult arise among people.
6Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
6Now when Jesus was in Bethany, in the house of Simon the leper,
7mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
7there came unto him a woman having an alabaster cruse of exceeding precious ointment, and she poured it upon his head, as he sat at meat.
8Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, "Ya nini hasara hii?
8But when the disciples saw it, they had indignation, saying, To what purpose is this waste?
9Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha."
9For this [ointment] might have been sold for much, and given to the poor.
10Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
10But Jesus perceiving it said unto them, Why trouble ye the woman? for she hath wrought a good work upon me.
11Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
11For ye have the poor always with you; but me ye have not always.
12Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
12For in that she poured this ointment upon my body, she did it to prepare me for burial.
13Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye."
13Verily I say unto you, Wheresoever this gospel shall be preached in the whole world, that also which this woman hath done shall be spoken of for a memorial of her.
14Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
14Then one of the twelve, who was called Judas Iscariot, went unto the chief priests,
15akawaambia, "Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?" Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
15and said, What are ye willing to give me, and I will deliver him unto you? And they weighed unto him thirty pieces of silver.
16na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
16And from that time he sought opportunity to deliver him [unto them.]
17Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, "Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?"
17Now on the first [day] of unleavened bread the disciples came to Jesus, saying, Where wilt thou that we make ready for thee to eat the passover?
18Yeye akawajibu, "Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu."
18And he said, Go into the city to such a man, and say unto him, The Teacher saith, My time is at hand; I keep the passover at thy house with my disciples.
19Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
19And the disciples did as Jesus appointed them; and they made ready the passover.
20Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
20Now when even was come, he was sitting at meat with the twelve disciples;
21Walipokuwa wakila, Yesu akasema, "Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti."
21and as they were eating, he said, Verily I say unto you, that one of you shall betray me.
22Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, "Bwana! Je, ni mimi?"
22And they were exceeding sorrowful, and began to say unto him every one, Is it I, Lord?
23Yesu akajibu, "Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
23And he answered and said, He that dipped his hand with me in the dish, the same shall betray me.
24Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa."
24The Son of man goeth, even as it is written of him: but woe unto that man through whom the Son of man is betrayed! good were it for that man if he had not been born.
25Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, "Mwalimu! Je, ni mimi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
25And Judas, who betrayed him, answered and said, Is it I, Rabbi? He saith unto him, Thou hast said.
26Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni mle; huu ni mwili wangu."
26And as they were eating, Jesus took bread, and blessed, and brake it; and he gave to the disciples, and said, Take, eat; this is my body.
27Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, "Nyweni nyote;
27And he took a cup, and gave thanks, and gave to them, saying, Drink ye all of it;
28maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
28for this is my blood of the covenant, which is poured out for many unto remission of sins.
29Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu."
29But I say unto you, I shall not drink henceforth of this fruit of the vine, until that day when I drink it new with you in my Father's kingdom.
30Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
30And when they had sung a hymn, they went out unto the mount of Olives.
31Kisha Yesu akawaambia, "Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
31Then saith Jesus unto them, All ye shall be offended in me this night: for it is written, I will smite the shepherd, and the sheep of the flock shall be scattered abroad.
32Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya."
32But after I am raised up, I will go before you into Galilee.
33Petro akamwambia Yesu "Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe."
33But Peter answered and said unto him, If all shall be offended in thee, I will never be offended.
34Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
34Jesus said unto him, Verily I say unto thee, that this night, before the cock crow, thou shalt deny me thrice.
35Petro akamwambia, "Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe." Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
35Peter saith unto him, Even if I must die with thee, [yet] will I not deny thee. Likewise also said all the disciples.
36Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, "Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali."
36Then cometh Jesus with them unto a place called Gethsemane, and saith unto his disciples, Sit ye here, while I go yonder and pray.
37Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
37And he took with him Peter and the two sons of Zebedee, and began to be sorrowful and sore troubled.
38Hapo akawaambia, "Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami."
38Then saith he unto them, My soul is exceeding sorrowful, even unto death: abide ye here, and watch with me.
39Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: "Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe."
39And he went forward a little, and fell on his face, and prayed, saying, My Father, if it be possible, let this cup pass away from me: nevertheless, not as I will, but as thou wilt.
40Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, "Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
40And he cometh unto the disciples, and findeth them sleeping, and saith unto Peter, What, could ye not watch with me one hour?
41Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu."
41Watch and pray, that ye enter not into temptation: the spirit indeed is willing, but the flesh is weak.
42Akaenda tena mara ya pili akasali: "Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike."
42Again a second time he went away, and prayed, saying, My Father, if this cannot pass away, except I drink it, thy will be done.
43Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
43And he came again and found them sleeping, for their eyes were heavy.
44Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
44And he left them again, and went away, and prayed a third time, saying again the same words.
45Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, "Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
45Then cometh he to the disciples, and saith unto them, Sleep on now, and take your rest: behold, the hour is at hand, and the Son of man is betrayed into the hands of sinners.
46Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti."
46Arise, let us be going: behold, he is at hand that betrayeth me.
47Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
47And while he yet spake, lo, Judas, one of the twelve, came, and with him a great multitude with swords and staves, from the chief priest and elders of the people.
48Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: "Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni."
48Now he that betrayed him gave them a sign, saying, Whomsoever I shall kiss, that is he: take him.
49Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, "Shikamoo, Mwalimu!" Kisha akambusu.
49And straightway he came to Jesus, and said, Hail, Rabbi; and kissed him.
50Yesu akamwambia, "Rafiki, fanya ulichokuja kufanya." Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
50And Jesus said unto him, Friend, [do] that for which thou art come. Then they came and laid hands on Jesus, and took him.
51Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
51And behold, one of them that were with Jesus stretched out his hand, and drew his sword, and smote the servant of the high priest, and struck off his ear.
52Hapo Yesu akamwambia, "Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
52Then saith Jesus unto him, Put up again thy sword into its place: for all they that take the sword shall perish with the sword.
53Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
53Or thinkest thou that I cannot beseech my Father, and he shall even now send me more than twelve legions of angels?
54Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?"
54How then should the scriptures be fulfilled that thus it must be?
55Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, "Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
55In that hour said Jesus to the multitudes, Are ye come out as against a robber with swords and staves to seize me? I sat daily in the temple teaching, and ye took me not.
56Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie." Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
56But all this is come to pass, that the scriptures of the prophets might be fulfilled. Then all the disciples left him, and fled.
57Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
57And they that had taken Jesus led him away to [the house of] Caiaphas the high priest, where the scribes and the elders were gathered together.
58Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
58But Peter followed him afar off, unto the court of the high priest, and entered in, and sat with the officers, to see the end.
59Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
59Now the chief priests and the whole council sought false witness against Jesus, that they might put him to death;
60lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
60and they found it not, though many false witnesses came. But afterward came two,
61wakasema, "Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu."
61and said, This man said, I am able to destroy the temple of God, and to build it in three days.
62Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, "Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?"
62And the high priest stood up, and said unto him, Answerest thou nothing? what is it which these witness against thee?
63Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, "Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!"
63But Jesus held his peace. And the high priest said unto him, I adjure thee by the living God, that thou tell us whether thou art the Christ, the Son of God.
64Yesu akamwambia, "Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni."
64Jesus said unto him, Thou hast said: nevertheless I say unto you, Henceforth ye shall see the Son of man sitting at the right hand of Power, and coming on the clouds of heaven.
65Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, "Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
65Then the high priest rent his garments, saying, He hath spoken blasphemy: what further need have we of witnesses? behold, now ye have heard the blasphemy:
66Ninyi mwaonaje?" Wao wakamjibu, "Anastahili kufa!"
66what think ye? They answered and said, He is worthy of death.
67Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
67Then did they spit in his face and buffet him: and some smote him with the palms of their hands,
68wakasema, "Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!"
68saying, Prophesy unto us, thou Christ: who is he that struck thee?
69Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, "Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya."
69Now Peter was sitting without in the court: and a maid came unto him, saying, Thou also wast with Jesus the Galilaean.
70Petro akakana mbele ya wote akisema, "Sijui hata unasema nini."
70But he denied before them all, saying, I know not what thou sayest.
71Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, "Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti."
71And when he was gone out into the porch, another [maid] saw him, and saith unto them that were there, This man also was with Jesus of Nazareth.
72Petro akakana tena kwa kiapo: "Simjui mtu huyo."
72And again he denied with an oath, I know not the man.
73Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, "Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha."
73And after a little while they that stood by came and said to Peter, Of a truth thou also art [one] of them; for thy speech maketh thee known.
74Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, "Simjui mtu huyo!" Mara jogoo akawika.
74Then began he to curse and to swear, I know not the man. And straightway the cock crew.
75Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: "Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu." Basi, akatoka nje akalia sana.
75And Peter remembered the word which Jesus had said, Before the cock crow, thou shalt deny me thrice. And he went out, and wept bitterly.