Swahili: New Testament

Croatian

John

11

1Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
1Bijaše neki bolesnik, Lazar iz Betanije, iz sela Marije i sestre joj Marte.
2Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
2Marija bijaše ono pomazala Gospodina pomašću i otrla mu noge svojom kosom. Njezin dakle brat Lazar bijaše bolestan.
3Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: "Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!"
3Sestre stoga poručiše Isusu: "Gospodine, evo onaj koga ljubiš, bolestan je."
4Yesu aliposikia hivyo akasema, "Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe."
4Čuvši to, Isus reče: "Ta bolest nije na smrt, nego na slavu Božju, da se po njoj proslavi Sin Božji."
5Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
5A Isus ljubljaše Martu i njezinu sestru i Lazara.
6Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
6Ipak, kad je čuo za njegovu bolest, ostade još dva dana u onome mjestu gdje se nalazio.
7Kisha akawaambia wanafunzi wake, "Twendeni tena Yudea!"
7Istom nakon toga reče učenicima: "Pođimo opet u Judeju!"
8Wanafunzi wakamwambia, "Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?"
8Kažu mu učenici: "Učitelju, Židovi su sad tražili da te kamenuju, pa da opet ideš onamo?"
9Yesu akajibu, "Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
9Odgovori Isus: "Nema li dan dvanaest sati? Hodi li tko danju, ne spotiče se jer vidi svjetlost ovoga svijeta.
10Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake."
10Hodi li tko noću, spotiče se jer nema svjetlosti u njemu."
11Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, "Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha."
11To reče, a onda im dometnu: "Lazar, prijatelj naš, spava, no idem probuditi ga."
12Wanafunzi wake wakamwambia, "Bwana, ikiwa amelala, basi atapona."
12Rekoše mu nato učenici: "Gospodine, ako spava, ozdravit će."
13Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
13No Isus to reče o njegovoj smrti, a oni pomisliše da govori o spavanju, o snu.
14Basi, Yesu akawaambia waziwazi, "Lazaro amekufa;
14Tada im Isus reče posve otvoreno: "Lazar je umro.
15Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake."
15Ja se radujem što ne bijah ondje, i to poradi vas - da uzvjerujete. Nego pođimo k njemu!"
16Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, "Twendeni nasi tukafe pamoja naye!"
16Nato Toma zvani Blizanac reče suučenicima: "Hajdemo i mi da umremo s njime!"
17Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
17Kad je dakle Isus stigao, nađe da je onaj već četiri dana u grobu.
18Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
18Betanija bijaše blizu Jeruzalema otprilike petnaest stadija.
19Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
19A mnogo Židova bijaše došlo tješiti Martu i Mariju zbog brata njihova.
20Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
20Kad Marta doču da Isus dolazi, pođe mu u susret dok je Marija ostala u kući.
21Martha akamwambia Yesu, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
21Marta reče Isusu: "Gospodine, da si bio ovdje, brat moj ne bi umro.
22Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa."
22Ali i sada znam: što god zaišteš od Boga, dat će ti."
23Yesu akamwambia, "Kaka yako atafufuka."
23Kaza joj Isus: "Uskrsnut će brat tvoj!"
24Martha akamjibu, "Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho."
24A Marta mu odgovori: "Znam da će uskrsnuti o uskrsnuću, u posljednji dan."
25Yesu akamwambia, "Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
25Reče joj Isus: "Ja sam uskrsnuće i život: tko u mene vjeruje, ako i umre, živjet će.
26na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?"
26I tko god živi i vjeruje u mene, neće umrijeti nikada. Vjeruješ li ovo?"
27Martha akamwambia, "Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni."
27Odgovori mu: "Da, Gospodine! Ja vjerujem da si ti Krist, Sin Božji, Onaj koji dolazi na svijet!"
28Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, "Mwalimu yuko hapa, anakuita."
28Rekavši to ode, zovnu svoju sestru Mariju i reče joj krišom: "Učitelj je ovdje i zove te."
29Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
29A ona, čim doču, brzo ustane i pođe k njemu.
30Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
30Isus još ne bijaše ušao u selo, nego je dotada bio na mjestu gdje ga je Marta susrela.
31Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
31Kad Židovi, koji su s Marijom bili u kući i tješili je, vidješe kako je brzo ustala i izišla, pođoše za njom; mišljahu da ide na grob plakati.
32Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!"
32A kad Marija dođe onamo gdje bijaše Isus i kad ga ugleda, baci mu se k nogama govoreći: "Gospodine, da si bio ovjde, brat moj ne bi umro."
33Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
33Kad Isus vidje kako plače ona i Židovi koji je dopratiše, potresen u duhu i uzbuđen
34Kisha akawauliza, "Mlimweka wapi?" Wakamwambia, "Bwana, njoo uone."
34upita: "Kamo ste ga položili?" Odgovoriše mu: "Gospodine, dođi i pogledaj!"
35Yesu akalia machozi.
35I zaplaka Isus.
36Basi, Wayahudi wakasema, "Tazameni jinsi alivyompenda!"
36Nato su Židovi govorili: "Gle, kako ga je ljubio!"
37Lakini baadhi yao wakasema, "Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?"
37A neki između njih rekoše: "Zar on, koji je slijepcu otvorio oči, nije mogao učiniti da ovaj ne umre?"
38Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
38Isus onda, ponovno potresen, pođe grobu. Bila je to pećina, a na nju navaljen kamen.
39Yesu akasema, "Ondoeni hilo jiwe!" Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, "Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!"
39Isus zapovjedi: "Odvalite kamen!" Kaže mu pokojnikova sestra Marta: "Gospodine, već zaudara. Ta četvrti je dan."
40Yesu akamwambia, "Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?"
40Kaže joj Isus: "Nisam li ti rekao: budeš li vjerovala, vidjet ćeš slavu Božju?"
41Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, "Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
41Odvališe dakle kamen. A Isus podiže oči i reče: "Oče, hvala ti što si me uslišao.
42Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma."
42Ja sam znao da me svagda uslišavaš; no rekoh to zbog nazočnog mnoštva: da vjeruju da si me ti poslao."
43Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: "Lazaro! Toka nje!"
43Rekavši to povika iza glasa: "Lazare, izlazi!"
44Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, "Mfungueni, mkamwache aende zake."
44I mrtvac iziđe, noge mu i ruke bile povezane povojima, a lice omotano ručnikom. Nato Isus reče: "Odriješite ga i pustite neka ide!"
45Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
45Tada mnogi Židovi koji bijahu došli k Mariji, kad vidješe što Isus učini, povjerovaše u nj.
46Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
46A neki od njih odu farizejima i pripovjede im što Isus učini.
47kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, "Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
47Stoga glavari svećenički i farizeji sazvaše Vijeće. Govorili su: "Što da radimo? Ovaj čovjek čini mnoga znamenja.
48Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!"
48Ako ga pustimo tako, svi će povjerovati u nj pa će doći Rimljani i oduzeti nam ovo mjesto i narod!"
49Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, "Ninyi hamjui kitu!
49A jedan od njih - Kajfa, veliki svećenik one godine - reče im: "Vi ništa ne znate.
50Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?"
50I ne mislite kako je za vas bolje da jedan čovjek umre za narod, nego da sav narod propadne!"
51Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
51To ne reče sam od sebe, nego kao veliki svećenik one godine prorokova da Isus ima umrijeti za narod;
52na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
52ali ne samo za narod nego i zato da raspršene sinove Božje skupi u jedno.
53Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
53Toga dana dakle odluče da ga ubiju.
54Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
54Zbog toga se Isus više nije javno kretao među Židovima, nego je odatle otišao u kraj blizu pustinje, u grad koji se zove Efrajim. Tu se zadržavao s učenicima.
55Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
55Bijaše blizu židovska Pasha i mnogi iz toga kraja uziđoše prije Pashe u Jeruzalem da se očiste.
56Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, "Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?"
56Iskahu dakle Isusa te se stojeći u Hramu zapitkivahu: "Što vam se čini? Zar on ne kani doći na Blagdan?"
57Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.
57A glavari svećenički i farizeji izdadoše naredbu: ako tko sazna gdje je, neka dojavi da ga uhvate.