Swahili: New Testament

Croatian

John

12

1Siku sita kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu alifika Bethania alikoishi Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka wafu.
1Šest dana prije Pashe dođe Isus u Betaniju gdje bijaše Lazar koga je Isus uskrisio od mrtvih.
2Huko walimwandalia chakula cha jioni, naye Martha akawa anawatumikia. Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa mezani pamoja na Yesu.
2Ondje mu prirediše večeru. Marta posluživaše, a Lazar bijaše jedan od njegovih sustolnika.
3Basi, Maria alichukua chupa ya marashi ya nardo safi ya thamani kubwa, akampaka Yesu miguu na kuipangusa kwa nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marashi.
3Tada Marija uzme libru prave dragocjene nardove pomasti, pomaže Isusu noge i otare ih svojom kosom. I sva se kuća napuni mirisom pomasti.
4Basi, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
4Nato reče Juda Iškariotski, jedan od njegovih učenika, onaj koji ga je imao izdati:
5"Kwa nini marashi hayo hayakuuzwa kwa fedha dinari mia tatu, wakapewa maskini?"
5"Zašto se ta pomast nije prodala za trista denara i razdala siromasima?"
6Alisema hivyo, si kwa kuwa alijali chochote juu ya maskini, bali kwa sababu alikuwa mweka hazina, na kwa kuwa alikuwa mwizi, mara kwa mara aliiba kutoka katika hiyo hazina.
6To ne reče zbog toga što mu bijaše stalo do siromaha, nego što bijaše kradljivac: kako je imao kesu, kradom je uzimao što se u nju stavljalo.
7Lakini Yesu akasema, "Msimsumbue huyu mama! Mwacheni ayaweke kwa ajili ya siku ya mazishi yangu.
7Nato Isus odvrati: "Pusti je! Neka to izvrši za dan mog ukopa!
8Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote."
8Jer siromahe imate uvijek uza se, a mene nemate uvijek."
9Wayahudi wengi walisikia kwamba Yesu alikuwa Bethania. Basi, wakafika huko si tu kwa ajili ya kumwona Yesu, ila pia wapate kumwona Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka wafu.
9Silno mnoštvo Židova dozna da je Isus ondje pa se okupi, ne samo zbog Isusa, već i zato da vide Lazara kojega on bijaše uskrisio od mrtvih.
10Makuhani wakuu waliamua pia kumwua Lazaro,
10A glavari svećenički odlučiše i Lazara ubiti
11Maana kwa sababu ya Lazaro Wayahudi wengi waliwaasi viongozi wao, wakamwamini Yesu.
11jer su zbog njega mnogi Židovi odlazili i vjerovali u Isusa.
12Kesho yake, kundi kubwa la watu waliokuja kwenye sikukuu walisikia kuwa Yesu alikuwa njiani kuja Yerusalemu.
12Kad je sutradan silan svijet koji dođe na Blagdan čuo da Isus dolazi u Jeruzalem,
13Basi, wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki; wakapaaza sauti wakisema: "Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana. Abarikiwe mfalme wa Israeli."
13uze palmove grančice i iziđe mu u susret. Vikahu: "Hosana! Blagoslovljen Onaj koji dolazi u ime Gospodnje! Kralj Izraelov."
14Yesu akampata mwana punda mmoja akapanda juu yake kama yasemavyo Maandiko:
14A Isus nađe magarčića i sjede na nj kao što je pisano:
15"Usiogope mji wa Sioni! Tazama, Mfalme wako anakuja, Amepanda mwana punda."
15Ne boj se, kćeri Sionska! Evo, kralj tvoj dolazi jašuć na mladetu magaričinu!
16Wakati huo wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipokwisha tukuzwa, ndipo walipokumbuka kwamba hayo yalikuwa yameandikwa juu yake, na kwamba watu walikuwa wamemtendea hivyo.
16To učenici njegovi isprva ne razumješe. Ali pošto je Isus bio proslavljen, prisjetiše se da je to bilo o njemu napisano i da mu baš to učiniše.
17Kundi la watu wale waliokuwa pamoja naye wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua kutoka wafu, walisema yaliyotukia.
17Mnoštvo koje bijaše s njime kad Lazara pozva iz groba i uskrisi od mrtvih pronosilo je svjedočanstvo o tome.
18Kwa hiyo umati huo wa watu ulimlaki, maana wote walisikia kwamba Yesu alikuwa amefanya ishara hiyo.
18Stoga mu je i izišao u susret silan svijet: pročulo se da je on učinio to znamenje.
19Basi, Mafarisayo wakaambiana, "Mnaona? Hatuwezi kufanya chochote! Tazameni, ulimwengu wote unamfuata."
19Farizeji nato rekoše među sobom: "Vidite da ništa ne postižete. Eno, svijet ode za njim!"
20Kulikuwa na Wagiriki kadhaa miongoni mwa watu waliokuwa wamefika Yerusalemu kuabudu wakati wa sikukuu hiyo.
20A među onima koji su se došli klanjati na Blagdan bijahu i neki Grci.
21Hao walimwendea Filipo, mwenyeji wa Bethsaida katika Galilaya, wakasema, "Mheshimiwa, tunataka kumwona Yesu."
21Oni pristupe Filipu iz Betsaide galilejske pa ga zamole: "Gospodine, htjeli bismo vidjeti Isusa."
22Filipo akaenda akamwambia Andrea, nao wawili wakaenda kumwambia Yesu.
22Filip ode i kaže to Andriji pa Andrija i Filip odu i kažu Isusu.
23Yesu akawaambia, "Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mtu imefika!
23Isus im odgovori: "Došao je čas da se proslavi Sin Čovječji.
24Kweli nawaambieni, punje ya ngano hubaki punje tu isipokuwa ikianguka katika udongo na kufa. Kama ikifa, basi huzaa matunda mengi.
24Zaista, zaista, kažem vam: ako pšenično zrno, pavši na zemlju, ne umre, ostaje samo; ako li umre, donosi obilat rod.
25Anayependa maisha yake, atayapoteza; anayeyachukia maisha yake katika ulimwengu huu, atayaweka kwa ajili ya uzima wa milele.
25Tko ljubi svoj život, izgubit će ga. A tko mrzi svoj život na ovome svijetu, sačuvat će ga za život vječni.
26Anayetaka kunitumikia ni lazima anifuate, hivyo kwamba popote pale nilipo mimi ndipo na mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu yeyote anayenitumikia Baba yangu atampa heshima.
26Ako mi tko hoće služiti, neka ide za mnom. I gdje sam ja, ondje će biti i moj služitelj. Ako mi tko hoće služiti, počastit će ga moj Otac."
27"Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: Baba, usiruhusu saa hii inifikie? Lakini ndiyo maana nimekuja--ili nipite katika saa hii.
27"Duša mi je sada potresena i što da kažem? Oče, izbavi me iz ovoga časa? No, zato dođoh u ovaj čas!
28Baba, ulitukuze jina lako." Hapo sauti ikasema kutoka mbinguni, "Nimelitukuza, na nitalitukuza tena."
28Oče, proslavi ime svoje!" Uto dođe glas s neba: "Proslavio sam i opet ću proslaviti!"
29Umati wa watu waliokuwa wamesimama hapo walisikia sauti hiyo, na baadhi yao walisema, "Malaika ameongea naye!"
29Mnoštvo koje je ondje stajalo i slušalo govoraše: "Zagrmjelo je!" Drugi govorahu: "Anđeo mu je zborio."
30Lakini Yesu akawaambia, "Sauti hiyo haikutokea kwa ajili yangu mimi, ila kwa ajili yenu.
30Isus na to reče: "Ovaj glas nije bio poradi mene, nego poradi vas."
31Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu atapinduliwa.
31"Sada je sud ovomu svijetu, sada će knez ovoga svijeta biti izbačen.
32Nami nitakapoinuliwa juu ya nchi nitamvuta kila mmoja kwangu."
32A ja kad budem uzdignut sa zemlje, sve ću privući k sebi."
33(Kwa kusema hivyo alionyesha atakufa kifo gani).
33To reče da označi kakvom će smrću umrijeti.
34Basi, umati huo ukamjibu, "Sisi tunaambiwa na Sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?"
34Nato mu mnoštvo odgovori: "Mi smo iz Zakona čuli da Krist ostaje zauvijek. Kako onda ti govoriš da Sin Čovječji treba da bude uzdignut? Tko je taj Sin Čovječji?"
35Yesu akawaambia, "Mwanga bado uko nanyi kwa muda mfupi. Tembeeni mngali mnao huo mwanga ili giza lisiwapate; maana atembeaye gizani hajui aendako.
35Isus im nato reče: "Još je malo vremena svjetlost među vama. Hodite dok imate svjetlost da vas ne obuzme tama. Tko hodi u tami, ne zna kamo ide.
36Basi, wakati mnao huo mwanga uaminini ili mpate kuwa watu wa mwanga." Baada ya kusema maneno hayo, Yesu alikwenda zake na kujificha mbali nao.
36Dok imate svjetlost, vjerujte u svjetlost da budete sinovi svjetlosti!" To Isus doreče, a onda ode i sakri se od njih.
37Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.
37Iako je Isus pred njima učinio tolika znamenja, oni ne povjerovaše u njega,
38Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia: "Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu? Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?"
38da se ispuni riječ koju kaza prorok Izaija: Gospodine! Tko povjerova našoj poruci? Kome li se otkri ruka Gospodnja?
39Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya tena alisema:
39Stoga i ne mogahu vjerovati, jer Izaija dalje kaže:
40"Mungu ameyapofusha macho yao, amezipumbaza akili zao; wasione kwa macho yao, wasielewe kwa akili zao; wala wasinigeukie, asema Bwana, ili nipate kuwaponya."
40Zaslijepi im oči, stvrdnu srca; da očima ne vide, srcem ne razumiju te se ne obrate pa ih ozdravim.
41Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliuona utukufu wa Yesu, akasema habari zake.
41Reče to Izaija jer je vidio slavu njegovu te o njemu zborio.
42Hata hivyo, wengi wa viongozi wa Wayahudi walimwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakumkiri hadharani kwa kuogopa kwamba watatengwa na sunagogi.
42Ipak, mnogi su i od glavara vjerovali u njega, ali zbog farizeja nisu to priznavali: da ne budu izopćeni iz sinagoge.
43Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu
43Jer više im je bilo do slave ljudske, nego do slave Božje.
44Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, "Mtu aliyeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.
44A Isus povika: "Tko u mene vjeruje, ne vjeruje u mene, nego u onoga koji me posla;
45Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
45i tko vidi mene, vidi onoga koji me posla.
46Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani.
46Ja - Svjetlost - dođoh na svijet da nijedan koji u mene vjeruje u tami ne ostane.
47Anayeyasikia maneno yangu lakini hayashiki mimi sitamhukumu; maana sikuja kuhukumu ulimwengu bali kuuokoa.
47I sluša li tko moje riječi, a ne čuva ih, ja ga ne sudim. Ja nisam došao suditi svijetu, nego svijet spasiti.
48Asiyeyashika maneno yangu anaye wa kumhukumu: neno lile nililosema ni hakimu wake siku ya mwisho.
48Tko mene odbacuje i riječi mojih ne prima, ima svoga suca: riječ koju sam zborio - ona će mu suditi u posljednji dan.
49Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini.
49Jer nisam ja zborio sam od sebe, nego onaj koji me posla - Otac - on mi dade zapovijed što da kažem, što da zborim.
50Nami najua kuwa amri yake huleta uzima wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme."
50I znam: zapovijed njegova jest život vječni. Što ja dakle zborim, tako zborim kako mi je rekao Otac."