Swahili: New Testament

Croatian

John

13

1Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
1Bijaše pred blagdan Pashe. Isus je znao da je došao njegov čas da prijeđe s ovoga svijeta Ocu, budući da je ljubio svoje, one u svijetu, do kraja ih je ljubio.
2Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
2I za večerom je đavao već bio ubacio u srce Judi Šimuna Iškariotskoga da ga izda.
3Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
3A Isus je znao da mu je Otac sve predao u ruke i da je od Boga izišao te da k Bogu ide pa
4Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
4usta od večere, odloži haljine, uze ubrus i opasa se.
5Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
5Nalije zatim vodu u praonik i počne učenicima prati noge i otirati ih ubrusom kojim je bio opasan.
6Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, "Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?"
6Dođe tako do Šimuna Petra. A on će mu: "Gospodine! Zar ti da meni pereš noge?"
7Yesu akamjibu, "Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye."
7Odgovori mu Isus: "Što ja činim, ti sada ne znaš, ali shvatit ćeš poslije."
8Petro akamwambia, "Wewe hutaniosha miguu kamwe!" Yesu akamjibu, "Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena."
8Reče mu Petar: "Nećeš mi prati nogu nikada!" Isus mu odvrati: "Ako te ne operem, nećeš imati dijela sa mnom."
9Simoni Petro akamwambia, "Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia."
9Nato će mu Šimun Petar: "Gospodine, onda ne samo noge, nego i ruke i glavu!"
10Yesu akamwambia, "Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote."
10Kaže mu Isus: "Tko je okupan, ne treba drugo da opere nego noge - i sav je čist! I vi ste čisti, ali ne svi!"
11(Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: "Ninyi mmetakata, lakini si nyote.")
11Jer znao je tko će ga izdati. Stoga je i rekao: "Niste svi čisti."
12Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, "Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
12Kad im dakle opra noge, uze svoje haljine, opet sjede i reče im: "Razumijete li što sam vam učinio?
13Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
13Vi me zovete Učiteljem i Gospodinom. Pravo velite jer to i jesam!
14Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
14Ako dakle ja - Gospodin i Učitelj - vama oprah noge, treba da i vi jedni drugima perete noge.
15Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
15Primjer sam vam dao da i vi činite kao što ja vama učinih."
16Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
16Zaista, zaista, kažem vam: nije sluga veći od gospodara niti poslanik od onoga koji ga posla.
17Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
17Ako to znate, blago vama budete li tako i činili!"
18"Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
18"Ne govorim o svima vama! Ja znam koje izabrah! Ali - neka se ispuni Pismo: Koji blaguje kruh moj, petu na me podiže."
19Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
19"Već vam sada kažem, prije negoli se dogodi, da kad se dogodi vjerujete da Ja jesam.
20Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma."
20Zaista, zaista, kažem vam: Tko primi onoga kojega ja šaljem, mene prima. A tko mene primi, prima onoga koji je mene poslao."
21Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, "Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!"
21Rekavši to, potresen u duhu Isus posvjedoči: "Zaista, zaista, kažem vam: jedan će me od vas izdati!"
22Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
22Učenici se zgledahu među sobom u nedoumici o kome to govori.
23Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
23A jedan od njegovih učenika - onaj kojega je Isus ljubio - bijaše za stolom Isusu do krila.
24Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: "Mwulize anasema juu ya nani."
24Šimun Petar dade mu znak i reče: "Pitaj tko je taj o kome govori."
25Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, "Bwana, ni nani?"
25Ovaj se privine Isusu uz prsa i upita: "Gospodine, tko je taj?"
26Yesu akajibu, "Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye." Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
26Isus odgovori: "Onaj je kome ja dadnem umočen zalogaj."
27Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, "Unachotaka kufanya, kifanye haraka!"
27Tada umoči zalogaj, uze ga i dade Judi Šimuna Iškariotskoga. Nakon zalogaja uđe u nj Sotona. Nato mu Isus reče: "Što činiš, učini brzo!"
28Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
28Nijedan od sustolnika nije razumio zašto mu je to rekao.
29Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
29Budući da je Juda imao kesu, neki su mislili da mu je Isus rekao: "Kupi što nam treba za blagdan!" - ili neka poda nešto siromasima.
30Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
30On dakle uzme zalogaj i odmah iziđe. A bijaše noć.
31Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, "Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
31Pošto Juda iziđe, reče Isus: "Sada je proslavljen Sin Čovječji i Bog se proslavio u njemu!
32Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
32Ako se Bog proslavio u njemu, i njega će Bog proslaviti u sebi, i uskoro će ga proslaviti!
33"Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
33Dječice, još sam malo s vama. Tražit ćete me, ali kao što rekoh Židovima, kažem sada i vama: kamo ja odlazim, vi ne možete doći.
34Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
34Zapovijed vam novu dajem: ljubite jedni druge; kao što sam ja ljubio vas tako i vi ljubite jedni druge.
35Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu."
35Po ovom će svi znati da ste moji učenici: ako budete imali ljubavi jedni za druge."
36Simoni Petro akamwuliza, "Bwana, unakwenda wapi?" Yesu akajibu, "Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye."
36Kaže mu Šimun Petar: "Gospodine, kamo to odlaziš?" Isus mu odgovori: "Kamo ja odlazim, ti zasad ne možeš poći za mnom. No poći ćeš poslije."
37Petro akamwambia "Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!"
37Nato će mu Petar: "Gospodine, a zašto sada ne bih mogao poći za tobom? Život ću svoj položiti za tebe!"
38Yesu akajibu, "Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!"
38Odgovori Isus: "Život ćeš svoj položiti za mene? Zaista, zaista, kažem ti: Pijetao neće zapjevati dok me triput ne zatajiš."