Swahili: New Testament

Croatian

John

6

1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
1Nakon toga ode Isus na drugu stranu Galilejskog, Tiberijadskog mora.
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
2Slijedilo ga silno mnoštvo jer su gledali znamenja što ih je činio na bolesnicima.
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
3A Isus uziđe na goru i ondje sjeđaše sa svojim učenicima.
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
4Bijaše blizu Pasha, židovski blagdan.
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
5Isus podigne oči i ugleda kako silan svijet dolazi k njemu pa upita Filipa: "Gdje da kupimo kruha da ovi blaguju?"
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
6To reče kušajući ga; jer znao je što će učiniti.
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
7Odgovori mu Filip: "Za dvjesta denara kruha ne bi bilo dosta da svaki nešto malo dobije."
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
8Kaže mu jedan od njegovih učenika, Andrija, brat Šimuna Petra:
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
9"Ovdje je dječak koji ima pet ječmenih kruhova i dvije ribice! Ali što je to za tolike?"
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
10Reče Isus: "Neka ljudi posjedaju!" A bilo je mnogo trave na tome mjestu. Posjedaše dakle muškarci, njih oko pet tisuća.
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
11Isus uze kruhove, izreče zahvalnicu pa razdijeli onima koji su posjedali. A tako i od ribica - koliko su god htjeli.
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
12A kad se nasitiše, reče svojim učenicima: "Skupite preostale ulomke da ništa ne propadne!"
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
13Skupili su dakle i napunili dvanaest košara ulomaka što od pet ječmenih kruhova pretekoše onima koji su blagovali.
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
14Kad su ljudi vidjeli znamenje što ga Isus učini, rekoše: "Ovo je uistinu Prorok koji ima doći na svijet!"
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
15Kad Isus spozna da kane doći, pograbiti ga i zakraljiti, povuče se ponovno u goru, posve sam.
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
16Kad nasta večer, siđoše njegovi učenici k moru,
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
17uđoše u lađicu i krenuše na onu stranu mora, u Kafarnaum. Već se i smrklo, a Isusa još nikako k njima.
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
18More se uzburkalo od silnog vjetra što je zapuhao.
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
19Pošto su dakle isplovili oko dvadeset i pet do trideset stadija, ugledaju Isusa gdje ide po moru i približava se lađici. Prestraše se,
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
20a on će njima: "Ja sam! Ne bojte se!"
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
21Htjedoše ga uzeti u lađicu, kadli se lađica odmah nađe na obali kamo su se zaputili.
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
22Sutradan mnoštvo, koje osta s onu stranu mora, zapazi da ondje bijaše samo jedna lađica i da Isus nije bio ušao zajedno sa svojim učenicima u lađicu, nego da oni odoše sami.
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
23Iz Tiberijade pak stigoše druge lađice blizu onog mjesta gdje jedoše kruh pošto je Gospodin izrekao zahvalnicu.
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
24Kada dakle mnoštvo vidje da ondje nema Isusa ni njegovih učenika, uđu u lađice i odu u Kafarnaum tražeći Isusa.
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
25Kad ga nađoše s onu stranu mora, rekoše mu: "Učitelju, kad si ovamo došao?"
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
26Isus im odgovori: "Zaista, zaista, kažem vam: tražite me, ali ne stoga što vidjeste znamenja, nego stoga što ste jeli od onih kruhova i nasitili se.
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
27Radite, ali ne za hranu propadljivu, nego za hranu koja ostaje za život vječni: nju će vam dati Sin Čovječji jer njega Otac - Bog - opečati."
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
28Rekoše mu dakle: "Što nam je činiti da bismo radili djela Božja?"
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
29Odgovori im Isus: "Djelo je Božje da vjerujete u onoga kojega je on poslao."
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
30Rekoše mu onda: "Kakvo ti znamenje činiš da vidimo pa da ti vjerujemo? Koje je tvoje djelo?
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
31Očevi naši blagovaše manu u pustinji, kao što je pisano: Nahrani ih kruhom nebeskim."
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
32Reče im Isus: "Zaista, zaista, kažem vam: nije vam Mojsije dao kruh s neba, nego Otac moj daje vam kruh s neba, kruh istinski;
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
33jer kruh je Božji Onaj koji silazi s neba i daje život svijetu."
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
34Rekoše mu nato: "Gospodine, daj nam uvijek toga kruha."
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
35Reče im Isus: "Ja sam kruh života. Tko dolazi k meni, neće ogladnjeti; tko vjeruje u mene, neće ožednjeti nikada.
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
36No rekoh vam: vidjeli ste me, a opet ne vjerujete.
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
37Svi koje mi daje Otac doći će k meni, i onoga tko dođe k meni neću izbaciti;
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
38jer siđoh s neba ne da vršim svoju volju, nego volju onoga koji me posla.
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
39A ovo je volja onoga koji me posla: da nikoga od onih koje mi je dao ne izgubim, nego da ih uskrisim u posljednji dan.
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
40Da, to je volja Oca mojega da tko god vidi Sina i vjeruje u njega, ima život vječni i ja da ga uskrisim u posljednji dan."
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
41Židovi nato mrmljahu protiv njega što je rekao: "Ja sam kruh koji je sišao s neba."
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
42Govorahu: "Nije li to Isus, sin Josipov? Ne poznajemo li mu oca i majku? Kako sada govori: 'Sišao sam s neba?'"
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
43Isus im odvrati: "Ne mrmljajte među sobom!
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
44Nitko ne može doći k meni ako ga ne povuče Otac koji me posla; i ja ću ga uskrisiti u posljednji dan.
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
45Pisano je u Prorocima: Svi će biti učenici Božji. Tko god čuje od Oca i pouči se, dolazi k meni.
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
46Ne da bi tko vidio Oca, doli onaj koji je kod Boga; on je vidio Oca.
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
47Zaista, zaista, kažem vam: tko vjeruje, ima život vječni.
48Mimi ni mkate wa uzima.
48Ja sam kruh života.
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
49Očevi vaši jedoše u pustinji manu i pomriješe.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
50Ovo je kruh koji silazi s neba: da tko od njega jede, ne umre.
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
51Ja sam kruh živi koji je s neba sišao. Tko bude jeo od ovoga kruha, živjet će uvijeke. Kruh koji ću ja dati tijelo je moje - za život svijeta."
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
52Židovi se nato među sobom prepirahu: "Kako nam ovaj može dati tijelo svoje za jelo?"
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
53Reče im stoga Isus: "Zaista, zaista, kažem vam: ako ne jedete tijela Sina Čovječjega i ne pijete krvi njegove, nemate života u sebi!
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
54Tko blaguje tijelo moje i pije krv moju, ima život vječni; i ja ću ga uskrisiti u posljednji dan.
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
55Tijelo je moje jelo istinsko, krv je moja piće istinsko.
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
56Tko jede moje tijelo i pije moju krv, u meni ostaje i ja u njemu.
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
57Kao što je mene poslao živi Otac i ja živim po Ocu, tako i onaj koji mene blaguje živjet će po meni.
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
58Ovo je kruh koji je s neba sišao, ne kao onaj koji jedoše očevi i pomriješe. Tko jede ovaj kruh, živjet će uvijeke."
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
59To reče Isus naučavajući u sinagogi u Kafarnaumu.
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
60Mnogi od njegovih učenika čuvši to rekoše: "Tvrda je to besjeda! Tko je može slušati?"
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
61A Isus znajući sam od sebe da njegovi učenici zbog toga mrmljaju, reče im: "Zar vas to sablažnjava?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
62A što ako vidite Sina Čovječjega kako uzlazi onamo gdje je prije bio?"
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
63"Duh je onaj koji oživljuje, tijelo ne koristi ništa. Riječi koje sam vam govorio duh su i život su."
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
64"A ipak, ima ih među vama koji ne vjeruju." Jer znao je Isus od početka koji su oni što ne vjeruju i tko je onaj koji će ga izdati.
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
65I doda: "Zato sam vam i rekao da nitko ne može doći k meni ako mu nije dano od Oca."
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
66Otada mnogi učenici odstupiše, više nisu išli s njime.
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
67Reče stoga Isus dvanaestorici: "Da možda i vi ne kanite otići?"
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
68Odgovori mu Šimun Petar: "Gospodine, kome da idemo? Ti imaš riječi života vječnoga!
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
69I mi vjerujemo i znamo: ti si Svetac Božji."
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
70Odgovori im Isus: "Nisam li ja vas dvanaestoricu izabrao? A ipak, jedan je od vas đavao."
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.
71Govoraše to o Judi, sinu Šimuna Iškariotskoga, jednom od dvanaestorice, jer on ga je imao izdati.