1Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
1Nakon toga Isus je obilazio po Galileji; nije htio u Judeju jer su Židovi tražili da ga ubiju.
2Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
2Bijaše blizu židovski Blagdan sjenica.
3Basi ndugu zake wakamwambia, "Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
3Rekoše mu stoga njegova braća: "Otiđi odavle i pođi u Judeju da i tvoji učenici vide djela što činiš.
4Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu."
4Ta tko želi biti javno poznat, ne čini ništa u tajnosti. Ako već činiš sve to, očituj se svijetu."
5(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
5Jer ni braća njegova nisu vjerovala u njega.
6Basi, Yesu akawaambia, "Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
6Reče im nato Isus: "Moje vrijeme još nije došlo, a za vas je vrijeme svagda pogodno.
7Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
7Vas svijet ne može mrziti, ali mene mrzi jer ja svjedočim protiv njega: da su mu djela opaka.
8Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika."
8Vi samo uziđite na blagdan. Ja još ne uzlazim na ovaj blagdan jer moje se vrijeme još nije ispunilo."
9Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
9To im reče i ostade u Galileji.
10Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
10Ali pošto njegova braća uziđoše na blagdan, uziđe i on, ne javno, nego potajno.
11Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: "Yuko wapi?"
11A Židovi su ga tražili o blagdanu pitajući : "Gdje je onaj?"
12Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, "Ni mtu mwema." Wengine walisema, "La! Anawapotosha watu."
12I među mnoštvom o njemu se mnogo šaptalo. Jedni govorahu: "Dobar je!" Drugi pak: "Ne, nego zavodi narod."
13Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
13Ipak nitko nije otvoreno govorio o njemu zbog straha od Židova.
14Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
14Usred blagdana uziđe Isus u Hram i stade naučavati.
15Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema "Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?"
15Židovi se u čudu pitahu: "Kako ovaj znade Pisma, a nije učio?"
16Hapo Yesu akawajibu, "Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
16Nato im Isus odvrati: "Moj nauk nije moj, nego onoga koji me posla.
17Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
17Ako tko hoće vršiti volju njegovu, prepoznat će da li je taj nauk od Boga ili ja sam od sebe govorim.
18Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
18Tko sam od sebe govori, svoju slavu traži, a tko traži slavu onoga koji ga posla, taj je istinit i nema u njemu nepravednosti.
19Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?"
19Nije li vam Mojsije dao Zakon? Pa ipak nitko od vas ne vrši Zakona." "Zašto tražite da me ubijete?"
20Hapo watu wakamjibu, "Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?"
20Odgovori mnoštvo: "Zloduha imaš! Tko traži da te ubije?"
21Yesu akawajibu, "Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
21Uzvrati im Isus: "Jedno djelo učinih i svi se čudite.
22Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
22Mojsije vam dade obrezanje - ne, ono i nije od Mojsija, nego od otaca - i vi u subotu obrezujete čovjeka.
23Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
23Ako čovjek može primiti obrezanje u subotu da se ne prekrši Mojsijev zakon, zašto se ljutite na mene što sam svega čovjeka ozdravio u subotu?
24Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki."
24Ne sudite po vanjštini, nego sudite sudom pravednim!"
25Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, "Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
25Rekoše tada neki Jeruzalemci: "Nije li to onaj koga traže da ga ubiju?
26Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
26A evo, posve otvoreno govori i ništa mu ne kažu. Da nisu možda i glavari doista upoznali da je on Krist?
27Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!"
27Ali za njega znamo odakle je, a kad Krist dođe, nitko neće znati odakle je!"
28Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, "Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
28Nato Isus, koji je učio u Hramu, povika: "Da! Poznajete me i znate odakle sam! A ipak ja nisam došao sam od sebe: postoji jedan istiniti koji me posla. Njega vi ne znate.
29Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma."
29Ja ga znadem jer sam od njega i on me poslao."
30Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
30Židovi su otad vrebali da ga uhvate. Ipak nitko ne stavi na nj ruke jer još nije bio došao njegov čas.
31Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, "Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?"
31A mnogi iz mnoštva povjerovaše u nj te govorahu: "Zar će Krist, kada dođe, činiti više znamenja nego što ih ovaj učini?"
32Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
32Dočuli farizeji da se to u mnoštvu o njemu šapće. Stoga glavari svećenički i farizeji poslaše stražare da ga uhvate.
33Yesu akasema, "Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
33Tada Isus reče: "Još sam malo vremena s vama i odlazim onomu koji me posla.
34Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika."
34Tražit ćete me i nećete me naći; gdje sam ja, vi ne možete doći."
35Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, "Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
35Rekoše nato Židovi među sobom: "Kamo to ovaj kani da ga mi nećemo naći? Da ne kani poći raseljenima među Grcima i naučavati Grke?
36Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?"
36Što li znači besjeda koju reče: 'Tražit ćete me i nećete me naći; gdje sam ja, vi ne možete doći'?"
37Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, "Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
37U posljednji, veliki dan blagdana Isus stade i povika: "Ako je tko žedan, neka dođe k meni! Neka pije
38Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!"
38koji vjeruje u mene! Kao što reče Pismo: 'Rijeke će žive vode poteći iz njegove utrobe!'"
39(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
39To reče o Duhu kojega su imali primiti oni što vjeruju u njega. Tada doista ne bijaše još došao Duh jer Isus nije bio proslavljen.
40Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, "Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!"
40Kad su neki iz naroda čuli te riječi, govorahu: "Ovo je uistinu Prorok."
41Wengine wakasema, "Huyu ndiye Kristo!" Lakini wengine walisema, "Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
41Drugi govorahu: "Ovo je Krist." A bilo ih je i koji su pitali: "Pa zar Krist dolazi iz Galileje?
42Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!"
42Ne kaže li Pismo da Krist dolazi iz potomstva Davidova, i to iz Betlehema, mjesta gdje bijaše David?"
43Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
43Tako je u narodu nastala podvojenost zbog njega.
44Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
44Neki ga čak htjedoše uhvatiti, ali nitko ne stavi na nj ruke.
45Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, "Kwa nini hamkumleta?"
45Dođoše dakle stražari glavarima svećeničkim i farizejima, a ovi im rekoše: "Zašto ga ne dovedoste?"
46Walinzi wakawajibu, "Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!"
46Stražari odgovore: "Nikada nitko nije ovako govorio."
47Mafarisayo wakawauliza, "Je, nanyi pia mmedanganyika?
47Nato će im farizeji: "Zar ste se i vi dali zavesti?
48Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
48Je li itko od glavara ili farizeja povjerovao u njega?
49Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!"
49Ali ta svjetina koja ne pozna Zakona - to je prokleto!"
50Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
50Kaže im Nikodem - onaj koji ono prije dođe k Isusu, a bijaše jedan od njih:
51"Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?"
51"Zar naš Zakon sudi čovjeku ako ga prije ne sasluša i ne dozna što čini?"
52Nao wakamjibu, "Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!"
52Odgovoriše mu: "Da nisi i ti iz Galileje? Istraži pa ćeš vidjeti da iz Galileje ne ustaje prorok."
53Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;
53I otiđoše svaki svojoj kući.