1lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
1A Isus se uputi na Maslinsku goru.
2Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
2U zoru eto ga opet u Hramu. Sav je narod hrlio k njemu. On sjede i stade poučavati.
3Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
3Uto mu pismoznanci i farizeji dovedu neku ženu zatečenu u preljubu. Postave je u sredinu
4Kisha wakamwuliza Yesu, "Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
4i kažu mu: "Učitelju! Ova je žena zatečena u samom preljubu.
5Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?"
5U Zakonu nam je Mojsije naredio takve kamenovati. Što ti na to kažeš?"
6Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
6To govorahu samo da ga iskušaju pa da ga mogu optužiti. Isus se sagne pa stane prstom pisati po tlu.
7Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, "Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe."
7A kako su oni dalje navaljivali, on se uspravi i reče im: "Tko je od vas bez grijeha, neka prvi na nju baci kamen."
8Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
8I ponovno se sagnuvši, nastavi pisati po zemlji.
9Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
9A kad oni to čuše, stadoše odlaziti jedan za drugim, počevši od starijih. Osta Isus sam - i žena koja stajaše u sredini.
10Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, "Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?"
10Isus se uspravi i reče joj: "Ženo, gdje su oni? Zar te nitko ne osudi?"
11Huyo mwanamke akamjibu, "Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!" Naye Yesu akamwambia, "Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena."
11Ona reče: "Nitko, Gospodine." Reče joj Isus: "Ni ja te ne osuđujem. Idi i odsada više nemoj griješiti."
12Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, "Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima."
12Isus im zatim ponovno progovori: "Ja sam svjetlost svijeta; tko ide za mnom, neće hoditi u tami, nego će imati svjetlost života."
13Basi, Mafarisayo wakamwambia, "Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali."
13Farizeji mu nato rekoše: "Ti svjedočiš sam za sebe: svjedočanstvo tvoje nije istinito!"
14Yesu akawajibu, "Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
14Odgovori im Isus: "Ako ja i svjedočim sam za sebe, svjedočanstvo je moje istinito jer znam odakle dođoh i kamo idem. A vi ne znate ni odakle dolazim ni kamo idem.
15Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
15Vi sudite po tijelu; ja ne sudim nikoga;
16Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
16no ako i sudim, sud je moj istinit jer nisam sam, nego - ja i onaj koji me posla, Otac.
17Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
17Ta i u vašem zakonu piše da je svjedočanstvo dvojice istinito.
18Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia."
18Ja svjedočim za sebe, a svjedoči za mene i onaj koji me posla, Otac."
19Hapo wakamwuliza, "Baba yako yuko wapi?" Yesu akawajibu "Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia."
19Nato ga upitaju: "Gdje je tvoj Otac?" Odgovori Isus: "Niti mene poznajete niti Oca mojega. Kad biste poznavali mene, i Oca biste moga poznavali."
20Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
20Te riječi rekao je Isus u riznici dok je naučavao u Hramu. I nitko ga ne uhvati jer još ne bijaše došao njegov čas.
21Yesu akawaambia tena, "Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika."
21Reče im ponovno Isus: "Ja odlazim, a vi ćete me tražiti i u svojem ćete grijehu umrijeti. Kamo ja odlazim, vi ne možete doći."
22Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, "Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?"
22Židovi se nato stanu pitati: "Da se možda ne kani ubiti kad govori: 'Kamo ja odlazim, vi ne možete doći'?"
23Yesu akawaambia, "Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
23A Isus nastavi: "Vi ste odozdol, ja sam odozgor. Vi ste od ovoga svijeta, a ja nisam od ovoga svijeta.
24Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu."
24Stoga vam i rekoh: 'Umrijet ćete u grijesima svojim.' Uistinu, ako ne povjerujete da Ja jesam, umrijet ćete u grijesima svojim."
25Nao wakamwuliza, "Wewe ni nani?" Yesu akawajibu, "Nimewaambieni tangu mwanzo!
25Nato mu oni rekoše: "A tko si ti?" Odvrati Isus:
26Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake."
26"Ta što da vam s početka opet zborim? Mnogo toga imam o vama zboriti i suditi; no onaj koji me posla istinit je, i što sam čuo od njega, to ja zborim svijetu."
27Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
27Ne shvatiše da im govori o Ocu.
28Basi, Yesu akawaambia, "Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
28Isus im nato reče: "Kad uzdignete Sina Čovječjega, tada ćete upoznati da Ja jesam i da sam od sebe ne činim ništa, nego da onako zborim kako me naučio Otac.
29Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza."
29Onaj koji me posla sa mnom je i ne ostavi me sama jer ja uvijek činim što je njemu milo."
30Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
30Na te njegove riječi mnogi povjerovaše u njega.
31Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, "Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
31Tada Isus progovori Židovima koji mu povjerovaše: "Ako ostanete u mojoj riječi, uistinu, moji ste učenici;
32Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru."
32upoznat ćete istinu i istina će vas osloboditi."
33Nao wakamjibu, "Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?"
33Odgovore mu: "Potomstvo smo Abrahamovo i nikome nikada nismo robovali. Kako to ti govoriš: 'Postat ćete slobodni?'"
34Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
34Odgovori im Isus: "Zaista, zaista, kažem vam: tko god čini grijeh, rob je grijeha.
35Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu.
35Rob ne ostaje u kući zauvijek, a sin ostaje zauvijek.
36Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
36Ako vas dakle Sin oslobodi, zbilja ćete biti slobodni.
37Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
37Znam: potomstvo ste Abrahamovo, a ipak tražite da me ubijete jer moja riječ nema mjesta u vama.
38Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu."
38Ja govorim što vidjeh kod Oca, a vi činite što čuste od svog oca."
39Wao wakamjibu, "Baba yetu ni Abrahamu!" Yesu akawaambia, "Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
39Odgovoriše mu: "Naš je otac Abraham". Kaže im Isus: "Da ste djeca Abrahamova, djela biste Abrahamova činili.
40Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
40A eto, tražite da ubijete mene, mene koji sam vam govorio istinu što sam je od Boga čuo. Takvo što Abraham nije učinio!
41Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu." Wao wakamwambia, "Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu."
41Vi činite djela oca svojega." Rekoše mu: "Mi se nismo rodili iz preljuba, jedan nam je Otac - Bog."
42Yesu akawaambia, "Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
42Reče im Isus: "Kad bi Bog bio vaš Otac, ljubili biste mene jer sam ja od Boga izišao i došao; nisam sam od sebe došao, nego on me posla.
43Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
43Zašto moje besjede ne razumijete? Zato što niste kadri slušati moju riječ.
44Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
44Vama je otac đavao i hoće vam se vršiti prohtjeve oca svoga. On bijaše čovjekoubojica od početka i ne stajaše u istini jer nema istine u njemu: kad govori laž, od svojega govori jer je lažac i otac laži.
45Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
45A meni, jer istinu govorim, meni ne vjerujete.
46Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
46Tko će mi od vas dokazati grijeh? Ako istinu govorim, zašto mi ne vjerujete?
47Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu."
47Tko je od Boga, riječi Božje sluša; vi zato ne slušate jer niste od Boga."
48Wayahudi wakamwambia, "Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?"
48Odgovoriše mu Židovi: "Ne kažemo li pravo da si ti Samarijanac i da imaš zloduha?"
49Yesu akajibu, "Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
49Odgovori Isus: "Ja nemam zloduha, nego častim svoga Oca, a vi me obeščašćujete.
50Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
50No ja ne tražim svoje slave; ima tko traži i sudi.
51Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele."
51Zaista, zaista, kažem vam: ako tko očuva moju riječ, neće vidjeti smrti dovijeka."
52Basi, Wayahudi wakasema, "Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele!
52Rekoše mu Židovi: "Sada vidimo da imaš zloduha. Abraham umrije, tako i proroci, a ti kažeš: 'Ako tko čuva moju riječ, neće okusiti smrti dovijeka.'
53Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?"
53Zar si ti veći od oca našega Abrahama, koji je umro? Pa i proroci pomriješe. Kime se to praviš?"
54Yesu akawajibu, "Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
54Odgovori Isus: "Ako ja sam sebe slavim, slava moja nije ništa. Ima koji me slavi - Otac moj, a vi velite da je on vaš Bog,
55Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
55no ne poznajete ga, a ja ga znam. Ako vam reknem da ga ne znam, bit ću lažac jednak vama. No znam ga i riječ njegovu čuvam.
56Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi."
56Abraham, otac vaš, usklikta što će vidjeti moj Dan. I vidje i obradova se."
57Basi, Wayahudi wakamwambia, "Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?"
57Rekoše mu nato Židovi: "Ni pedeset ti još godina nije, a vidio si Abrahama?"
58Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko."
58Reče im Isus: "Zaista, zaista, kažem vam: prije negoli Abraham posta, Ja jesam!"
59Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.
59Nato pograbiše kamenje da bace na nj. No Isus se sakri te iziđe iz Hrama.