1Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
1Pogleda i vidje kako bogataši bacaju u riznicu svoje darove.
2akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
2A ugleda i neku ubogu udovicu kako baca onamo dva novčića.
3Basi, akasema, "Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
3I reče: "Uistinu, kažem vam: ova je sirota udovica ubacila više od sviju.
4Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."
4Svi su oni zapravo među darove ubacili od svog suviška, a ona je od svoje sirotinje ubacila sav žitak što ga imaše."
5Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
5I dok su neki razgovarali o Hramu, kako ga resi divno kamenje i zavjetni darovi, reče:
6"Haya yote mnayoyaona--zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
6"Doći će dani u kojima se od ovoga što motrite neće ostaviti ni kamen na kamenu nerazvaljen."
7Basi, wakamwuliza, "Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?"
7Upitaše ga: "Učitelju, a kada će to biti? I na koji se znak to ima dogoditi?"
8Yesu akawajibu, "Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
8A on reče: "Pazite, ne dajte se zavesti. Mnogi će doista doći u moje ime i govoriti: 'Ja sam' i: 'Vrijeme se približilo!' Ne idite za njima.
9Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado."
9A kad čujete za ratove i pobune, ne prestrašite se. Doista treba da se to prije dogodi, ali to još nije odmah svršetak."
10Halafu akaendelea kusema: "Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
10Tada im kaza: "Narod će ustati protiv naroda i kraljevstvo protiv kraljevstva.
11Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
11I bit će velikih potresa i po raznim mjestima gladi i pošasti; bit će strahota i velikih znakova s neba."
12Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
12"No prije svega toga podignut će na vas ruke i progoniti vas, predavati vas u sinagoge i tamnice. Vući će vas pred kraljeve i upravitelje zbog imena mojega.
13Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
13Zadesit će vas to radi svjedočenja."
14Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
14"Stoga uzmite k srcu: nemojte unaprijed smišljati obranu!
15kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
15Ta ja ću vam dati usta i mudrost kojoj se neće moći suprotstaviti niti oduprijeti nijedan vaš protivnik.
16Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
16A predavat će vas čak i vaši roditelji i braća, rođaci i prijatelji. Neke će od vas i ubiti."
17Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
17"Svi će vas zamrziti zbog imena mojega.
18Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
18Ali ni vlas vam s glave neće propasti.
19Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
19Svojom ćete se postojanošću spasiti."
20"Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
20"Kad ugledate da vojska opkoljuje Jeruzalem, tada znajte: približilo se njegovo opustošenje.
21Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
21Koji se tada zateknu u Judeji, neka bježe u gore; a koji u Gradu, neka ga napuste; koji pak po poljima, neka se u nj ne vraćaju
22Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
22jer to su dani odmazde, da se ispuni sve što je pisano."
23Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
23"Jao trudnicama i dojiljama u one dane jer bit će jad velik na zemlji i gnjev nad ovim narodom.
24Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
24Padat će od oštrice mača, odvodit će ih kao roblje po svim narodima. I Jeruzalem će gaziti pogani sve dok se ne navrše vremena pogana."
25"Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
25"I bit će znaci na suncu, mjesecu i zvijezdama, a na zemlji bezizlazna tjeskoba naroda zbog huke mora i valovlja.
26Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
26Izdisat će ljudi od straha i iščekivanja onoga što prijeti svijetu. Doista, sile će se nebeske poljuljati.
27Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
27Tada će ugledati Sina Čovječjega gdje dolazi u oblaku s velikom moći i slavom.
28Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia."
28Kad se sve to stane zbivati, uspravite se i podignite glave jer se približuje vaše otkupljenje."
29Kisha akawaambia mfano: "Angalieni mtini na miti mingine yote.
29I reče im prispodobu: "Pogledajte smokvu i sva stabla.
30Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
30Kad već propupaju, i sami vidite i znate: blizu je već ljeto.
31Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
31Tako i vi kad vidite da se to zbiva, znajte: blizu je kraljevstvo Božje.
32Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
32Zaista, kažem vam, ne, neće uminuti naraštaj ovaj dok se sve ne zbude.
33Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
33Nebo će i zemlja uminuti, ali moje riječi ne, neće uminuti."
34"Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
34"Pazite na se da vam srca ne otežaju u proždrljivosti, pijanstvu i u životnim brigama te vas iznenada ne zatekne onaj Dan
35Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
35jer će kao zamka nadoći na sve žitelje po svoj zemlji."
36Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu."
36"Stoga budni budite i u svako doba molite da uzmognete umaći svemu tomu što se ima zbiti i stati pred Sina Čovječjega."
37Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
37Danju je učio u Hramu, a noću bi izlazio i noćio na gori zvanoj Maslinska.
38Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.
38A sav bi narod rano hrlio k njemu u Hram da ga sluša.