1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
1Bližio se Blagdan beskvasnih kruhova zvan Pasha.
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
2Glavari svećenički i pismoznanci tražili su kako da Isusa smaknu jer se bojahu naroda.
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
3A Sotona uđe u Judu zvanog Iškariotski koji bijaše iz broja dvanaestorice.
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
4On ode i ugovori s glavarima svećeničkim i zapovjednicima kako da im ga preda.
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
5Oni se povesele i ugovore da će mu dati novca.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
6On pristade. Otada je tražio priliku da im ga preda mimo naroda.
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
7Kada dođe Dan beskvasnih kruhova, u koji je trebalo žrtvovati pashu,
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
8posla Isus Petra i Ivana i reče: "Hajdete, pripravite nam da blagujemo pashu."
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
9Rekoše mu: "Gdje hoćeš da pripravimo?"
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
10On im reče: "Evo, čim uđete u grad, namjerit ćete se na čovjeka koji nosi krčag vode. Pođite za njim u kuću u koju uniđe
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
11i recite domaćinu te kuće: 'Učitelj veli: Gdje je svratište u kojem bih blagovao pashu sa svojim učenicima?'
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
12I on će vam pokazati na katu veliko blagovalište prostrto: ondje pripravite."
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
13Oni odu, nađu kako im je rekao i priprave pashu.
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
14Kada dođe čas, sjede Isus za stol i apostoli s njim.
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
15I reče im: "Svom sam dušom čeznuo ovu pashu blagovati s vama prije svoje muke.
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
16Jer kažem vam, neću je više blagovati dok se ona ne završi u kraljevstvu Božjem."
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
17I uze čašu, zahvali i reče: "Uzmite je i razdijelite među sobom.
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
18Jer kažem vam, ne, neću više piti od roda trsova dok kraljevstvo Božje ne dođe."
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
19I uze kruh, zahvali, razlomi i dade im govoreći: "Ovo je tijelo moje koje se za vas predaje. Ovo činite meni na spomen."
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
20Tako i čašu, pošto večeraše, govoreći: "Ova čaša novi je Savez u mojoj krvi koja se za vas prolijeva."
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
21"A evo, ruka mog izdajice sa mnom je na stolu.
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
22Sin Čovječji, istina, ide kako je određeno, ali jao čovjeku onomu koji ga predaje."
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
23I oni se počeše ispitivati tko bi od njih mogao takvo što učiniti.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
24Uto nasta među njima prepirka tko bi od njih bio najveći.
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
25A on im reče: "Kraljevi gospoduju svojim narodima i vlastodršci nazivaju sebe dobrotvorima.
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
26Vi nemojte tako! Naprotiv, najveći među vama neka bude kao najmlađi; i predstojnik kao poslužitelj.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
27Ta tko je veći? Koji je za stolom ili koji poslužuje? Zar ne onaj koji je za stolom? A ja sam posred vas kao onaj koji poslužuje."
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
28"Da, vi ste sa mnom ustrajali u mojim kušnjama.
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
29Ja vam stoga u baštinu predajem kraljevstvo što ga je meni predao moj Otac:
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
30da jedete i pijete za mojim stolom u kraljevstvu mojemu i sjedite na prijestoljima sudeći dvanaest plemena Izraelovih."
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
31"Šimune, Šimune, evo Sotona zaiska da vas prorešeta kao pšenicu.
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
32Ali ja sam molio za tebe da ne malakše tvoja vjera. Pa kad k sebi dođeš, učvrsti svoju braću."
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
33Petar mu reče: "Gospodine, s tobom sam spreman i u tamnicu i u smrt."
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
34A Isus će mu: "Kažem ti, Petre, neće se danas oglasiti pijetao dok triput ne zatajiš da me poznaš."
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
35I reče: "Kad sam vas poslao bez kese i bez torbe i bez sandala, je li vam što nedostajalo?" Oni odgovore: "Ništa."
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
36Nato će im: "No sada tko ima kesu, neka je uzme! Isto tako i torbu! A koji nema, neka proda svoju haljinu i neka kupi sebi mač
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
37jer kažem vam, ono što je napisano treba se ispuniti na meni: Među zlikovce bi ubrojen. Uistinu, sve što se odnosi na mene ispunja se."
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
38Oni mu rekoše: "Gospodine, evo ovdje dva mača!" Reče im: "Dosta je!"
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
39Tada iziđe te se po običaju zaputi na Maslinsku goru. Za njim pođoše i njegovi učenici.
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
40Kada dođe onamo, reče im: "Molite da ne padnete u napast!"
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
41I otrgnu se od njih koliko bi se kamenom dobacilo, pade na koljena pa se molio:
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
42"Oče! Ako hoćeš, otkloni ovu čašu od mene. Ali ne moja volja, nego tvoja neka bude!"
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
43A ukaza mu se anđeo s neba koji ga ohrabri. A kad je bio u smrtnoj muci, usrdnije se molio.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
44I bijaše znoj njegov kao kaplje krvi koje su padale na zemlju.
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
45Usta od molitve, dođe učenicima i nađe ih snene od žalosti
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
46pa im reče: "Što spavate? Ustanite! Molite da ne padnete u napast!"
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
47Dok je on još govorio, eto svjetine, a pred njom jedan od dvanaestorice, zvani Juda. On se približi Isusu da ga poljubi.
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
48Isus mu reče: "Juda, poljupcem Sina Čovječjeg predaješ?"
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
49A oni oko njega, vidjevši što se zbiva, rekoše: "Gospodine, da udarimo mačem?"
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
50I jedan od njih udari slugu velikoga svećenika i odsiječe mu desno uho.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
51Isus odgovori: "Pustite! Dosta!" Onda se dotače uha i zacijeli ga.
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
52Nato Isus reče onima koji se digoše na nj, glavarima svećeničkim, zapovjednicima hramskim i starješinama: "Kao na razbojnika iziđoste s mačevima i toljagama!
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
53Danomice bijah s vama u Hramu i ne digoste ruke na me. No ovo je vaš čas i vlast Tmina."
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
54Uhvatiše ga dakle, odvedoše i uvedoše u dom velikoga svećenika. Petar je išao za njim izdaleka.
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
55A posred dvorišta naložiše vatru i posjedaše uokolo. Među njih sjedne Petar.
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
56Ugleda ga neka sluškinja gdje sjedi kraj vatre, oštro ga pogleda i reče: "I ovaj bijaše s njim!"
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
57A on zanijeka: "Ne znam ga, ženo!"
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
58Malo zatim opazi ga netko drugi i reče: "I ti si od njih!" A Petar reče: "Čovječe, nisam!"
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
59I nakon otprilike jedne ure drugi neki navaljivaše: "Doista, i ovaj bijaše s njim! Ta Galilejac je!"
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
60A Petar će: "Čovječe, ne znam što govoriš!" I umah, dok je on još govorio, oglasi se pijetao.
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
61Gospodin se obazre i upre pogled u Petra, a Petar se spomenu riječi Gospodinove, kako mu ono reče: "Prije nego se danas pijetao oglasi, zatajit ćeš me tri puta."
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
62I iziđe te gorko zaplaka.
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
63A ljudi koji su Isusa čuvali udarajući ga poigravali se njime
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
64i zastirući mu lice, zapitkivali ga: "Proreci tko te udario!"
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
65I mnogim se drugim pogrdama nabacivali na nj.
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
66A kad se razdanilo, sabra se starješinstvo narodno, glavari svećenički i pismoznanci te ga dovedoše pred svoje Vijeće
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
67i rekoše: "Ako si ti Krist, reci nam!" A on će im: "Ako vam reknem, nećete vjerovati;
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
68ako vas zapitam, nećete odgovoriti.
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
69No od sada će Sin Čovječji sjedjeti zdesna Sile Božje."
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
70Nato svi rekoše: "Ti si, dakle, Sin Božji!" On im reče: "Vi velite! Ja jesam!"
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."
71Nato će oni: "Što nam još svjedočanstvo treba? Ta sami smo čuli iz njegovih usta!"