Swahili: New Testament

Croatian

Luke

23

1Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
1I ustade sva ona svjetina. Odvedoše ga Pilatu
2Wakaanza kumshtaki wakisema: "Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme."
2i stadoše ga optuživati: "Ovoga nađosmo kako zavodi naš narod i brani davati caru porez te za sebe tvrdi da je Krist, kralj."
3Pilato akamwuliza Yesu, "Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
3Pilat ga upita: "Ti li si kralj židovski?" On mu odgovori: "Ti kažeš!"
4Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, "Sioni kosa lolote katika mtu huyu."
4Tada Pilat reče glavarima svećeničkim i svjetini: "Nikakve krivnje ne nalazim na ovom čovjeku!"
5Lakini wao wakasisitiza wakisema: "Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa."
5No oni navaljivahu: "Buni narod naučavajući po svoj Judeji, počevši od Galileje pa dovde!"
6Pilato aliposikia hayo, akauliza, "Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?"
6Čuvši to, Pilat propita da li je taj čovjek Galilejac.
7Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
7Saznavši da je iz oblasti Herodove, posla ga Herodu, koji i sam bijaše onih dana u Jeruzalemu.
8Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
8A kad Herod ugleda Isusa, veoma se obradova jer ga je već odavna želo vidjeti zbog onoga što je o njemu slušao te se nadao od njega vidjeti koje čudo.
9Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
9Postavljao mu je mnoga pitanja, ali mu Isus uopće nije odgovarao.
10Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
10A stajahu ondje i glavari svećenički i pismoznanci optužujući ga žestoko.
11Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
11Herod ga zajedno sa svojom vojskom prezre i ismija: obuče ga u bijelu haljinu i posla natrag Pilatu.
12Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
12Onoga se dana Herod i Pilat sprijateljiše, jer prije bijahu neprijatelji.
13Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
13A Pilat dade sazvati glavare svećeničke, vijećnike i narod
14akawaambia, "Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
14te im reče: "Doveli ste mi ovoga čovjeka kao da buni narod. Ja ga evo ispitah pred vama pa ne nađoh na njemu ni jedne krivice za koju ga optužujete.
15Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
15A ni Herod jer ga posla natrag nama. Evo, on nije počinio ništa čime bi zaslužio smrt.
16Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia."
16Kaznit ću ga dakle i pustiti."
17Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
17#
18Lakini wote wakapiga kelele pamoja: "Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!"
18I povikaše svi uglas: "Smakni ovoga, a pusti nam Barabu!"
19(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
19A taj bijaše bačen u tamnicu zbog neke pobune u gradu i ubojstva.
20Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
20Pilat im stoga ponovno progovori hoteći osloboditi Isusa.
21lakini wao wakapiga kelele: "Msulubishe, msulubishe!"
21Ali oni vikahu: "Raspni, raspni ga!"
22Pilato akawaambia mara ya tatu, "Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie."
22On im treći put reče: "Ta što je on zla učinio? Ne nađoh na njemu smrtne krivice. Kaznit ću ga dakle i pustiti."
23Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
23Ali oni navaljivahu iza glasa ištući da se razapne. I vika im bivala sve jača.
24Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
24Pilat presudi da im bude što ištu.
25Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
25Pusti onoga koji zbog pobune i ubojstva bijaše bačen u tamnicu, koga su iskali, a Isusa preda njima na volju.
26Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
26Kad ga odvedoše, uhvatiše nekog Šimuna Cirenca koji je dolazio s polja i stave na nj križ da ga nosi za Isusom.
27Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
27Za njim je išlo silno mnoštvo svijeta, napose žena, koje su plakale i naricale za njim.
28Yesu akawageukia, akasema, "Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
28Isus se okrenu prema njima pa im reče: "Kćeri Jeruzalemske, ne plačite nada mnom, nego plačite nad sobom i nad djecom svojom.
29Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
29Jer evo idu dani kad će se govoriti: 'Blago nerotkinjama, utrobama koje ne rodiše i sisama koje ne dojiše.'
30Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
30Tad će početi govoriti gorama: 'Padnite na nas!' i bregovima: 'Pokrijte nas!'
31Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?"
31Jer ako se tako postupa sa zelenim stablom, što li će biti sa suhim?"
32Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
32A vodili su i drugu dvojicu, zločince, da ih s njime pogube.
33Walipofika mahali paitwapo, "Fuvu la Kichwa," ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
33I kada dođoše na mjesto zvano Lubanja, ondje razapeše njega i te zločince, jednoga zdesna, drugoga slijeva.
34Yesu akasema, "Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya." Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
34A Isus je govorio: "Oče, oprosti im, ne znaju što čine!" I razdijeliše među se haljine njegove bacivši kocke.
35Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: "Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!"
35Stajao je ondje narod i promatrao. A podrugivali se i glavari govoreći: "Druge je spasio, neka spasi sam sebe ako je on Krist Božji, Izabranik!"
36Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
36Izrugivali ga i vojnici, prilazili mu i nudili ga octom
37wakisema: "Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe."
37govoreći: "Ako si ti kralj židovski, spasi sam sebe!"
38Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: "Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi."
38A bijaše i natpis ponad njega: "Ovo je kralj židovski."
39Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: "Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia."
39Jedan ga je od obješenih zločinaca pogrđivao: "Nisi li ti Krist? Spasi sebe i nas!"
40Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: "Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
40A drugi ovoga prekoravaše: "Zar se ne bojiš Boga ni ti, koji si pod istom osudom?
41Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya."
41Ali mi po pravdi jer primamo što smo djelima zaslužili, a on - on ništa opako ne učini."
42Kisha akasema, "Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako."
42Onda reče: "Isuse, sjeti me se kada dođeš u kraljevstvo svoje."
43Yesu akamwambia, "Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi."
43A on će mu: "Zaista ti kažem: danas ćeš biti sa mnom u raju!"
44Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
44Bijaše već oko šeste ure kad nasta tama po svoj zemlji - sve do ure devete,
45na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
45jer sunce pomrča, a hramska se zavjesa razdrije po sredini.
46Yesu akalia kwa sauti kubwa: "Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako." Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
46I povika Isus iza glasa: "Oče, u ruke tvoje predajem duh svoj!" To rekavši, izdahnu.
47Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: "Hakika huyu alikuwa mtu mwema."
47Kad satnik vidje što se zbiva, stane slaviti Boga: "Zbilja, čovjek ovaj bijaše pravednik!"
48Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
48I kad je sav svijet koji se zgrnuo na taj prizor vidio što se zbiva, vraćao se bijući se u prsa.
49Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
49Stajahu podalje i gledahu to svi znanci njegovi i žene koje su za njim išle iz Galileje.
50Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
50I dođe čovjek imenom Josip, vijećnik, čovjek čestit i pravedan;
51Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
51on ne privoli njihovoj odluci i postupku. Bijaše iz Arimateje, grada judejskoga i iščekivaše kraljevstvo Božje.
52Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
52Taj dakle pristupi Pilatu i zaiska tijelo Isusovo.
53Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
53Zatim ga skinu, povi u platno i položi u grob isklesan u koji još ne bijaše nitko položen.
54Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
54Bijaše dan Priprave; subota je svitala.
55Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
55A pratile to žene koje su s Isusom došle iz Galileje: motrile grob i kako je položeno tijelo njegovo.
56Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.
56Zatim se vrate i priprave miomirise i pomasti. U subotu mirovahu po propisu.