Swahili: New Testament

Croatian

Luke

3

1Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
1Petnaeste godine vladanja cara Tiberija, dok je upravitelj Judeje bio Poncije Pilat, tetrarh Galileje Herod, a njegov brat Filip tetrarh Itureje i zemlje trahonitidske, i Lizanije tetrarh Abilene,
2na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
2za velikog svećenika Ane i Kajfe, dođe riječ Božja Ivanu, sinu Zaharijinu, u pustinji.
3Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
3On obiđe svu okolicu jordansku propovijedajući obraćeničko krštenje na otpuštenje grijeha
4Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
4kao što je pisano u Knjizi besjeda Izaije proroka: Glas viče u pustinji: Pripravite put Gospodinu, poravnite mu staze!
5Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
5Svaka dolina neka se ispuni, svaka gora i brežuljak neka se slegne! Što je krivudavo, neka se izravna, a hrapavi putovi neka se izglade!
6Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."
6I svako će tijelo vidjeti spasenje Božje.
7Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
7Govoraše dakle mnoštvu koje je dolazilo da se krsti: "Leglo gujinje! Tko vas samo upozori da bježite od skore srdžbe?
8Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
8Donosite dakle plodove dostojne obraćenja. I nemojte početi u sebi govoriti: 'Imamo oca Abrahama!' Jer, kažem vam: Bog iz ovog kamenja može podići djecu Abrahamovu.
9Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni."
9Već je sjekira položena na korijen stablima: svako dakle stablo koje ne donosi dobra roda siječe se i u oganj baca."
10Umati wa watu ukamwuliza, "Tufanye nini basi?"
10Pitalo ga mnoštvo: "Što nam je dakle činiti?"
11Akawajibu, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."
11On im odgovaraše: "Tko ima dvije haljine, neka podijeli s onim koji nema. U koga ima hrane, neka učini isto tako."
12Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, "Mwalimu, tufanye nini?"
12Dođoše krstiti se i carinici pa ga pitahu: "Učitelju, što nam je činiti?"
13Naye akawaambia, "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."
13Reče im: "Ne utjerujte više nego što vam je određeno."
14Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?" Naye akawajibu, "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."
14Pitahu ga i vojnici: "A nama, što je nama činiti?" I reče im: "Nikome ne činite nasilja, nikoga krivo ne prijavljujte i budite zadovoljni svojom plaćom."
15Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
15Narod bijaše u iščekivanju i svi se u srcu pitahu o Ivanu nije li on možda Krist.
16Hapo Yohane akawaambia wote, "Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
16Zato im Ivan svima reče: "Ja vas, istina, vodom krstim. Ali dolazi jači od mene. Ja nisam dostojan odriješiti mu remenje na obući. On će vas krstiti Duhom Svetim i ognjem.
17Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika."
17U ruci mu vijača da pročisti gumno svoje i sabere žito u žitnicu svoju, a pljevu će spaliti ognjem neugasivim."
18Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
18I mnogim je drugim pobudama Ivan narodu navješćivao evanđelje.
19Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
19A Heroda je tetrarha Ivan prekorio zbog Herodijade, žene njegova brata i zbog svih njegovih zlodjela.
20Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
20Svemu tome nadoda Herod još i ovo: zatvori Ivana u tamnicu.
21Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
21Kad se krstio sav narod, krstio se i Isus. I dok se molio, rastvori se nebo,
22na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
22siđe na nj Duh Sveti u tjelesnom obličju, poput goluba, a glas se s neba zaori: "Ti si Sin moj, Ljubljeni! U tebi mi sva milina!"
23Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
23Kad je Isus nastupio, bilo mu je oko trideset godina. Bijaše - kako se smatralo - sin Josipov, Elijev,
24Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
24Matatov, Levijev, Malkijev, Janajev, Josipov.
25mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
25Matatijin, Amosov, Naumov, Heslijev, Nagajev,
26mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
26Mahatov, Matatijin, Šimijev, Josehov, Jodin,
27mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
27Johananov, Resin, Zerubabelov, Šealtielov, Nerijev,
28mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
28Malkijev, Adijev, Kosamov, Elmadamov, Erov,
29mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
29Jošuin, Eliezerov, Jorimov, Matatov, Levijev,
30mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
30Šimunov, Judin, Josipov, Jonamov, Elijakimov,
31mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
31Melejin, Menin, Matatin, Natanov, Davidov,
32mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
32Jišajev, Obedov, Boazov, Salin, Nahšonov,
33mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
33Aminadabov, Adminov, Arnijev, Hesronov, Peresov, Judin,
34mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
34Jakovljev, Izakov, Abrahamov, Terahov, Nahorov,
35mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
35Serugov, Reuov, Pelegov, Eberov, Šelahov,
36mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
36Kenanov, Arpakšadov, Šemov, Noin, Lamekov,
37mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
37Metušalahov, Henokov, Jeredov, Mahalalelov, Kenanov,
38mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
38Enošev, Šetov, Adamov, Božji.