1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
1Isus se, pun Duha Svetoga, vratio s Jordana i Duh ga četrdeset dana vodio pustinjom,
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
2gdje ga je iskušavao đavao. Tih dana nije ništa jeo, te kad oni istekoše, ogladnje.
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
3A đavao mu reče: "Ako si Sin Božji, reci ovom kamenu da postane kruhom."
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
4Isus mu odgovori: "Pisano je: Ne živi čovjek samo o kruhu."
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
5I povede ga đavao na visoko, pokaza mu odjednom sva kraljevstva zemlje
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
6i reče mu: "Tebi ću dati svu ovu vlast i slavu njihovu jer meni je dana i komu hoću, dajem je.
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
7Ako se dakle pokloniš preda mnom, sve je tvoje."
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
8Isus mu odgovori: "Pisano je: Klanjaj se Gospodinu, Bogu svomu, i njemu jedinomu služi!"
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
9Povede ga u Jeruzalem i postavi na vrh Hrama i reče mu: "Ako si Sin Božji, baci se odavde dolje!
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
10Ta pisamo je: Anđelima će svojim zapovjediti za tebe da te čuvaju.
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
11I: Na rukama će te nositi da se gdje nogom ne spotakneš o kamen."
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
12Odgovori mu Isus: "Rečeno je: Ne iskušavaj Gospodina, Boga svojega!"
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
13Pošto iscrpi sve kušnje, đavao se udalji od njega do druge prilike.
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
14A Isus se u snazi Duha vrati u Galileju te glas o njemu puče po svoj okolici.
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
15I slavljen od sviju, naučavaše po njihovim sinagogama.
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
16I dođe u Nazaret, gdje bijaše othranjen. I uđe po svom običaju na dan subotni u sinagogu te ustane čitati.
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
17Pruže mu Knjigu proroka Izaije. On razvije knjigu i nađe mjesto gdje stoji napisano:
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
18Duh Gospodnji na meni je jer me pomaza! On me posla blagovjesnikom biti siromasima, proglasiti sužnjima oslobođenje, vid slijepima, na slobodu pustiti potlačene,
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
19proglasiti godinu milosti Gospodnje.
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
20Tada savi knjigu, vrati je poslužitelju i sjede. Oči sviju u sinagogi bijahu uprte u njega.
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
21On im progovori: "Danas se ispunilo ovo Pismo što vam još odzvanja u ušima."
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
22I svi su mu povlađivali i divili se milini riječi koje su tekle iz njegovih usta. Govorahu: "Nije li ovo sin Josipov?"
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
23A on im reče: "Zacijelo ćete mi reći onu prispodobu: Liječniče, izliječi sam sebe! Što smo čuli da se dogodilo u Kafarnaumu, učini i ovdje, u svom zavičaju."
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
24I nastavi: "Zaista, kažem vam, nijedan prorok nije dobro došao u svom zavičaju.
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
25Uistinu, kažem vam, mnogo bijaše udovica u Izraelu u dane Ilijine kad se na tri godine i šest mjeseci zatvorilo nebo pa zavladala velika glad po svoj zemlji.
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
26I ni k jednoj od njih nije bio poslan Ilija doli k ženi udovici u Sarfati sidonskoj.
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
27I mnogo bijaše gubavaca u Izraelu za proroka Elizeja. I nijedan se od njih ne očisti doli Naaman Sirac."
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
28Čuvši to, svi se u sinagogi napune gnjevom,
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
29ustanu, izbace ga iz grada i odvedu na rub brijega na kojem je sagrađen njihov grad da ga strmoglave.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
30No on prođe između njih i ode.
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
31I siđe u Kafarnaum, grad galilejski. I poučavaše ih subotom
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
32te bijahu zaneseni njegovim naukom jer silna bijaše riječ njegova.
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
33A zatekao se u sinagogi čovjek s duhom nečistoga đavla. On povika u sav glas:
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
34"Hej, što ti imaš s nama, Isuse Nazarećanine? Došao si da nas uništiš! Znam ja tko si ti: Svetac Božji."
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
35Isus mu zaprijeti: "Umukni i iziđi iz njega!" Nato đavao čovjeka obori u sredinu te iziđe iz njega ne naudiv mu ništa.
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
36I nasta opće zaprepaštenje te se među sobom razgovarahu: "Kakve li riječi! S vlašću i snagom zapovijeda nečistim dusima te izlaze!"
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
37I glas se o njemu širio po svim okolnim mjestima.
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
38Ustavši iz sinagoge, uđe u kuću Šimunovu. A Šimunovu je punicu mučila velika ognjica. I zamole ga za nju.
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
39On se nadvi nad nju, zaprijeti ognjici i ona je pusti. I odmah ustade i posluživaše im.
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
40O zalazu sunca svi koji su imali bolesnike od raznih bolesti dovedoše ih k njemu. A on bi na svakoga od njih stavljao ruke i ozdravljao ih.
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
41A iz mnogih su izlazili i zlodusi vičući: "Ti si Sin Božji!" On im se prijetio i nije im dao govoriti jer su znali da je on Krist.
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
42Kad osvanu dan, iziđe i pođe na samotno mjesto. I mnoštvo ga tražilo. Dođoše k njemu i zadržavahu ga da ne ode od njih.
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
43A on im reče: "I drugim gradovima treba da navješćujem evanđelje o kraljevstvu Božjem. Jer za to sam poslan."
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.
44I naučavaše po sinagogama judejskim.