1Yesu alipokuwa anatoka Hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake alimwambia, "Mwalimu, tazama jinsi mawe haya na majengo haya yalivyo ya ajabu!"
1Kad je izlazio iz Hrama, rekne mu jedan od njegovih učenika: "Učitelju, gledaj! Kakva li kamenja, kakvih li zdanja!"
2Yesu akamwambia, "Je, unayaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitabomolewa."
2Isus mu odvrati: "Vidiš li ta veličanstvena zdanja? Ne, neće se ostaviti ni kamen na kamenu nerazvaljen."
3Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni akielekea Hekalu, Petro, Yakobo, Yohane na Andrea wakamwuliza kwa faragha,
3Dok je zatim na Maslinskoj gori sjedio sučelice Hramu, upitaju ga nasamo Petar, Jakov, Ivan i Andrija:
4"Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kwamba mambo haya karibu yatimizwe?"
4"Reci nam kada će to biti i na koji se znak sve to ima svršiti?"
5Yesu akaanza kuwaambia, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
5Tada im Isus poče govoriti: "Pazite da vas tko ne zavede.
6Maana wengi watakuja wakilitumia jina langu, wakisema, Mimi ndiye! nao watawapotosha watu wengi.
6Mnogi će doći u moje ime i govoriti: Ja sam! I mnoge će zavesti.
7Mtakaposikia juu ya vita na fununu za vita, msifadhaike. Mambo hayo lazima yatokee, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
7Kada pak čujete za ratove i za glasove o ratovima, ne uznemirujte se. Treba da se to dogodi, ali to još nije svršetak."
8Taifa moja litapigana na taifa lingine; utawala mmoja utapigana na utawala mwingine; kila mahali kutakuwa na mitetemeko ya ardhi na njaa. Mambo haya ni kama tu maumivu ya kwanza ya kujifungua mtoto.
8"Narod će ustati protiv naroda, kraljevstvo protiv kraljevstva. Bit će potresa po raznim mjestima, bit će gladi. To je početak trudova."
9"Lakini ninyi jihadharini. Maana watu watawapelekeni mahakamani, na kuwapigeni katika masunagogi. Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu ili mpate kunishuhudia kwao.
9"Vi pak pazite sami na sebe. Predavat će vas vijećima i tući vas u sinagogama, pred upraviteljima i kraljevima stajat ćete zbog mene, njima za svjedočanstvo.
10Lakini lazima kwanza Habari Njema ihubiriwe kwa mataifa yote.
10A treba da se najprije svim narodima propovijeda evanđelje."
11Nao watakapowatieni nguvuni na kuwapeleka mahakamani, msiwe na wasiwasi juu ya yale mtakayosema; saa ile itakapofika, semeni chochote mtakachopewa, maana si ninyi mtakaosema, bali Roho Mtakatifu.
11"Kad vas budu vodili na izručenje, ne brinite se unaprijed što ćete govoriti, nego govorite što vam bude dano u onaj čas. Ta niste vi koji govorite, nego Duh Sveti.
12Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanae; watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.
12Predavat će na smrt brat brata i otac sina. Djeca će ustajati na roditelje i ubijati ih.
13Watu wote watawachukieni ninyi kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.
13Svi će vas zamrziti zbog imena moga. Ali tko ustraje do svršetka, bit će spašen."
14"Mtakapoona Chukizo Haribifu limesimama mahali ambapo si pake, (msomaji na atambue maana yake!) Hapo watu walioko Yudea wakimbilie milimani.
14"I kad vidite da grozota pustoši stoluje gdje joj nije mjesto - tko čita, neka razumije - koji se tada zateknu u Judeji, neka bježe u gore!
15Mtu aliye juu ya paa la nyumba asishuke kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu.
15Tko bude na krovu, neka ne silazi i ne ulazi u kuću da iz nje što uzme.
16Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
16I tko bude u polju, neka se ne okreće natrag da uzme ogrtač!"
17Ole wao waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
17"Jao trudnicama i dojiljama u one dane!
18Ombeni ili mambo hayo yasitukie nyakati za baridi.
18A molite da to ne bude zimi
19Maana wakati huo kutakuwa na dhiki ambayo haijatokea tangu Mungu alipoumba ulimwengu mpaka leo, wala haitatokea tena.
19jer će onih dana biti tjeskoba kakve ne bi od početka stvorenja, koje stvori Bog, sve do sada, a neće je ni biti.
20Kama Bwana asingepunguza siku hizo, hakuna binadamu ambaye angeokolewa. Lakini kwa ajili ya wateule wake, Bwana amezipunguza siku hizo.
20I kad Gospodin ne bi skratio dane one, nitko se ne bi spasio. No poradi izabranih, koje on sebi izabra, skratio je on te dane."
21"Basi mtu akiwaambieni, Tazama, Kristo yupo hapa! au Yupo pale! msimsadiki.
21Ako vam tada tko rekne: 'Evo Krista ovdje! Eno ondje!' - ne vjerujte.
22Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo, watafanya ishara na maajabu, ili kuwapotosha wateule wa Mungu, kama ikiwezekana.
22Ustat će doista lažni kristi i lažni proroci i tvorit će znamenja i čudesa da, bude li moguće, zavedu izabrane.
23Lakini ninyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.
23Vi dakle budite na oprezu! Evo, prorekao sam vam sve!"
24"Basi, siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza na mwezi hautaangaza.
24Nego, u one dane, nakon one nevolje, sunce će pomrčati i mjesec neće više svijetljeti
25Nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
25a zvijezde će s neba padati i sile će se nebeske poljuljati.
26Hapo watamwona Mwana wa Mtu akija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utukufu.
26Tada će ugledati Sina Čovječjega gdje dolazi na oblacima s velikom moći i slavom.
27Kisha atawatuma malaika wake; atawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
27I razaslat će anđele i sabrati svoje izabranike s četiri vjetra, s kraja zemlje do na kraj neba."
28"Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
28A od smokve se naučite prispodobi! Kad joj grana već omekša i lišće potjera, znate: ljeto je blizu.
29Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo hayo yakitendeka, jueni kwamba Mwana wa Mtu yuko karibu sana.
29Tako i vi kad vidite da se to zbiva, znajte: blizu je, na vratima!
30Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
30Zaista, kažem vam, ne, neće uminuti naraštaj ovaj dok se sve to ne zbude.
31Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
31Nebo će i zemlja uminuti, ali riječi moje ne, neće uminuti."
32"Lakini hakuna mtu ajuaye siku au saa hiyo itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye.
32"A o onom danu i času nitko ne zna, pa ni anđeli na nebu, ni Sin, nego samo Otac."
33Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.
33"Pazite! Bdijte jer ne znate kada je čas.
34Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia mlinzi wa mlango awe macho.
34Kao kad ono čovjek neki polazeći na put ostavi svoju kuću, upravu povjeri slugama, svakomu svoj posao, a vrataru zapovjedi da bdije.
35Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.
35Bdijte, dakle, jer ne znate kad će se domaćin vratiti - da li uvečer ili o ponoći, da li za prvih pijetlova ili ujutro -
36Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.
36da vas ne bi našao pozaspale ako iznenada dođe."
37Ninayowaambieni ninyi, nawaambia wote: Kesheni!"
37"Što vama kažem, svima kažem: Bdijte!"