Swahili: New Testament

Croatian

Mark

5

1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
1Stigoše na onu stranu mora, u kraj gerazenski.
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
2Čim iziđe iz lađe, odmah mu iz grobnica pohiti u susret neki čovjek s nečistim duhom.
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
3Obitavalište je imao u grobnicama. I nitko ga više nije mogao svezati ni lancima
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
4jer je već često bio i okovima i lancima svezan, ali je raskinuo okove i iskidao lance i nitko ga nije mogao ukrotiti.
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
5Po cijele bi noći i dane u grobnicama i po brdima vikao i bio se kamenjem.
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
6Kad izdaleka opazi Isusa, dotrči i pokloni mu se,
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
7a onda u sav glas povika: "Što ti imaš sa mnom, Isuse, Sine Boga Svevišnjega? Zaklinjem te Bogom, ne muči me!"
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
8Jer Isus mu bijaše rekao: "Iziđi, duše nečisti, iz ovoga čovjeka!"
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
9Isus ga nato upita: "Kako ti je ime?" Kaže mu: "Legija mi je ime! Ima nas mnogo!"
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
10I uporno zaklinjaše Isusa da ih ne istjera iz onoga kraja.
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
11A ondje je pod brdom paslo veliko krdo svinja.
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
12Zaklinjahu ga dakle: "Pošalji nas u ove svinje da u njih uđemo!"
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
13I on im dopusti. Tada iziđoše nečisti duhovi i uđoše u svinje. I krdo od oko dvije tisuće jurnu niz obronak u more i podavi se u moru.
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
14Svinjari pobjegoše i razglasiše gradom i selima. A ljudi pođoše vidjeti što se dogodilo.
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
15Dođu Isusu. Ugledaju opsjednutoga: sjedio je obučen i zdrave pameti - on koji ih je imao legiju. I prestraše se.
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
16A očevici im razlagahu kako je to bilo s opsjednutim i ono o svinjama.
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
17Tada ga stanu moliti da ode iz njihova kraja.
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
18Kad je ulazio u lađu, onaj što bijaše opsjednut molio ga da bude uza nj.
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
19No on mu ne dopusti, nego mu reče: "Pođi kući k svojima pa im javi što ti je učinio Gospodin, kako ti se smilovao."
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
20On ode i poče razglašavati po Dekapolu što mu učini Isus. I svi su se divili.
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
21Kad se Isus lađom ponovno prebacio prijeko, zgrnu se k njemu silan svijet.
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
22Stajao je uz more. I dođe, gle, jedan od nadstojnika sinagoge, imenom Jair. Ugledavši ga, padne mu pred noge
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
23pa ga usrdno moljaše: "Kćerkica mi je na umoru! Dođi, stavi ruke na nju da ozdravi i ostane u životu!"
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
24I pođe s njima. A za njim je išao silan svijet i pritiskao ga.
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
25A neka je žena dvanaest godina bolovala od krvarenja,
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
26mnogo pretrpjela od pustih liječnika, razdala sve svoje i ništa nije koristilo; štoviše, bivalo joj je sve gore.
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
27Čuvši za Isusa, priđe mu među mnoštvom odostraga i dotaknu se njegove haljine.
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
28Mislila je: "Dotaknem li se samo njegovih haljina, bit ću spašena."
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
29I odmah prestane njezino krvarenje te osjeti u tijelu da je ozdravila od zla.
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
30Isus odmah u sebi osjeti da je iz njega izišla sila pa se okrenu usred mnoštva i reče: "Tko se to dotaknu mojih haljina?"
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
31A učenici mu rekoše: "Ta vidiš kako te mnoštvo odasvud pritišće i još pitaš: 'Tko me se to dotaknu?'"
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
32A on zaokruži pogledom da vidi onu koja to učini.
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
33Žena, sva u strahu i trepetu, svjesna onoga što joj se dogodilo, pristupi i baci se preda nj pa mu kaza sve po istini.
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
34On joj reče: "Kćeri, vjera te tvoja spasila! Pođi u miru i budi zdrava od svojega zla!"
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
35Dok je Isus još govorio, eto nadstojnikovih s porukom. "Kći ti je umrla. Čemu dalje mučiti učitelja?"
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
36Isus je čuo taj razgovor, pa će nadstojniku: "Ne boj se! Samo vjeruj!"
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
37I ne dopusti da ga itko drugi prati osim Petra i Jakova i Ivana, brata Jakovljeva.
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
38I dođu u kuću nadstojnikovu. Ugleda buku i one koji plakahu i naricahu u sav glas.
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
39Uđe i kaže im: "Što bučite i plačete? Dijete nije umrlo, nego spava."
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
40A oni mu se podsmjehivahu. No on ih sve izbaci, uzme sa sobom djetetova oca i majku i svoje pratioce pa uđe onamo gdje bijaše dijete.
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
41Primi dijete za ruku govoreći: "Talita, kum!" što znači: "Djevojko! Zapovijedam ti, ustani!"
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
42I djevojka odmah usta i poče hodati. Bijaše joj dvanaest godina. I u tren ostadoše zapanjeni, u čudu veliku.
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.
43On im dobro poprijeti neka toga nitko ne dozna; i reče da djevojci dadnu jesti.